Virusi vya Corona: Nadharia za kuficha ukweli zaibuka kuhusu kifo cha mtaalamu wa Corona, Bing Liu

Virusi vya Corona: Nadharia za kuficha ukweli zaibuka kuhusu kifo cha mtaalamu wa Corona, Bing Liu

Masi Lambo

JF-Expert Member
Joined
Apr 8, 2020
Posts
532
Reaction score
360
Bing Liu

Haki miliki ya pichaUNIVERSITY OF PITTSBURGH
Mauaji ya raia wa China, mtafiti wa masuala ya virusi vya corona kwenye ardhi ya Marekani yamesababisha nadharia mbalimbali duaniani kuwa kuna sababu iliyojificha kuhusu kifo chake.

Bing Liu, profesa msaidizi mwenye miaka 37 katika Chuo Kikuu cha Tiba cha Pittsburgh, Marekani alipatikana akiwa amekufa nyumbani kwake siku ya Jumamosi.

Wenzake walisema alikuwa karibu kupata "matokeo muhimu" ya tafiti kuhusu Covid-19, tukio lililosababisha kuwepo kwa maoni mitandaoni yanayoeleza kuwa yawezekana bwana Liu aliuawa lakini polisi wanasema ni tukio la kujiua.

Kwanini Liu aliuawa?
Alikutwa akiwa na majeraha mengi ya risasi kichwani, shingoni katika eneo la Pittsburgh yalipo makazi yake kwa mujibu wa polisi wa eneo hilo.

Mtu aliyekuwa na silaha alitambulika kuwa na miaka 46, mhandisi wa programu ya kompyuta, Hao Gu. Mamlaka zinasema muuaji naye alijiua baada ya kurudi kwenye gari lake.

Liu na Gu walikuwa wanafahamiana, maafisa wapelelezi wa mauaji walieleza.

Uchunguzi umebaini kuwa lilikuwa tukio la kuua na kujiua lililotokana na ''mgogoro wa muda mrefu wa masuala ya kimapenzi''.

Wamesema ''hakuna ushahidi'' wa kuhusisha tukio hilo na utafiti wa Liu na mazingira ya sasa ya changamoto za kiafya.

Liu ni nani?
Katika taarifa yao , wenzake wamemwelezea kama mtafiti wa kipekee ambaye ''alikuwa ukingoni kufanikisha kupata matokeo muhimu '' ya kuelewa maambukizi ya Covid-19.

Waliomboleza kifo cha Liu na kuahidi kumalizia utafiti wake ''zikiwa ni juhudi za kuenzi ubora wake katika uwanja wa kisanyansi''.

Liu, raia wa China alipata shahada yake ya kwanza na shahada ya uzamivu katika masomo ya sayansi ya kompyuta nchini Singapore kabla ya kufanya utafiti nchini Marekani.

Aliwahi kuungana na wanabaiolojia wengine kufanya utafiti kuhusu kinga ya binaadamu, kwa mujibu wa wasifu wake mtandaoni.

Yanayozungumzwa mitandaoni
''Mungu wangu'' mtumiaji mmoja wa mtandao wa kijamii wa Weibo aliandika. '' Labda alibaini kuwa virusi vilitengenezwa kwenye maabara nchini Marekani.''

Maoni kama hayo yalieleza kuwa Liu aliuawa kwa sababu pengine aligundua chanzo cha virusi vya corona.

Maafisa wa China na vyombo vya habari vya habari vya serikali vilisema kuwa madai yakuwa virusi vilitengenezwa Marekani na kupelekwa Wuhan na wanajeshi wa Marekani hayana msigi.

Wengine walisema ni tukio ambalo lina sababu iliyojificha.

''Inawezekana kuwa kuna siri iliyojificha gizani''. Alieleza mtu mmoja kwenye mtandao huo.
 
Hakuna Atakayebaki chini ya Jua, Apumzike kwa Amani Bing Liu.
 
Bing Liu


Mauaji ya raia wa China, mtafiti wa masuala ya virusi vya corona kwenye ardhi ya Marekani yamesababisha nadharia mbalimbali duaniani kuwa kuna sababu iliyojificha kuhusu kifo chake.

Bing Liu, profesa msaidizi mwenye miaka 37 katika Chuo Kikuu cha Tiba cha Pittsburgh, Marekani alipatikana akiwa amekufa nyumbani kwake siku ya Jumamosi.

Wenzake walisema alikuwa karibu kupata "matokeo muhimu" ya tafiti kuhusu Covid-19, tukio lililosababisha kuwepo kwa maoni mitandaoni yanayoeleza kuwa yawezekana bwana Liu aliuawa lakini polisi wanasema ni tukio la kujiua.

Kwa nini Liu aliuawa?
Alikutwa akiwa na majeraha mengi ya risasi kichwani,shingoni katika eneo la Pittsburgh yalipo makazi yake kwa mujibu wa polisi wa eneo hilo.

Mtu aliyekuwa na silaha alitambulika kuwa na miaka 46, mhandisi wa programu ya kompyuta, Hao Gu. Mamlaka zinasema muuaji naye alijiua baada ya kurudi kwenye gari lake.

Liu na Gu walikuwa wanafahamiana, maafisa wapelelezi wa mauaji walieleza.

Uchunguzi umebaini kuwa lilikuwa tukio la kuua na kujiua lililotokana na ''mgogoro wa muda mrefu wa masuala ya kimapenzi''.

Wamesema ''hakuna ushahidi'' wa kuhusisha tukio hilo na utafiti wa Liu na mazingira ya sasa ya changamoto za kiafya.

Liu ni nani?
Katika taarifa yao , wenzake wamemwelezea kama mtafiti wa kipekee ambaye ''alikuwa ukingoni kufanikisha kupata matokeo muhimu '' ya kuelewa maambukizi ya Covid-19.

Waliomboleza kifo cha Liu na kuahidi kumalizia utafiti wake ''zikiwa ni juhudi za kuenzi ubora wake katika uwanja wa kisanyansi''.

Liu, raia wa China alipata shahada yake ya kwanza na shahada ya uzamivu katika masomo ya sayansi ya kompyuta nchini Singapore kabla ya kufanya utafiti nchini Marekani.

Aliwahi kuungana na wanabaiolojia wengine kufanya utafiti kuhusu kinga ya binaadamu, kwa mujibu wa wasifu wake mtandaoni.

Yanayozungumzwa mitandaoni.

''Mungu wangu'' mtumiaji mmoja wa mtandao wa kijamii wa Weibo aliandika. '' Labda alibaini kuwa virusi vilitengenezwa kwenye maabara nchini Marekani.''

Maoni kama hayo yalieleza kuwa Liu aliuawa kwa sababu pengine aligundua chanzo cha virusi vya corona.
Maafisa wa China na vyombo vya habari vya habari vya serikali vilisema kuwa madai yakuwa virusi vilitengenezwa Marekani na kupelekwa Wuhan na wanajeshi wa Marekani hayana msigi.

Wengine walisema ni tukio ambalo lina sababu iliyojificha.

''Inawezekana kuwa kuna siri iliyojificha gizani''. Alieleza mtu mmoja kwenye mtandao huo.

Taarifa zaidi kuhusu virusi vya corona:

Maoni mengi ya watu kwenye mtandao huo yanasema kuwa historia ya Liu inaweza kuwa ndio iliyomuweka hatarini nchini Marekani, ingawa hakuna ushahidi ulioibuka kuwa Liu alikuwa akilengwa kwa sababu ya asili yake.

Gazeti ka Global Times linalofungamana na chombo cha habari cha taifa nchini china, lilichapisha makala kuhusu mazingira ya kifo cha Liu.

Kwenye mtandao wa Twitter, baadhi wameeleza hisia zao kuwa huenda serikali ya China ina mkono wake kwenye tukio hilo.

Kutokana na janga la Covid-19, nadharia mbalimbali kuhusu virusi na asili yake zimeendelea kusambaa kwenye mitandao ya kijamii.

Nyingine zikiwa na madai yasiyothibitishwa zimekuwa zikiungwa mkono na wanasiasa na vyombo vya habari vya China na Marekani.
 
Ninazidi kuamini hili gonjwa kuna powerful forces nyuma yake, kila mtu anayejaribu kuleta suluhisho, iwe utafiti ama tiba anapondwa sana labda dawa haitibu mfano ile ya Madagascar, huyu mchina pia kauliwa na alikua final stages kutoa utafiti muhimu ambao ungesaidia kuelewa huyu virus na kusaidia kutoa tiba, Mungu atusaidie maana tunapoelekea ni chaos zaidi kuongezeka duniani.
Screenshot_20200507-145541_Twitter~2.jpg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
download (1).jpeg


Mtafiti katika Chuo Kikuu cha Tiba aliyekaribia kupata ufumbuzi muhimu Virusi vya Corona ameuawa kwa kupigwa risasi kichwani na shingoni huko Pennyslavia, Marekani kwa mujibu wa ripoti.

Bing Liu, 37 mtafiti katika Idara ya Tiba ya Chuo Kikuu cha Pittsburgh alikutwa amekufa siku ya Jumamosi nyumbani kwake kwenye mji mdogo wa Ross Township, alisema mtafiti wa afya wa kaunti ya Allegheny. Alipopatikana, alikutwa amepigwa risasi mbili, moja kichwani na moja shingoni.

Saa moja baada ya mwili wa Liu kupatikana akiwa ameuawa, mtu wa pili, Hao Gu (46) alikutwa amekufa ndani ya gari umbali usiozidi kilomita mbili kutoka nyumbani kwa Bing. Afisa Mpelelezi kutoka mji wa Ross, Sajento Brian Kohlhepp aliliambia shirika la habari la NBC kuwa waliouawa walifahamiana kwa karibu. Wapelelezi wanaamini kuwa Gu alimuua Liu kabla ya kurudi kwenye gari yake ambapo alijipiga risasi iliyosababisha kifo chake ingawa hadi sasa mamlaka za Marekani zinachunguza sababu za tukio hilo.

‘’Bing alikuwa anakaribia kugundua mambo muhimu kabisa kuelewa mbinu za kiseli zinazohusiana na maambukizi ya virusi vya Corona na sababu za watu kuumwa kwa dalili zinazotokana na ugonjwa huo’’, taarifa ya Chuo kikuu cha Pittsburgh ilisema. Tutajitajidi kukamilisha kile ambacho alikianza ili kuwa heshima tutakayotoa kwake kwa juhudi zake katika sayansi’’, kilisema chou hicho..

Pia pitia:-
The Washingtonpost
https://www.google.com/amp/s/www.washingtonpost.com/nation/2020/05/06/bing-liu-university-of-pittsburgh-coronavirus-researcher-murder-suicide/?outputType=amp

Bbc
China netizens see conspiracy in US murder-suicide

Cnn
Professor researching Covid-19 was killed in an apparent murder-suicide, officials say
 
Then utasikia watu wanasema #covid19 imetoka kwa wanyama sijui kwa popo n.k
 
Harufu ya ujasusi (China Vs USA). China anafaidika na sakata la Covid 19. America analia

Odhis *
 
Kwa kweli Mungu ndio anaejua kinachoendelea dunia
Huku nilipo nashindwa kuelewa kabisa kitu wanafanya
Hii lockdowns kuna kitu nyuma yake pia
Najua niko nje ya mada sorry



Sent from my iPhone using Tapatalk
 
Back
Top Bottom