Habari za wakati huu wadau wa soka na mashabiki wa kandanda nchini Tanzania,
Mapambano yaendelee maana sio kwa msoto huu huku kitaani mambo ni magumu twende kwenye mada:–
Ukiangalia mambo yanayoendelea kwenye soka letu unaona kabisa kuanzia wachambuzi mpaka wadau wote wa soka wanaegemea upande mmoja na atakae jaribu kuwa kinyume na upande unaosifiwa wa jangwani basi atapondwa au atapewa kila jina lisilo faa mfano ALI KAMWE na Jemedari saidi ili usifiwe upande ule inabidi ukubali kuiponda na kuichafua simba.
Wachambuzi na wadau wa soka kuiponda simba na pre season kwa nguvu zote tena kwa hoja dhaifu na zisizo na mashiko kwa mifano ya kusema mabingwa wote hawajaenda pre season wapo makwao simba inapoteza mda tu.
Jana yanga wamefanya press conference ila kwenye ubao wa matangazo hakuna logo ya yanga kuna logo za mdhamini wachambuzi wapo kimya tu ila simba ilifanya press conference bila logo ya mdhamini wachambuzi wa mchongo wakaanza kelele unamalizaje league bila kujua mdhamini.
Kwenye utambulisho wakaanza kuiponda idara ya Digital platform ya simba wakaanza kuipa mileage ya yanga kwamba ni wabunifu kuliko simba inawezekana ikawa kweli ila mbona ikitokea kitu kibaya tu cha simba ndo kina pewa promo ila mazuri watayaponda au kutafuta kasoro.
Kwenye usajili wakati simba alipoondoka bwalya makanjanja wakasema ameondoka bora hajauzwa ila jana swala la Chiko ushindi makanja wote wamekaa kimya wakati alikuwa kwa mkopo na mkopo wake umeisha hakuna anayeongea kuhusu swala hilo.
Swala la Bernard Morrison kipindi yupo simba na wakatangaza wamempa likizo makanjanja wakahoji likizo wakati league inaendelea wengine wakamfanyia mpaka interview ila upande wa pili aliondoka saido ntibanzonkiza hakuna aliyehoji kuondoka kwake wala kutaka kujua nini kilitokea zaidi ya tetesi tu kwamba walienda kulewa na ambundo ila mwenzake bado yupo.
Kwenye uchaguzi engineer hersi alikuwa anagombea mwenyewe na kuwatuliza wote waliokuwa na nia ya kuchukua fomu ya kugombea uraisi ila makanjanja yalikaa kimya bila kuhoji wala kuongea lolote kutokana na umafia huo ila hilo swala angefanya MO Tanzania ingesimama na kuhoji ni utaratibu gani umetumika na sheria ipi kama alivyopewa cheo cha raisi wa heshima tu makanjanja yaliponda ingetokea umafia kama wa engineer ingekuwaje.
Kwenye tuzo makanjanja waliponda tuzo ya ENONGA na kuleta takwimu kwamba hakustahili ni yanga ndo walistahili tuzo zote wakasahau kuwa Enonga kabla ya kuja Simba alishinda tuzo ya beki bora Congo aliletewa wakati yupo Tanzania iweje kushinda Tanzania tuzo kwake iwe ajabu na kuponda kwa kigezo cha kadi nyekundu.
Furaha yao na lengo la hii vita ni Kuona MO anaondoka katika club ya simba na kuona simba wanapitisha bakuli na kuomba omba kama ilivyokuwa upande wa pili hapo itakuwa wamekamilisha Lengo lao walilolipanga wanasahau simba ni super brand matajiri wote Tanzani, wanaitaka ndo maana MO anang'ang'ania akiwemo boss wao baada ya kuona anapata hasara kule akataka simba wavae magodoro kwenye jezi hapo ndo iliongeza hii vita.