Vita uenyekiti Bunge la Katiba; CCM plan B kumuondoa Chenge na kumuweka Dr. Migiro

Vita uenyekiti Bunge la Katiba; CCM plan B kumuondoa Chenge na kumuweka Dr. Migiro

Mwana Mpotevu

Platinum Member
Joined
Sep 7, 2011
Posts
3,295
Reaction score
2,501
Nimefika Dodoma tangu wiki iliyopita mwanzoni na nimekuwa nafuatilia mwenendo wa bunge la katiba. Watu wamekuwa wakijiuliza ukimya wa chenge kuthibitisha kutaka kugombea uenyekiti wa bunge kama Samwel Sitta alivyoeleza bayana.

Kinachirndelea hapa ni kwamba sasa CCM wamekuja na plan B ya kutokumsimamisha Chenge na badala yake Dr Migiro ndie asimame kutaka uenyekiti kupambana na Sitta.

Sababu kubwa ni kwamba Chenge ndie amehusika kuandika rasimu mbadala ya katiba na hivyo anatakiwa kuwa mstari wa mbele kuielezea maudhui yake na CCM imeona asiwe mwenyekiti ili aweze kuisimamia rasimu mbadala ya CCM. Hapo ndipo wameona wamsimamishe Dr Migiro.

Ninapoandika hapa, CCM wabunge wake wanakutana saa kumi kamili leo jioni hii kupitisha azimio hilo licha ya kwamba kuna kundi kubwa linamtaka Sitta toka ndani ya CCM na wameapa hawatakubali kuburuzwa. Sitta na wenzake wanaendelea na kampeni na kufukia mashimo kuwa kumpa sitta uenyekiti ni ushindi kwa upinzani na wanaopenda haki walio against misimamo ya kichama.

Lakini upinzani nao unataka kusimamisha mgombea wao wa uenyekiti licha ya kumuunga pia mkono Sitta.

Nitaendelea kuwaeleza kitakachojiri katika party caucus ya CCM kama nikipata ukweli wa kilichojadiliwa na hata kinachozunguka duru hizi za uchaguzi wa mwenyekiti wa bunge la katiba. Kwa sasa tambueni kuwa sio Chenge vs Sitta tena bali Dr Migiro vs Sitta
 
Hujui uliloandika. Kwenye katiba acha mambo ya chama
 
Wapinzani hakuna haja ya kuweka mgombea maana hatapita, mnapoteza muda!!! Wekeni Nguvu mchagueni Samweli Sitta na hapo ndipo litakuwa Bunge la Nguvu la Katiba. Migiro atapita kama wapinzani mtaweka mgombea na itakula kwenu. Mr. 6 ni mpango mzima.
 
mafeta najua kuliko unavyodhani. Mambo ya vyama hayatakiwi kuwekwa katika swala hili lakini ili kusimamia maslahi na matakwa ya chama ndio sababu baadhi ya wanaccm wanataka mtu wao wa kusimamia matakwa ya chama awe mwenyekiti na si vinginevyo.

Kwa taarifa yako juzi upinzani ukiongozwa na Mbowe, Lipumba na Silinde waliongoza kikao maalumcha wajumbe baadhi na kuunda umoja wa katiba ya wananchi lakini wajumbe wa ccm hawamo. Kuna uchama mwingi sana katika hii kitu kwa taarifa yako licha ya kwamba sheria haikubali misimamo ya kichama katika utungaji wa katiba mpya
 
Last edited by a moderator:
Chizi Furesh hayo mambo ya chama kupendekeza hayapo ila ccm wanataka wawe na mtu wao licha ya kwamba wanaccm wengine hawakatazwi kugombea. Likewise wapinzani nqo wanafikiria kumsimamisha mtu wao
 
Last edited by a moderator:
mafeta najua kuliko unavyodhani. Mambo ya vyama hayatakiwi kuwekwa katika swala hili lakini ili kusimamia maslahi na matakwa ya chama ndio sababu baadhi ya wanaccm wanataka mtu wao wa kusimamia matakwa ya chama awe mwenyekiti na si vinginevyo.

Kwa taarifa yako juzi upinzani ukiongozwa na Mbowe, Lipumba na Silinde waliongoza kikao maalumcha wajumbe baadhi na kuunda umoja wa katiba ya wananchi lakini wajumbe wa ccm hawamo. Kuna uchama mwingi sana katika hii kitu kwa taarifa yako licha ya kwamba sheria haikubali misimamo ya kichama katika utungaji wa katiba mpya

Nimekusoma watuletee kwenye kura tutaamua wenye nchi ASante
 
Last edited by a moderator:
Nimefika Dodoma tangu wiki iliyopita mwanzoni na nimekuwa nafuatilia mwenendo wa bunge la katiba. Watu wamekuwa wakijiuliza ukimya wa chenge kuthibitisha kutaka kugombea uenyekiti wa bunge kama Samwel Sitta alivyoeleza bayana.

Kinachirndelea hapa ni kwamba sasa CCM wamekuja na plan B ya kutokumsimamisha Chenge na badala yake Dr Migiro ndie asimame kutaka uenyekiti kupambana na Sitta.

Sababu kubwa ni kwamba Chenge ndie amehusika kuandika rasimu mbadala ya katiba na hivyo anatakiwa kuwa mstari wa mbele kuielezea maudhui yake na CCM imeona asiwe mwenyekiti ili aweze kuisimamia rasimu mbadala ya CCM. Hapo ndipo wameona wamsimamishe Dr Migiro.

Ninapoandika hapa, CCM wabunge wake wanakutana saa kumi kamili leo jioni hii kupitisha azimio hilo licha ya kwamba kuna kundi kubwa linamtaka Sitta toka ndani ya CCM na wameapa hawatakubali kuburuzwa. Sitta na wenzake wanaendelea na kampeni na kufukia mashimo kuwa kumpa sitta uenyekiti ni ushindi kwa upinzani na wanaopenda haki walio against misimamo ya kichama.

Lakini upinzani nao unataka kusimamisha mgombea wao wa uenyekiti licha ya kumuunga pia mkono Sitta.

Nitaendelea kuwaeleza kitakachojiri katika party caucus ya CCM kama nikipata ukweli wa kilichojadiliwa na hata kinachozunguka duru hizi za uchaguzi wa mwenyekiti wa bunge la katiba. Kwa sasa tambueni kuwa sio Chenge vs Sitta tena bali Dr Migiro vs Sitta

Hivi hawa wajumbe wa bunge la katiba waliwahi kufanya nini huko Dodoma kama mpaka leo wiki imeisha hata hawajamchagua mwenyekiti? Yaani wanakula posho bure tu au mimi ndio sielewi inawezekana kuna kazi nyingine muhimu wanaifanya?

Mwenye kufahamu au wewe mleta mada hebu twambie wajumbe kwa kipindi hiki cha wiki nzima wamekuwa wanafanya kazi gani?

Tiba
 
wapigane wawaweke hata nani kuchukua hiyo nafasi tunachotaka ni katiba inayoeleweka .... hatutaki ujinga ujinga
 
Sitashangaa nikisikia mzee 6 akiambiwa tena aende akafanya plastic surgery kwanza ya kubadiri jinsia ili apewe kugombea, chezea rafu za magamba wewe!?
 
Tiba kinachoendelea hapa kinalalamikiwa hata na baadhi ya wajumbe wenyewe (wachache wenye uchungu na nchi). Kinachoelezwa ni kwamba rasimu ya kanuni za bunge hili zinazopitiwa na kamati ya Profesa Mahalu imebaini kuwa kanuni ni mbovu na za kidikteta na zitafanya mwenyekiti wa bunge kuwa dikteta na kuwa na maamuzi ya mwisho. Baadhi ya wajumbe wanaopitia kanuni hizi akiwemo Tundu lissu wakasema kanuni za aina hii hazikubaliki. Ikabidi wafumue na kuanza kuandika kanuni upya na ndio maana jana wakaomba muda ili waendelee kuandika rasimu mpya kabisa ya kanuni na zile za awali wakiziweka kando.

Lakini jana usiku.kazi walimaliza na leo wangeweza kuendelea lakini kwakuwa kificho alishasema watakutaka kesho jtano kwa semina kwahiyo hadi kesho ndo watafanya semina ya kanuni hizo mpya na sio ile rasimu waliyogawiwa wiki iliyopita. Axtually kuna kupoteza muda sana ingawa nahisi wanafanya hivi purposely!
 
Last edited by a moderator:
Kidumu chama chetu, Leo Mbowe yuko bize kumkampenia Sitta japo Slaa aliwahi kumwita ni mnafiki.
 
Kwani Dokita Asha Roze pia si mwana wa sheria tena wa Chuo kikuu cha Dalasalaama wajameni nyie?
 
Mimi hata siwaelewi posho wameshaanza kutafuna kabla hata majadiliano hayajaanza.na siku zinazidi kuyoyoma tu..
 
SITTA; MWENYEKITI WA BUNGE LA KATIBA = KURA YA SIRI/ELECTRONIC + CDM + NCCR + TLP + CUF + WAVUVI + WAGANGA WA KIENYEJI + WAFUGAJI + WALEMAVU + WATUMISHI + WASOMI + MALENGO YANAYOFANANA + CCM UAMSHO - CCM MAFISADI

Viva SITTA; Mzee wa Standard and speed. You are the man "mjengoni" who can deliver us a new constitution worthy of the name.
 
Back
Top Bottom