Soma uislamu uelewe.Mtume Muhammad hana ugomvi na Yesu.Mtume Muhammad ni Mtume wa Allah na na Yesu ni Nabii wa Allah.Hawana ugomvi.Tatizo lako wachanganya mambo katika uislamu.Hakuna mahali Mtume Muhammad na Yesu watapigana.
Katika uislamu,siku Yesu alipokuwa anataka kusulubiwa,aliomba kwa Mungu,amuepushe na kikombe kile cha umauti.Aliomba sana.Mungu akamkubalia ombi lake,akamuokoa kumchukuwa mbinguni,hawakumsulubu wala hawakumuuwa,hayo ndio maelezo ndani ya Qur'an.Fikiria ikiwa Yesu,aliomba kikombe cha kifo kimuepuke na Mungu hakumkubalia,kwa nini asimkubalie?Kumbuka Yesu aliomba sana.Na aliyoko mbinguni hai si Yesu tu,hata Enock,ambaye alichukuliwa na upepo wa kisuli suli(naye pia wakati wake ukifika atakufa).Yaonyesha Biblia husomi na Qur'an unaitafuta kwenye website za maadui wa uislamu.Wanaopindisha ukweli.Katika uislamu sahihi hakuna mtu anayesubiriwa anayeitwa Mahad,hizo ni itikadi za wasio waislamu,wakajiita waislamu.Nina hakika itakuwa wafunguwa website zinazoanzishwa na wasiokuwa waislamu,wakajifanya ni website za uislamu.
Ni sawa muislam,afunguwe website ya Mormonism,kutafuta habari za ukristo.Kwa asiye jua ataona Mormonism ni wakristo wana musmini Yesu,lakini kumbe wako tofauti sana na ukristo.