Vipimo vya COVID19: Dr. Mwele na Dr. John Nkengasong(Africa CDC) walitumika kupotosha ukweli wa kisayansi (wasaka tonge kazini)

Uzi mreeeefuuuuu yaan nimesoma paragraph 2 nimeona hamna haja ya kuandelea kusoma maana napoteza mda wangu kusoma upumbavu tu,, kamwambie aliekutuma hatudanganyiki sisi sio wajinga

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hili ni shimbuko la watoto wa uwanja wa fisi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ahsante kwa kutambua hili, bila kuwasaidia wananchi, wanaopambana na mafanikio ya JPM watatuingiza shimoni kwa kutunga uongo kila kukicha
Wanaopambana na mafanikio, mabeberu??

C.C Kambaku

Hivi kwanini watanzania hatutaki kuwa positive? Kuna shida gani hivi, kwanini kila kiongozi akiongea lazima kuongelea swala la 'maadui zetu'? Watu gani kila saa mnawaza mna maadui tu jamani, badala ku focus kwenye issues kila mara ni kupeleka lawama kwa maadui, maadui hao 2020 maadui gani. Tunapoteza focus wakuu.

Tunakuwa kama watu wachawi bwana, mchawi ndio ambae hata ukimsalimia tu lazima atasema unamsalimia umdhuru. Haiwezekani tukawa na mawazo ya maadui tuuuuuuu kila siku na kila mara. Na bahati mbaya maadui wenyewe hawatajwi!

Utaambiwa tu maadui zetu, mara tupo vitani na maadui zetu mara vita za kiuchumi na mabeberu, hivi kweli kwenye nafsi zenu mnaamini mna vita na wamarekani au EU kwenye uchumi? Marekani aache kuwa na vita kiuchumi na wachina au warusi aje kuwa na vita na Watanzania, watu ambao hadi vyoo anawasaidia bure, angekuwa na vita na nyie angewapa dawa za ukimwi bure muendelee kuishi?

Angewapa vyandarua msiumwe na mbu msife na marelia, unawezaje kumsaidia adui yako vitani apone? Mnawaita mabeberu wana vita kiuchumi na nyinyi ila mnajua kabisa bajeti yenu ya mwaka asilimia 60 wanajazia pesa zao muweze hata kulipa mishahara yenu, tangu lini adui yako vitani akakusaidia uweze kuishi?

Hebu tuache sababu, tupambane na maisha yetu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mwakani utateuliwa....hahahhaaa sijui utachukua nafasi ya Polepole🤣🤣UDSM mnahendekeza njaa sana. Hivi hamna namna nyingine ya kujitafutia kipato bila kushiriki pesa haramu za ccm na serikali yake?
 
Huyo ni beberu au mtetea!?
 
[emoji706]

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Usisahau hao hao wakenya waliwapima madereva wao na kupelekwa karantini, alipimwa mara ya pili ikaonekana hana corona. Aibu!!
Bahatai nzuri Ni kwamba wamerudishwa kwenu nyie ambayo mnaamini hamna korona Ni vipimo vinasema uongo, kwa hiyo endeleeni na maisha Kama kawaida, Wala msichukue tahadhari dhidi Yao maana hawana korona
 
Ashante kwa maelezo ya kitaalamu , wengine tumeambulia elimu nzuri sana. Ila naomba nisaidie kuelewa mambo yafuatayo

1. Kwa mfumo wa upimaji Tanzania ninavyoelewa umeratibiwa na wizara ya afya kupitia hospital teule, kwanini unaelekeza lawama kwa maabara ya taifa baada ya wizara husika maana ndio mratibu. Maabara ya taifa inawafanyakazi wataalamu wakuweze kwenda kila wilaya kwa ajili ya sample collection? Nadhani hili ni kosa la wizara kutofanya maandalizi ya mapema ya kukabiliana na hili janga.

2. Kwanini njia Bora iwe kuwasimamisha na kupisha uchunguzi wakati ambao watanzania wanapigania afya yao. Hivi kama taifa tulishindwa kununua kifaa kingine na kuendelea na vipimo wakati tunakitafiti hiki kifaa, kama tumeweza kutuma ndege kufuata mitishamba, tulishindwa kutuma ndege kununua kifaa kingine ili watanzania waendelee na matibabu kuepusha vifo vilivyoweza kuepukika?

3. Kama wataalamu wa maabara ya taifa wameshahukumiwa na mkuu wa nchi , je hiki ulichokiandika na kinatotarajiwa kuandikwa na tume si moja ya justifications za kuhalalisha statement ya mkuu wa nchi _ "The boss is always right, _ The president is the president "

4. Nini hatama ya vifo vinavyotokea sasa na ambavyo watu hawahapewa majibu, marehemu huzikwa kwa tamaduni zetu na kuacha aambukize ndugu na majirani? Au hizikwa kufuata mwongozo wa WHO na kuwanyima ndugu na jamaa fursa ya kuaga wapendwa wetu kwa kufuata imani na mira zetu ?

5. Mbona sample zinazopimwa na majirani bado wanakuta rate ya positive ni kubwa pia? Kwanini tutilie mashaka kwenye majibu yetu na sio majibu ya majirani?

Nimeuliza kwasababu umesema wewe ni mtaalamu, nilitegemea uje na constructive ideas kuokoa maisha ya watanzania na sio kusifika wanasiasa na kuwakandamiza wataalamu wenzako. Ikiwa hao wataalamu wametumiwa basi kama yaafa hatukujiandaa na wanaostahili kuwajibika ni viongozi wakuu wa vizara na hao wataalamu pia.



Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ni swala la ufahamu, kwamba chanzo cha korona huko China ni nyama pori. Hapa kwetu unapopima mbuzi ukakuta anayo korona, si ni sawa na China waliopima nyama pori? Naomba jibu toka mtoa mada.

Sent using Jamii Forums mobile app
 

Ka jamaa na uaskari kanzu wake mwisho October, maana ruzuku yao yote itakuwa imekatwa. watatoka mfuto.
 
Nimeuliza uhalisia kupima virus kutoka nyama pori ya uchina, mahali korona ilipoanzia na sisi tunaopima mbuzi. Kwangu mimi naona kama China wamepata kirusi toka nyama pori ni sahihi hata sisi kupata kirusi kwenye mbuzi. Naomba ufafanuzi wa biotechnology?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hilo swali lina msingi nyuma yake,tunanawa kwa sababu mikono inashika object mbalimbali kama meza,vitasa vya mlango nk ambako ndipo virus wanakaa,hivyo kama itakuwa umeshika hao virus ili usiambukizwe na kuambukiza wengine ndio maana tunanawa mikono au kui sanitize
Kwani ww ni object?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…