Hongereni wakuu,
Hii kwa mtazamo wangu ingekua hadithi ya kisiasa ingependeza sana.
Mfano,(post ya kwanza) Mwanakijiji anataka uongozi lakini kutokea upinzani lakini tayari wenye madaraka yaani ccm wanadai wao kuongoza milele kama wafanyavyo sasa.Anawaambia uongozi ni wa yoyote tu mwenye ridhaa ya wananchi (wanawakirishwa na ndege kwenye shairi),sasa manza inaanzia hapo anadai nia na hari (manati) anayo ya kupata hicho anacho taka huyo ndege (uongozi).
Post ya pili,anapata na mashabiki pia kwamba watamwezesha na kwamba wenyewe (ccm) habari wamepata kwamba sasa kazi ipo.
Post ya tatu,Mwanakijiji anajitutumua na kuleta mbwembwe mbele ya wapambe kwamba anaweza.
Post ya nne,Duh!wenyewe wanamjibu mwanakijiji,kwamba asijisumbue uongozi ni wao siku nyingi na hilo halina shaka kwanza yeye Mwanakijiji uongozi (ndege) wala hafanani nao ila wao tu "wagombea".Tena wanamwambia ,kweli nia ya uongozi unayo ila wewe bado mwanafunzi nenda kajifunze tena kwao.
Salale,kumbe Mwanakijiji hayuko pekeyake anayetaka kua na huyo ndege,wako wengine,Bwn.Mswahili pia anasema wamwachie yeye kwani sio yeye mwanakijiji wala mgombea anayestahiri huyo ndege yeye pekee yake ndio mahususi.Anadai yeye sikunyingi ndege wake yeye ila wao tu wanamtolea macho,basi wamuaachie huo ungozi yeye kwani ndio anafaa,kwanza mfano yeye Mwkjj,kapelekwa shule na yeye Mswahili kwa kutumia ndege huyo huyo asione gele.
Inakua kama hari sio shwari kati ya Mgombea na Bwn. mswahili inavyoonekana wanatoka kwenye chama kimoja,ila sasa kuna mgongano wa kimaslai na mawazo pia wanagombana wenyewe kwa wenyewe.Ila inaonekana mgomea ananguvu kweli kweli chamani huko,anamwambia Bwn.mswahili asithubutu kutaka kisichokua chake na huyo Mwkjj bora yeye aendelee kuandika habari tu magazetini na kwenye wavuti.
Pia nawapuuza wote wale wanaoshangilia na kushabikia yasio wahusu,mfano Bwn Abi,mwawado na bwn bosi.
Bwn.Abi hakubari anadai yeye pia anaweza kumpata ndege na,yeye mgombea sio lolote ,basi kamavipi wakae wote wasubiri nani ndege (sasa hapa ndege ,watakua wananchi) atamchagua.
Lakini mwisho wa yote mgombea hakubarivijana wamshinde anawaambia,wanyamaze tu kwani wanapika makelele na kupoteza nguvu zao kwa jambo ambalo yeye anajua ni la kwake na wao ni wadokozi tu wanataka kuvamia mambo yasio wahusu.kwani wao bado vijana hawaju wakitakacho,kesho kesho kutwa wataacha uongozi kwenda fata jambo lingine vision ikapote.
Huo ni mtazamo wangu tu wa kifasihi kutokana na beti za wahusika,hazihusiani na chochote kama hicho kwenye maana harisi ya tungo za wenyewe hao .
Ni hadithi tu nimeipata hapo hapo