Viongozi wasio na maono, weledi na ubovu wa mifumo unaifanya serikali kulipa watumishi wengi wasiokuwa majukumu ya kazi

Mkuu maoni yako ni mazuri mno, kwa ninavyojua ofisi nyingi sasa zina punching machine za kusign in and out.

Sasa tatzo ni hapa kwenye assessment kama unavyosema, kwa mfano idara ya Estate imefutwa na Kuna watumishi bado wapo na ni maengineer by professional, na mshahara anakula na allowance huku akiwa hana majukumu.. hapa utamfanyia vipi assessment wakati majukumu yake tayari hayapo kwenye taasisi?

Hawa walinzi ambao mheshimiwa raisi aliagiza serikali isiajiri tena na badala yake watumie wa kampuni ya SUMA JKT, still waliokuwa wameshaajiriwa wako wanakula mshahara ila hawalindi wanalinda wa kampuni ya Suma... Huyu utamfanyia vipi assessment wakati majukumu yake hafanyi? Au kapangiwa majukumu ambayo haendani nayo ana anaperfom chini ya kiwango utamchukulia hatua?

Hapa solution ilikuwa ni kupelekwa sehemu watakazofanya kazi za kada zao....

Umri wa kustaafu miaka60 bado naona sio mbaya mengine yote uko sawa kabisaa mkuu
 
Mkuu usisahau na mlundikano wa vyeo huku mikoani yaani.

Mkuu wa Mkoa
Mkuu wa wilaya
Katibu tawala wa Mkoa
Katibu tawala wa wilaya
Mkurugenzi
Meya
Mbunge
Diwani
Mtendaji
Mwenyekiti wa serikali ya mtaa

Tungeweza kuangalia upya muundo wetu wa utawala ili tubadilike tusiishi tu kwa mazoea.
 
Tanzania hii Kuna mambo yanasikitisha sana
 
Mkuu bora hao wanafanya kazi Kuna watu hawafanyi kazi kabisa zaidi ya kusign na kusoma magazeti, kupiga umbeya na kuperuzi mtandaoni kwa computer za ofisi na mshahara wanakula
 
Hahaha
 
Hahaha matumizi mabaya ya rasimali watu
 
Mifumo mibovu ya serikali ya kijani..ndo matokeo yake haya...Afisa nyuki mjini ana majukumu Gani!! kwa Nini wasipelekwe mahali Wana Tija wakaongeze utendaji!! PhD zetu zinapaswa kuchunguzwa..hiyo mishahara ingepelekwa kwenye miradi ya uzalishaji Ingekuwa na Tija...
 
Ushauri wa kitoto sana huu
 
Nakubaliana na wewe mkuu
 
Si unalipwa vizuri shida nn
 
Unashangaa hao MBONA majeshini wako iddle wanasubiria hadi vita au operations ndio wapige Kazi hapo vipi tutasema nao awafanyi Kazi
 
usisahau mishahara na maslahi ya watumishi yaboreshwe
 
Unashangaa hao MBONA majeshini wako iddle wanasubiria hadi vita au operations ndio wapige Kazi hapo vipi tutasema nao awafanyi Kazi
Wewe jamaa umefikiria vizuri kweli?
 
Hicho ulicho eleza tofauti na mtoa mada. Mtoa mada anasema kutokana na mifumo mibovu ya utumishi serikali kuna watu hawana majukumu wanakula mishahara ya bure. Jambo ambalo ni kweli, wapo wanao wahi kazini na kuondoka muda unaotakiwa lkn hakuna cha maana wanachofanya zaidi ya kwenda kwenye chai na baadaye kwenye lunch na kusubiri saa za kurudi nyumbani.
 
Kabisa mkuu.
 
Naunga mkono hoja nadhani serikali yetu sikivu watendaji wote wakuu wangeenda kujifunza namna makampuni ya watu binafsi wanvyofanya kazi hata ikibidi waende kuangalia ofisi za mabalozi wa nje waliopo nchini wanavyochapa kazi. Sehemu nyingine hata kuongea na simu binafsi ni shida lakini ofisi za uma hapa kwetu wanaongea na simu binafsi bila aibu hata kama mteja anataka kuhudumiwa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…