Vipi mke wa kutafutiwa anaweza kudumu kwenye ndoa?

Vipi mke wa kutafutiwa anaweza kudumu kwenye ndoa?

Prakatatumba abaabaabaa

JF-Expert Member
Joined
Aug 2, 2022
Posts
1,842
Reaction score
6,087
Mshikaji wangu baada ya kunusurika kwenye ajali nyingi na misukosuko ya mahusiano ikabidi aanze kushirikisha watu Ili apate mke sahii wa kuoa.

Kwenye harakati hizo huku akiendelea kumuomba Mungu (Kwa mujibu wake), jamaa yake mmoja aliepo kigoma akamwambia Kuna Binti anamuona kanisani na inaonekana katulia, jamaa akafunga safari kutoka Dodoma mpaka kasulu vijijini kwenda kumuona mchumba 😁😁.

Kufika huko akakutanishwa na mchumba, jamaa ananiambia binti sio mzuri sana akimaanisha sio yule akipita watu wote lazima wamuangalie, ni binti wa kawaida tu, wala sio mbaya heshima hiko asilimia 99.99 kwa jinsi alivyomuona.

Jamaa akamuuliza kuhusu habari za washikaji zake binti wa nyuma binti akamuhakikishia yuko bikira, yaani tokea kuzaliwa hajawahi kuguswa. Aliniambia alimuuliza maswali mengi ya kiintelijensia lakini binti licha ya kua ni wakijijini sana lakini alijibu maswali vizuri.

Mwisho wa siku jamaa akakata shauri ya kumuoa kabisa na hapa tumeshaungwa kwenye group la whatsapp ya harusi. Ndoa inafungwa mwezi wa 8 huko.

Imenifanya nitafakari kidogo, hivi hawa wanawake wa kutafutiwa wanadumu kweli? Mimi nadhani upendo wa kweli lazima umuone mwanamke/mwanaume ndio umpende ukishampenda ndio unakata shauri.
 
Mshikaji wangu baada ya kunusurika kwenye ajali nyingi na misukosuko ya mahusiano ikabidi aanze kushirikisha watu Ili apate mke sahii wa kuoa...
Upendo unajitengeneza kutegemeana na wahusika walivyo. Hata hao unaojitafutia, mwanzo Kila mmoja anakuwa ni stranger kwa mwingine.

Kama jamaa katika Dar kuifata mali Kigoma, hiyo itakuwa chachu ya kudevelop upendo.
 
Najibu kichwa cha habari!

Inategemeana, inaweza kudumu au isidumu.

Vijijini kutafutiwa ni jambo la kawaida na zinadumu vizuri tu.

Wengi wenye exposure ukiwaambia nitafutie watakataa kuepuka lawama endapo ndoa isipokuja kudumu.
Jamaa alitest akakuta kitu sealed, anasema binti alimwambia niko tayari tusex lakini unioe,
 
Mshikaji wangu baada ya kunusurika kwenye ajali nyingi na misukosuko ya mahusiano ikabidi aanze kushirikisha watu Ili apate mke sahii wa kuoa...
Nikiangalia ndoa za wahindi walioko Marekani zinadumu sana na wanaheshimiana sana katika ndoa; wao hutafutiwa wenza na wazazi wao huko kwao.

Arranged marriages zinaweza kuwa ni nzuri zaidi ya hizi za kukutana wenyewe, kwani kila mnapotaka kukorofishana mnajikuta mnajisuta kwa kuwaheshimu wale waliowasaidia katika kupanga hiyo ndoa yenu.
 
Jamaa alitest akakuta kitu sealed, anasema binti alimwambia niko tayari tusex lakini unioe,
Kwa nini asingemwambia amuoe ndipo waanze safari ya kujimwaga.

Mambo yashabadilika lakini sisi wenyewe tunayafosi kubadilika hata kama bado yako vile vile.

NB: Sio kila kitu cha kukibadili, kitu kama kizuri hata cha zamani kibaki vile vile.

Hivi Brand ya Kalamu ya BIC si iko vile vile tangu miaka ya 1950 hadi sasa, na ubora upo vile vile
 
Back
Top Bottom