Viongozi wafuatao washitakiwe, aidha wako kwenye madaraka au wamestaafu

Viongozi wafuatao washitakiwe, aidha wako kwenye madaraka au wamestaafu

Mwamuzi wa Tanzania

JF-Expert Member
Joined
Apr 7, 2020
Posts
15,486
Reaction score
45,256
Habari,

Kama taifa ni vyema tukaishi kwa misimamo thabiti. Ni vizuri tukaanza kuwajibishana bila kuoneana aibu ili kuleta fundisho kwa vizazi vya sasa na vile vinavyokuja.

Napendekeza viongozi wafuatao washitakiwe haraka, maana wamelitia taifa hasara.

1. Waziri wa maliasili na katibu mkuu wa wizara ya maliasili.
Washitakiwe kwa kosa la matumizi mabaya ya ofisi.

Je, ilikuwa sahihi kutumia fedha kuhamishia wanyama Hifadhi ya Burigi-Chato huku hifadhi nyingi ambazo tayari zina wanyama wa kutosha zinakosa fedha za miundombinu bora?

Waliohusika wote wafunguliwe kesi ya uhujumu uchumi.

2. Mkurugenzi mkuu wa TAA
Mkurugenzi mkuu wa Mamlaka ya Viwanja Vya Ndege ( TAA) .
Huyu afunguliwe mashitaka ya matumizi mabaya ya ofisi.

Aliidhinishaje fedha nyingi zikajenge Chato Airport ambayo hatukuwahi kuona impacts zake za kiuchumi hapo awali na kuacha kuboresha Viwanja vya mikoa ambavyo vilikuwa miaka mingi? Atuelezee je, backup ya gharama zilizotumika kuujenga ule Uwanja zitapatikanaje?

3. Mkurugenzi mkuu wa TRC.
Huyu afunguliwe mashitaka ya matumizi mabaya ya ofisi.

Kwanini hajatumia trilioni 2 kuboresha na kufufua shirika la reli kwa kununua mabehewa na vichwa vipya, kukarabati njia na vituo vya reli na badala yake yametumika ma trilioni kutujengea reli ya mwendokasi ambayo yataathiri watoto wetu?

4. Waziri wa maji.
Mawaziri waliohudumu wizara hii kwa kipindi kirefu wafunguliwe mashitaka .

Waeleze kwanini wameshindwa kusambaza maji kwa wananchi kwa 100% wakati tuna maziwa, mito na bahari.

N.k
N.k
 
Hivi unajua kuwa kama serikali ingetumia kati ya trilioni 1-2 kukarabati reli za zamani tungenufaika zaidi kuliko huu mradi wa masifa wa treni za mwendokasi?
Dunia nzima unahama kwenye mfumo wa reli ya zamani sio matakwa ya ccm ni makubaliano ya biashara za kimataifa na hii sgr inaunga mpaka Rwanda Burundi congo nk Kenya tayari Uganda inajiandaa.
 
Hakuna kosa lolote la kumfunga mtu hapo , punguza Tu mihemko uendelee kulala, makosa yako yote mhusika mkuu ni Maghufuli , nenda kamfufue umpeleke mahakamani
 
Hakuna kosa lolote la kumfunga mtu hapo , punguza Tu mihemko uendelee kulala, makosa yako yote mhusika mkuu ni Maghufuli , nenda kamfufue umpeleke mahakamani
Uko sahihi kabisa. Makosa yote yalifanywa na marehemu. Na kwa bahati mbaya marehemu akishaondoka, ndiyo basi tena. Kila kitu kinazikwa naye.
 
Na waziri wa ujenzi akamatwe mara moja kwa kutujengea interchange stend ya mabasi ya magufuri ya mbezi na pia kujenga daraja la busisi, pia ujenzi wa bwawa la umeme .kenge wewe
 
Punguza mihemko ya kijinga..huko Chato kuna waTanzania pia na wala mkoa wa Geita haukua na uwanja a ndege kama kwingineko

Chuki zetu ni za kipuuzi sana
 
Haya ainisha gharama zilizotumika kuujenga ule Uwanja wa ndege wa Chato na onyesha flights zinazoanzia au kupita pale per day.
Mwisho wa siku utajikuta unatetea ukichaa wako.
Wananchi wa Chato wana ndege?
Kwa thanani ya uwanja ule ni sahihi kutagia popo?
Punguza mihemko ya kijinga..huko Chato kuna waTanzania pia na wala mkoa wa Geita haukua na uwanja a ndege kama kwingineko

Chuki zetu ni za kipuuzi sana
 
Hivi unajua kuwa kama serikali ingetumia kati ya trilioni 1-2 kukarabati reli za zamani tungenufaika zaidi kuliko huu mradi wa masifa wa treni za mwendokasi?
Wangeifanyaje sasa kwa pesa hizo maana hakuna speed, acha sgr ijengwe bana, kwangu mimi wangelitemana na ndege wakapambana na sgr ifike mwanza tu.
 
Waziri Mkuu,kwakutudanganya Rais wetu kipenzi yupo poa anasoma Mafaili,Kumbe either alikuwa anapumulia Mipira au Kwenye chumba cha Barafu.
 
Back
Top Bottom