Vipimo vya COVID19: Dr. Mwele na Dr. John Nkengasong(Africa CDC) walitumika kupotosha ukweli wa kisayansi (wasaka tonge kazini)

Ungejipambanua wewe ni Mzalendo bana na uko tayari kuonyesha kwamba Raisi wetu hakosei badala ya hizi blah blah babu lai... sijui PHD tueleze sisi wa la tatu B tuelewe basi na tuna swali wenzetu walijuaje vinakaa kwenye meza,chuma na vitu vingine kwa masaa kadhaa walitumia nini kujua ndo hiyo Swab au na walijuaje vinakaa hewani kwa masaa kadhaa haya ndo maswali yetu wa Darasa la tatu B na A...
 
Kitaalamu, maelezo uliyotoa yanaeleweka. Tatizo ni MUKTADHA.

1) Umeeleza vizuri kwamba kama kulikuwa na haja ya kutathmini ubora wa hizo mashine kwenye hiyo maabara, zipo njia rasmi kabisa za kufanya hivyo, hakuna haja ya kuleta oili au mapapai. Sasa imekuwaje hayo yamefanyika, shida ipo kwenye Muktadha wa kisiasa. Kupima oili na mapapai ni more sensational. Inapamba headline za magazeti. Pia jiulize lengo kuu la Magufuli. Hataki data za Tanzania za covid19 ziwekwe wazi. Sababu? Data zinaonesha Hypothesis za Magufuli zimekwama. Hivyo anatafuta sababu za kufanya UHAKIKI wa maabara, INDEFINITELY .

Unakumbuka kisingizio cha kwanza alichotoa Magufuli kukwepa ishu ya kuboresha mishahara ya wafanyakazi, ambayo ilikuwa ahadi yake katika kampeni 2015? UHAKIKI. Uhakikivwa wafanyakazi hewa. Alisema anaomba mwezi mmoja au miwili. Matokeo yake? Mwaka wa tano huu hakuna maboresho ya mishahara, ila bei za vitu na huduma zimepanda sana. Maisha Magumu. Uhakiki unaendelea. Mpaka sasa serikali haitoi taarifa za maambukizi. Kisaikolojia, wengi watachukulia kwamba korona imekwisha! Taifa linapoteza nguvu kazi, ali mradi ego ya Magufuli itunzwe.

2) Suala la ubovu wa vifaa ni administrative, nchi nyingi zimekutana na hiyo changamoto. Wameipatia ufumbuzi haraka tu na upimaji unaendelea, data zinatolewa, hadi tunaambiwa Malkia wa Uingereza kapata covid, waziri mkuu Boris naye kapata hadi kalazwa ICU. Sasa kwetu kuna kipya chepi?

3) Ukitaka kujua Magufuli kaficha mbuzi kwenye gunia, angalia anachora ardhi kwa vidole vya miguu, wanaume kina Kagame na Kenyata wanapomuita waongee kiume. Si angekutana nao tu akawaeleza Theories zake?
 
Muda huu wote tunaozozana kwamba Je why Papai, Je why Mbuzi, Je vipimo bomu, Je wataalam bomu, Je sample handling process hovyo nk huyu COVID-19 anatusubiria tumalize kwanza mzozo wetu?

Hakuna matokeo ya vipimo wala vifo hii wiki ya pili sasa, hii inatufanya tuanze kutengwa na mataifa jirani...

Je hii ni njia sahihi ya kupambana na COVID-19?

Watanzania tuna tatizo kubwa sana kwenye hii issue ya COVID-19 tukatae ama tukubali.
 
Anyway, kuua kirusi kwa fumigation ni kichekesho, virusi vinahitaji living cells ili kuendelea kuishi, fumigation inafanyika kwenye objects which does not necessarily host viruses.
Changamoto moja ya kujibu kwa kutumia tumbo..siku zote mda utakuumbua...mbili.....kuna kile kitu tunaita third part proof analysis...wewe kama mtaalam lazima ujue Ni bora kuamini taasisi 3 tofauti kuliko majibu ya mtu mmoja anayesubiri huruma ya watawala....unatia aibu
 
Sawa ila kwa kuwa maabara inachunguzwa ungeacha hii makala yako tusubirie taarifa ya kamati
Mzee maabara imeshachunguzwa na ripoti imeshakabidhiwa kwa wahusika, si ndio zililkuwa ToR za kamati ?
 
Sawa..Tungeomba akina Dr. Mwele nao waje watoe ya kwao on this.,
 
Mnafaid8ka na nini? Voltmeter inapimer voltage tu... haiwezi kupima kingine
 
The best way you would have done: weka hiyo story in a very good English na uipeleke Kwa institutions za kimataifa kama lancet, John Hopkins Equivalent etc, wafanye peer review tungeziona kokote zingechapishwa, hii ya kuja kuwalazimisha watu na kuwadharau ili wasome report yako umekosa ethics kabisa.

mkuu alivyoelezea hatusoma JF tu tumesoma hata majalada ya dunia. Unaweza kumaaidia kuondoa utatanishi
 
Kuendelea kusoma ambavyo huvijui. Karibu kwenye darasa letu la "Drug Design"
Kiongozi ungeeleza tu, maana hatujuani humu... kwa elimu wala uelewa.... NIAMBIE TU VOLTMETER INAPIMA NINI KINGINE..!?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…