Viongozi wasio na maono, weledi na ubovu wa mifumo unaifanya serikali kulipa watumishi wengi wasiokuwa majukumu ya kazi

Viongozi wasio na maono, weledi na ubovu wa mifumo unaifanya serikali kulipa watumishi wengi wasiokuwa majukumu ya kazi

Parabora

JF-Expert Member
Joined
Jul 6, 2019
Posts
1,504
Reaction score
2,203
Nasema hili nikiwa nimeliona katika ofisi nyingi za serikali baada ya kurudi likizo huko nyumbani, Serikali inatumia gharama nyingi sana kulipa mishahara na posho za watumishi lakini ni wachache sana, wachache mno wanaofanya kazi, wengi wao wanaripoti na kupiga soga mda wote wakiwa kazini ilimradi tu wamefika kazini na wamesaini na pengine sio kwamba wanapenda ni kutokana na ubovu wa sera na mifumo yetu, kiukweli mifumo mibovu ya serikali inachangia kwa kiasi kikubwa hii hali.

KWA NINI NASEMA HIVI
Kuna baadhi ya kada (vitengo) katika taasisi za umma kwa ofisi nyigi ambazo nilibahatika kuzitembelea havina majukumu tena lakini watumishi wake bado wanaendelea kuwepo na wanalipwa mshahara bila hata kufanya kazi yoyote kwa kipindi chote wanachokuwa hapo. Mfano: Labda taasisi A kipindi inaundwa ilikuwa na uhitaji wa watu wa masoko kulingana na maboresho na mabadiliko ya taasisi husika, kitengo hicho hakihitajiki tena kwenye muundo wa taasisi hiyo na kinavunjwa lakini watumishi wa kada yake wanaendelea kuwepo bila majukumu huku wakila mishahara bila kufanya kazi.

Wao wanafika na kusaini tu then wanaendelea na majukumu yao bnafsi, wakati kuna sehemu taasisi nyingine kuna uhitaji wa kada hiyo, kwanini hizi taasisi wasiwe wanawasiliana na utumishi wawapangie sehemu zenye uhitaj?

Ukitembelea taasisi za serikali kuna rasimali watu hazitumiki ipasavyo huku wakiwa wanakula mishahara kama kawaida, na wengine wamekuwa frustrated kutoka na roho mbaya za viongozi wao wasiokuwa na karama za uongozi. Just imagine mtumishi anataka kubadilisha kituo ch kazi kutoka mkoa A kwenda mkoa B ofisi hiyo hiyo na ana sababu za msingi kabisa badala ya kusikilizwa anapuuzwa na anapotelekeza majukumu yake chini ya kiwango anawekwa benchi huku mshahara anaendelea kupata na stahiki zake zingine. Hapa viongozi waliopewa madaraka ya kusimamia hizi taasisi huwa inamkomoa nani?

Just Imagine, serikali imefuta kada ya ulinzi katika taasisi zake nyingi za umma na tenda wamepewa SUMA JKT, lakini wale walinzi walioajiriwa wapo na hawana majukumu wanaingia ofisini wanachati tu na kupiga story mda wote na mda wa kuondoka ukifka wanaondoka ama wanatumika katika majukumu wasiyoyamudu kiasi kwamba hawaleti ufanisi unaotakiwa, huwa najiuliza kwa nini utumishi isingewasambaza hawa security katika taasisi zinazohitaji hiyo kada kama TPA, KADCO, TAA, TANAPA, UDSM, MUHAS, SUA na kwingineko ili wakaongeze nguvu kuliko kulipwa mishahara huku wakiwa hawana kazi za kufanya, Ukiangalia bandari zipo nyingi ukiachana na ya Dar, Tanga na Mtwara zipo za Kigoma, Mwanza, Rukwa, Bukoba, Geita, Musoma na kwingineko.

Na viwanja vya ndege vipo vingi karibia kila mkoa na hata watumishi wa kada hiyo hawatoshi ni wachache hali inayopelekea kuwa na usalama duni hasa kwenye airport nyingi, TANAPA kwenye hifadhi ndio usiseme kwa nini hawa watu wasiende kuongeza nguvu huko kuliko kuwalipa mishahara bila kutekeleza majukumu yao, yaani mtu anaenda kazini kupiga stori tu na umbeya unamlipa mshahara. Utumishi inaweza kuwa ni wizara mbovu kabisa hapa nchini, yaani unalipa kada ya ulinzi mara 2 kwa SUMA JKT wanaofanya kazi na walioajiriwa ambao hawana tena majukumu yao ya kufanya huku wakiwa kwenye payroll.

Kuna haja hata ya kuwahamisha walimu walioomba uhamisho walio na sababu za msingi kabisa kwenda kwenye vituo walivyoomba, kuwakatilia ni kuwatengenezea msongo wa mawazo na hata kazi za kufundisha hawatafanya kwa ufanisi.

Sio mwandishi mzuri, lakini ninachojaribu kusema serikali ina mfumo mbovu sana inalalamika haina watumishi wakati huohuo vijana wako mtaani hawawaajiri na wengine wametelekezwa bila majukumu wanakula mishahara ya bure wakati wangeweza kutumika sehemu zenye uhitaji na wakaongeza ufanisi na sijui kazi ya Wizara ya Utumishi wa Umma huwa ni nini hasa?
 
Parabora,
Ndugu parabora wewe kweli ni mzalendo, nathubutu kusema ni mzalendo namba 3 baada ya Mwalimu Nyerere na mimi. Ulichoeleza humu ni ukweli mtupu, wapo watumishi wengi sana wanaolipwa mishahara na marupurupu mengi tu na hawana kazi yoyote isipokuwa wanaujua unafiki/usanii vizuri. Na kwa sababu hatuna uongozi makini au mfumo mzuri hatulioni hili.

Nashauri kura ya maoni ya wazi kwa wananchi utaona matokeo wataisaidia sana serikali. Watumishi hewa walioondolewa tunaipongeza serikali ingawaje walioondolewa ni wale Mshika mpini aliotaka kuwaondoa na si hewa wote zaidi ya 60% hawakuguswa.Hongereni wa TZ
 
MANILABHONA,
Mkuu serikali ni moja hawa watu ambao hawana majukumu ya kufanya katika taasisi A ni bora wakahamishiwa taasisi B ILIYO na uhitaji ili wakafanye na majukumu yao ya kujenga taifa kuliko kuwalipa mishahara na posho bila kufanya kazi, Hii ni kwa sababu nchi ina mifumo mibovu na hakuna anaejali
 
Depal na wewe inabidi uhamishwe😀
Nifanyie mpango basi na mm nije Serikalini...huku kwetu unafanya kazi mpaka kazi zenyewe zinakufanya.
Imagine mtu unaSign in 7:30 Am kuja kutoka 17:00 PM bado kuna zile Fanya hiki Fanya kile ukija kumaliza saa 18:30 hiyoo.
Nihamishe huku basi 😀😀
 
Nifanyie mpango basi na mm nije Serikalini...huku kwetu unafanya kazi mpaka kazi zenyewe zinakufanya.
Imagine mtu unaSign in 7:30 Am kuja kutoka 17:00 PM bado kuna zile Fanya hiki Fanya kile ukija kumaliza saa 18:30 hiyoo.
Nihamishe huku basi 😀😀
😳😳😳kumbe wew mvivu
 
Tanzania anaefanya kazi ni Rais.

Wengine wanasubiria MATAMKO.
 
Ni kazi rahisi sana kuongeza ufanisi Serikalini na kwenye mashirika ya umma basi ndio vile tu tunapenda kuchekeana na kusaidiana saidiana siku ziende maana maisha yetu haya tunafahamiana.

  1. Kila ofisi lazima iwe na biometric machine kwa wafanyakazi kupunch in and out.
  2. Kila ofisi lazima iwe na Job Card ambazo kila mtu anapewa asubuhi ajaze masaa aliyofanya kazi na kazi husika.
  3. Tupunguze ajira za moja kwa moja, baadhi ya kazi ziwe kwa masaa na watu walipwe kwa masaa waondoke.
  4. Kila bosi kila ofisi apewe target na kuwe na mfumo wa kumuasses na kujiasses mwenyewe.
  5. Kila Mfanyakazi kila mwaka awe assesed mara mbili mpaka tatu kwa mwaka.
  6. Tea break iwe nusu saa na wawe wanapunch out and in na huo uwe muda wao sio wa mwajili GOVT.
  7. Lunch time iwe lisaa limoja na usiwe muda wa mwajili na punch in and out kama kawaida.
  8. Masaa ya kazi manane kuanzia saa mbili mpaka saa kumi na moja na nusu plus ule muda wa kula lisaa na nusu.
  9. Baadhi ya vyeo marufuku kuendeshwa lazima ujiendeshe mwenyewe hapa dereva tunamtoa.
TANZANIA NI NCHI MASIKINI SERIKALI IANGALIE UWEZEKANO WA KUONGEZA MASAA YA KAZI WATU WAANZE KAZI SAA KUMI NA MBILI NA KUTOKA SAA KUMI NA MBILI JIONI KWA MAANA YA MASAA KUMI NA MBILI KWA SIKU.
BARABARA ZOTE ZIFAGILIWE USIKU NA WAFAGIAJI WALIPWE KWA MASAA, MAHOSPITALI YOTE YA UMMA YAFAGILIWE USIKU NA WAFAGIAJI WALIPWE KWA MASAA..
 
Masaa ya kazi yaongezwe yafikie kumi na mbili kwa siku, Umri wa kustaafu uwe miaka 45.
Elimu ya msigi iwe miaka mitano, na sekodari minne tu, form six ifutwe watu wote waende College.
Shule watoto waanze na miaka mitatu, hapa ustawi na jamii na wizara ya afya wahusike juu ya Lishe za watoto, mama wajawazito na jamii kwa ujumla ili watoto wote waanze kuelewa kuanzia miaka mitatu.
 
Vijana wote wasio na ajira waandikishwe jeshini haraka, Jeshi lianze uzarishaji mali mkubwa kuanzia ujenzi wa majumba, madaraja, vivuko, mashamba ya kisasa, karakana za vipuri mbali mbali, mahospitali, viwanda vya madawa vya jeshi, research center's chini ya jeshi, Magari ya kijeshi, silaha za kivita nk

Jeshi la polisi lifutwe, baadala yake iwe kitengo chini ya JWTZ, na polisi wote wawe sehemu ya jeshi aka jeshi la akiba incase of war nao ni sehemu ya JWTZ kulinda uvamizi wa ndani na JWTZ wanabaki mipakani na kupambana na adui wa nje..

Hivyo pia vikifanyika tunaweza kuwa na jamii yenye ufanisi na kujielewa.
 
Ni kazi rahisi sana kuongeza ufanisi Serikalini na kwenye mashirika ya umma basi ndio vile tu tunapenda kuchekeana na kusaidiana saidiana siku ziende maana maisha yetu haya tunafahamiana.

  1. Kila ofisi lazima iwe na biometric machine kwa wafanyakazi kupunch in and out.
  2. Kila ofisi lazima iwe na Job Card ambazo kila mtu anapewa asubuhi ajaze masaa aliyofanya kazi na kazi husika.
  3. Tupunguze ajira za moja kwa moja, baadhi ya kazi ziwe kwa masaa na watu walipwe kwa masaa waondoke.
  4. Kila bosi kila ofisi apewe target na kuwe na mfumo wa kumuasses na kujiasses mwenyewe.
  5. Kila Mfanyakazi kila mwaka awe assesed mara mbili mpaka tatu kwa mwaka.
  6. Tea break iwe nusu saa na wawe wanapunch out and in na huo uwe muda wao sio wa mwajili GOVT.
  7. Lunch time iwe lisaa limoja na usiwe muda wa mwajili na punch in and out kama kawaida.
  8. Masaa ya kazi manane kuanzia saa mbili mpaka saa kumi na moja na nusu plus ule muda wa kula lisaa na nusu.
  9. Baadhi ya vyeo marufuku kuendeshwa lazima ujiendeshe mwenyewe hapa dereva tunamtoa.
TANZANIA NI NCHI MASIKINI SERIKALI IANGALIE UWEZEKANO WA KUONGEZA MASAA YA KAZI WATU WAANZE KAZI SAA KUMI NA MBILI NA KUTOKA SAA KUMI NA MBILI JIONI KWA MAANA YA MASAA KUMI NA MBILI KWA SIKU.
BARABARA ZOTE ZIFAGILIWE USIKU NA WAFAGIAJI WALIPWE KWA MASAA, MAHOSPITALI YOTE YA UMMA YAFAGILIWE USIKU NA WAFAGIAJI WALIPWE KWA MASAA..

IDEA Nzuri ila Tanzania tuko kama hatuna vipaumbele.
 
NIKUJIBUNI? Jibu ni kwamba wakolononi hawakuturuhusu tubadili mambo yetu ni mwiko.Hebu ona! Kikwete alibadiri mfumo wa elimu msingi uwe miaka sita, kaingia bwana mkubwa karudisha miaka saba.Uganda,Kenya,rwanda nasikia miaka 6.Wenzetu Zanzibar wapo kwenye mchakato wa kurekebisha mtaala iwe miaka sita.
Serikali yetu haijawahi kaa na kupima tija za idara mbalimbali walizorithi kwa wakoloni.
Ofisi ya kijiji ina mtendaji wa kijiji,mwenyekiti wa kijiji bwana shamba kijiji.Mabwana shamba wana shughuli gani hasa zinazowaweka ofisini.Nimelima miaka mingi sijawahi muona bwanashamba mashambani kwangu.Bwana shamba angeweza kupewa afanye kazi za kilimo na utawala mtendaji aondolewe.
Ofisi ya kata kuna diwani,mtendaji,bibi maendeleo,bwana shamba,mratibu elimu kata,bibi afya nk.Hawa wote wanafanya nini!!Majukumu wanayofanya walimu wakuu yangeweza kusimamiwa na maafisa elimu kwa kutumia mifumo ya kisasa ya mitandao badaka ya waratibu kata
Mtendaji kata angeweza kuratibu na kufanya kazi za watendaji wa kijiji akishirikiana na diwani.ukweli ni kwanba tunatakiwa tufanye research juu ya uwepo au kufutwa kwa hizo idara kichaa zisizo na tija.Tuidara twingi lakin hali huko vijijini ni mbaya kabisa.Baadhi ya idara zipo kulinda maslahi ya siasa tu sio kwa ajili ya kuleta maendeleo Natamani mtu afanye PhD kuchunguza hizi idara zetu na tija zake.Serikali inatakiwa iwe inatathmini mifumo yake kila baada ya miaka kadhaa na kufanya mabadiriko makubwa.
 
Nasema hili nikiwa nimeliona katika ofisi nyingi za serikali, Serikali inatumia gharama nyingi sana kulipa mishahara na posho za watumishi lakini ni wachache sana, wachache mno wanaofanya kazi, wengi wao wanaripoti na kupiga soga mda wote wakiwa kazini ilimradi tu wamefika kazini na wamesaini na pengine sio kwamba wanapenda ni kutokana na ubovu wa sera na mifumo yetu, kiukweli mifumo mibovu ya serikali inachangia kwa kiasi kikubwa hii hali.

KWA NINI NASEMA HIVI
Kuna baadhi ya kada (vitengo) katika taasisi za umma kwa ofisi nyigi ambazo nilibahatika kuzitembelea havina majukumu tena lakini watumishi wake bado wanaendelea kuwepo na wanalipwa mshahara bila hata kufanya kazi yoyote kwa kipindi chote wanachokuwa hapo. Mfano: Labda taasisi A kipindi inaundwa ilikuwa na uhitaji wa watu wa masoko kulingana na maboresho na mabadiliko ya taasisi husika, kitengo hicho hakihitajiki tena kwenye muundo wa taasisi hiyo na kinavunjwa lakini watumishi wa kada yake wanaendelea kuwepo bila majukumu huku wakila mishahara bila kufanya kazi.

Wao wanafika na kusaini tu then wanaendelea na majukumu yao bnafsi, wakati kuna sehemu taasisi nyingine kuna uhitaji wa kada hiyo, kwanini hizi taasisi wasiwe wanawasiliana na utumishi wawapangie sehemu zenye uhitaj?

Ukitembelea taasisi za serikali kuna rasimali watu hazitumiki ipasavyo huku wakiwa wanakula mishahara kama kawaida, na wengine wamekuwa frustrated kutoka na roho mbaya za viongozi wao wasiokuwa na karama za uongozi. Just imagine mtumishi anataka kubadilisha kituo ch kazi kutoka mkoa A kwenda mkoa B ofisi hiyo hiyo na ana sababu za msingi kabisa badala ya kusikilizwa anapuuzwa na anapotelekeza majukumu yake chini ya kiwango anawekwa benchi huku mshahara anaendelea kupata na stahiki zake zingine. Hapa viongozi waliopewa madaraka ya kusimamia hizi taasisi huwa inamkomoa nani?

Just Imagine, serikali imefuta kada ya ulinzi katika taasisi zake nyingi za umma na tenda wamepewa SUMA JKT, lakini wale walinzi walioajiriwa wapo na hawana majukumu wanaingia ofisini wanachati tu na kupiga story mda wote na mda wa kuondoka ukifka wanaondoka ama wanatumika katika majukumu wasiyoyamudu kiasi kwamba hawaleti ufanisi unaotakiwa, huwa najiuliza kwa nini utumishi isingewasambaza hawa security katika taasisi zinazohitaji hiyo kada kama TPA, KADCO, TAA, TANAPA na kwingineko ili wakaongeze nguvu huko maana ukiangalia bandari zipo nyingi ukiachana na ya Dar, Tanga na Mtwara zipo za Kigoma, Mwanza, Rukwa, Bukoba, Geita na kwingineko.

Na viwanja vya ndege vipo vingi karibia kila mkoa na hata watumishi wa kada hiyo hawatoshi ni wachache hali inayopelekea kuwa na usalama duni hasa kwenye airport nyingi, TANAPA kwenye hifadhi ndio usiseme kwa nini hawa watu wasiende kuongeza nguvu huko kuliko kuwalipa mishahara bila kutekeleza majukumu yao, yaani mtu anaenda kazini kupiga stori tu na umbeya unamlipa mshahara. Utumishi inaweza kuwa ni wizara mbovu kabisa hapa nchini, yaani unalipa kada ya ulinzi mara 2 kwa SUMA JKT wanaofanya kazi na walioajiriwa ambao hawana tena majukumu yao ya kufanya huku wakiwa kwenye payroll.

Kuna haja hata ya kuwahamisha walimu walioomba uhamisho walio na sababu za msingi kabisa kwenda kwenye vituo walivyoomba, kuwakatilia ni kuwatengenezea msongo wa mawazo na hata kazi za kufundisha hawatafanya kwa ufanisi.

Sio mwandishi mzuri, lakini ninachojaribu kusema serikali ina mfumo mbovu sana inalalamika haina watumishi wakati huohuo vijana wako mtaani hawawaajiri na wengine wametelekezwa bila majukumu wanakula mishahara ya bure wakati wangeweza kutumika sehemu zenye uhitaji na wakaongeza ufanisi na sijui kazi ya Wizara ya Utumishi wa Umma huwa ni nini hasa?
Ni kweli kabisa. Nenda kwenye mashirika ya umma, sehemu ambayo kazi inaweza kufanywa na MTU mmoja kuna watu watano, na wanalipwa overtime. Kama hamuamini undeni tume, kwa kweli mtaona ni maajabu makubwa. Sehemu nyingi ni za mikoani hasa mashirika makubwa
 
Nifanyie mpango basi na mm nije Serikalini...huku kwetu unafanya kazi mpaka kazi zenyewe zinakufanya.
Imagine mtu unaSign in 7:30 Am kuja kutoka 17:00 PM bado kuna zile Fanya hiki Fanya kile ukija kumaliza saa 18:30 hiyoo.
Nihamishe huku basi 😀😀
hapo kwenye kufanya kazi hadi zinakufanya daaaa atar
 
Mleta mada umegusa panapo...
Ukienda pale DSM kwenye kila Halmashauri kuna Maafisa Nyuki, wakati Dsm nzima hakuna hata mzinga wa nyuki. Kuna Injinia wa Kilimo cha Umwagiliaji wakati hata Skimu hakuna Yaaani kuna vyeo lukuki ambavyo ukitafakari bandiko lako lina mantiki.
Nikwambie ukweli wazo lako lina mashiko, limesemwa sana lkn tatizo anayelisema ni nani sasa, ana nini!
 
Hata Mimi huwa nashangaa sana! Katikati ya jiji mfano Dodoma kuna maafisa uvuvi wakati hakuna bahari/ziwa! Maafisa nyuki! Hao nyuki wanafugwa mjini? Maafisa misitu mi naona majumba tu kwenye majiji misitu imetoka wapi? Maafisa umwagiliaji mijini! Wazimamoto kila wilaya wakati mioto haipo, na ikitokea bado hawezi kuzima! Watasema hatuna maji/vifaa sasa serikali hawa watu nyie wanawasaidia nini? Yaani huwa najiuliza sipatagi majibu!
 
Back
Top Bottom