Vita vya Kagera: Historia yangu - Sehemu ya kwanza

Two of my uncles participated in that War from day 1 and they share the same stories of what happened during that war. Therefore it is the TRUTH you can take it or leave and formulate your own truth.
Muwe mnatutafsiria kwa Kiswahili!
 
That’s you opinion but you were not there when my Uncles shared their stories about what happened during that war.

I don't buy this pal.
Its all made up
 
Vita ni kitu kibaya sana japo story zake huwa za kusisimua.
Ni kweli vita ni mbaya sana maana inaleta huzuni kwenye familia nyingi inaleta Umaskini kwenye Taifa hata familia watu wanakufa na wengine wanaporudi au wanapokuwa vitani wanapata matatizo ya kisaikolojia na wanakosa msaada huvyo wengi hupoteza maisha na kuacha familia zikiwa kwenye shida lukuki.
 
Vita ni kitu kibaya sana japo story zake huwa za kusisimua.
Vita siyo lelemama, tena afadhali siku hizi kuna GPS. Wakati huo makamanda wetu walikuwa wanaongoza vikosi kwa kutumia ramani, rula na compass tu. Mojawapo ya mafunzo ya makamanda wakati huo ilikuwa ni map reading: kwa hiyo hakuna kamanda wa jeshi ambaye alikuwa hajui kusoma grid reference, magnetic variation, contours na kutumia namba hizo kupanga ruti. Wakati mwingine makamanda walikuwa wanakutana na vikwazo kuwa ramani haikuonyesha chaka zito lisilopitika ambalo sasa wamekutana nalo kwenye ruti zao lakini wanalipangua. Halafu sehemu kubwa ya mapigano yale yalikuwa ni ya kutembea kwa miguu maporini.

Niliandika sehemu nyingine kuwa vita ni mapigano siyo ya kutupiana ngumi bali ni ya kurushiana risasi za moto na mizinga na vile vile kutegana mabomu njiani. Chochote kati ya hivyo kikikukuta hakikuachi kama mwanzo; ama utakufa, au utapoteza viungo kadhaa kwenye mwili wako. Ni bahati nzuri sana sehemu iliyokuwa na resistance kubwa dhidi ya jeshi letu ilikuwa ni huku maeneo ya kusini tu. Baada ya Colonel Msuya kuteka Kampala, kaskazini ya Kampala hakukuwa na resistance kubwa tena kwani askari wengi wa amini walikuwa wakikimbilia ama Sudan au Zaire. Askari wetu wengi waliofariki katika vita ile ilikuwa ni kwenye mapambano ya mwazo pale mto Kagera, na kwenye meneo ya Masaka, Mbarara na kidogo sana (huenda wasisozidi 10) kule maeneo Kasese. Casualty report ya jeshi letu lilipoingia Kampala ilikuwa pia ni ndogo sana.

Jeshi liliporudi, kulikuwa na vilema kadhaa ambao Nyerere aliahidi kuwa watatunzwa na taifa, ila sijui kama hali zao zilendeleaje. Kaka yangu ambaye alikuwa frontline kwenye kikosi cha mizinga sasa hivi yuko hoi bin taaban huko kijijini akisumbuliwa na uzee na ufukara, mimi huwa nampelekea allowance ya kama dola 300 kwa mwezi ili alipe bili zake. Rafiki zangu tuliokuwa nao reserve pale brigade ya faru wakamua kuendelea na jeshi baadhi yao bado wako jeshini. Wawili ni majenerali kwa ngazi tofauti, mmoja alikuwa Luteni kanali JKT ila akapata msukosuko fulani ya ufisadi ambao mahakama iliimkuta hana hatia, ila akaamua kustaafu mapema. Mwingine alikuwa Kanali wa Air Force (huyu nilisoma habari zake kama miaka kumi iliyopita alipomtolea bastola mfanyakazi wa kampuni ya kupaki magari ambaye alikuwa ameweka chain ya kulock gari yake akimtaka alipe ushuru wa parking katikati ya jiji) na mwingine alikuwa Luteni Kanali wa Infantry lakini leo sijui wote hao wawili wako wapi kwani sijapata habari zao kwa muda mrefu sasa, nadhani wameshastaafu. Ninaojua kuwa bado wako active ni wale majenerali wawili ambao habari zao bado zinandikwa magazetini.
 
Simulizi yako imekosa uhalisia kwa kukosekana mchango wa MTU muhimu sana katka vita vya Kagera ambae hakutajwa na si mwingine ni Brig Kitete ambae alikuwa mkuu wa mbinu za kivita (War Planner) alifariki muda mfupi baada ya vita kwa ajali ya gari jijini dar.
 
Soma vizuri hiyo ipo na nimeelezea vizuri sana pitia sehemu ya Pili na ya Tatu!!
 
Soma vizuri hiyo ipo na nimeelezea vizuri sana pitia sehemu ya Pili na ya Tatu!!
Nimeona mkuu, hongera sana.
Ni masahibu gani yalimkuta kamanda Dominic Nshimani mpaka kupelekea kunyongwa? A decorated hero, so sad.
 

VITA VYA KAGERA: Nyerere, Samora wakubaliana kumpiga Idi Amin-5​


Muda mfupi baada ya Rais Julius Nyerere kulitangazia Taifa jijini Dar es Salaam kuhusu uvamizi wa Idi Amin na uamuzi wa Tanzania kumpiga, Alhamisi ya Novemba 2, 1978, alipanda ndege kwenda Beira, Msumbiji kwenye mkutano na mwenyeji wake, Rais Samora Machel.

Ilikuwa aahirishe safari hiyo lakini alilazimika kwenda kwa sababu alikuwa mwenyekiti wa Nchi za Mstari wa Mbele (FLS) katika ukombozi. Nchi nyingine ni Angola, Botswana, Msumbiji, Tanzania, Zambia na Zimbabwe.

Wakati huo pia kulikuwa na mgogoro wa mpaka kati ya Zambia na Zimbabwe (zamani Rhodesia) uliosababishwa na Rais Kenneth Kaunda wa Zambia. Nyerere ndiye aliyekuwa ameitisha mkutano wa kushughulikia mgogoro huo.

Kaunda alikuwa amefungua mpaka wake na Zimbabwe, jambo lililomkera sana Nyerere na Samora.

Nchini Rhodesia, mwanasiasa aliyeitwa Ndabaningi Sithole, ambaye ni mwanzilishi wa chama cha Zimbabwe African National Union (Zanu) kabla ya kuangushwa na Robert Mugabe, alikuwa mshirika wa karibu sana wa Idi Amin.

Kwa hiyo kufunguliwa kwa mpaka huo kulimfadhaisha Mwalimu Nyerere, hasa wakati huo ambao tayari alikuwa na mgogoro na Uganda. Kwa namna fulani Rhodesia ilikuwa na uhusiano wa kijeshi na utawala wa Idi Amin wa Uganda.

Katika ukurasa wa 114 wa kitabu chake cha For the Sake of Argument: Essays and Minority Reports, mwandishi Christopher Hitchens anasema wakati fulani “akiwa ofisini, (Sithole) aliomba msaada wa Idi Amin wa kuunda jeshi lake binafsi”.

Jumatatu ya Julai 17, 1978, ikiwa ni miezi minne kabla ya kuzuka kwa Vita vya Uganda, jarida la Facts and Reports (volume 8), katika habari iliyoandikwa na David Martin iliyokuwa na kichwa kilichosomeka “Sithole Guerrillas Fly to Amin for Training”, kulikuwa na tuhuma za uhusiano huo wa kijeshi.

“Dikteta Idi Amin ameshutumiwa vikali kwa kutoa mafunzo ya kijeshi kwa maelfu ya vijana wa washirika wa Ian Smith (wa Rhodesia) kwa madhumuni ya kuwatumia kuvuruga harakati za ukombozi nchini Zimbabwe,” aliandika mwandishi huyo.

Jarida jingine la International Bulletin (volume 4) la Julai 1978, lilizungumzia suala hilo.

“Mshirika mweusi wa Ian Smith, Mchungaji Ndabaningi Sithole anafundisha jeshi lake binafsi nchini Uganda,” liliandika jarida hilo. Pia, jarida la Africa Research Bulletin’ likaripoti kuwa “Mchungaji Ndabaningi Sithole amepokea idadi kubwa ya wapiganaji kutoka Uganda kwa Idi Amin pamoja na vifaa vya mafunzo”.

Zilikuwapo pia habari kwamba ndege za Rhodesia zilikuwa zikitua katika viwanja vya ndege vya Uganda—Entebbe na Nakosongola.

Habari hizo na nyinginezo za ushirika wa Idi Amin na Sithole, zikijumlishwa na ile ya Zambia kufungua mpaka wake na Rhodesia, zilimfanya Mwalimu Nyerere kwenda Beira, Msumbiji, kujadili jambo hilo haraka kadri ilivyowezekana.

Nyerere na Samora walikutana jioni ya Novemba 2, 1978 kujadili jambo hilo na kuridhika kuwa Idi Amin alitumiwa na mataifa mengine kuivamia Tanzania kwa lengo la kumuondoa Nyerere katika harakati zake za ukombozi wa Zimbabwe dhidi ya akina Ian Smith na mshirika wake, Mchungaji Ndabaningi Sithole, na kwamba huenda Uingereza ilikuwa nyuma ya mpango huo.

Baadhi ya wanazuoni wanaamini kuwa halikuwa jambo la bahati mbaya kwamba vita vya Kagera kuzuka wakati huo muhimu wa mazungumzo kati ya vikosi vya ukombozi na serikali ya wachache ya Ian Smith nchini Zimbabwe.

Walisema wapinzani wa ukombozi walitaka kudhoofisha jitihada za Mwalimu Nyerere “kwa gharama zozote”.

Baada ya kutafakari yote hayo, Nyerere alimhakikishia Samora kwamba Tanzania ingeweza kupambana na Idi Amin bila kupoteza lengo lake la harakati za ukombozi wa Zimbabwe.

Walikubaliana kuwa kikosi cha jeshi la Tanzania kilichokuwa katika mpaka wa Msumbiji na Rhodesia kirejee Tanzania na, zaidi ya hilo, Samora naye akaahidi kutoa kikosi chake kuja kusaidiana na Tanzania.

Ndani ya siku chache, wanajeshi wa Msumbiji wakawa wamewasili Kagera tayari kwa mapigano. Hakuna chombo chochote cha habari cha Tanzania kilichoandika taarifa zozote za wapiganaji wa Msumbiji kuwasili Kagera.

Hata hivyo, kitabu cha War in Uganda cha Tony Avirgan na ?Martha Honey kinasema “ushahidi mdogo sana kwamba wapiganaji wa Msumbiji walikuwa Tanzania ni nakala ya gazeti Noticias iliyoachwa kwenye ukumbi wa mapumziko wa Uwanja wa Ndege wa Mwanza.”

Waandishi wa kitabu hicho, ambao walikuwa uwanja wa vita, wamesema mbali na wapiganaji hao 800 kutoka Msumbiji, hakukuwa na wapiganaji wengine kutoka taifa jingine lolote duniani waliokuwa wakipigana bega kwa bega na wapiganaji wa Tanzania dhidi ya majeshi ya Idi Amin.

Katika lile juma la pili la Novemba 1978, pamoja na magumu yote waliyokumbana nayo kama mvua, Tanzania iliweza kuwaandaa vyema wapiganaji wake.

Soma Zaidi: Idi Amin avunja daraja la Mto Kagera - 4

Juma hilo ndipo alipowasili Meja Jenerali Tumainieli Kiwelu kuongoza mapambano. Pamoja na kwamba Tanzania ilisikitishwa sana na kuvunjwa kwa daraja la Mto Kagera, ilipata nafasi ya kufanya maandalizi ya kutosha bila hofu ya kuvamiwa na majeshi ya Idi Amin ambayo yangeweza kulitumia daraja hilo kushambulia upande wa pili.

Cc Nguruvi3 , Kichuguu, Pascal Mayalla , Shwari
 
@Elichoma ulituahidi kitabu mrejesho ukoje kuhusu kitabu mzee wangu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…