Vita ya Azania na Tambaza (1993 - 1994)

Vita ya Azania na Tambaza (1993 - 1994)

Kurunzi

JF-Expert Member
Joined
Jul 31, 2009
Posts
9,753
Reaction score
10,747
VITA YA AZANIA NA TAMBAZA (1993 - 1994)

Mwaka 1993 Jeshi la Sekondari ya Tambaza liliivamia Sekondari ya Azania kutokea Bonde la Jangwani nyuma ya Hospitali ya Muhimbili baada ya juhudi za kutama kusitisha mapigano kushindikana! Kufumba na kufumbua, askari wa Tambaza walirusha makombora na kuanza kulipua jengo la Maabara ya Kemia wakitumia Mabomu ya Petroli.

Wakati huo mimi nilikuwa Kidato cha Sita na mmoja wa viongozi katika Ushirika wa Kikristo wa Wanafunzi Tanzania (UKWATA) katika Tawi la Azania na Jangwani (Azajangwa). Nilikuwa pia kiongozi katika Serikali ya Wanafunzi ya Azania ambapo nilikuwa General Prefect!

Mimi na Kiongozi mwenzangu wa UKWATA aliyeitwa Enock Mayage, tuliitisha kikao cha viongozi wa vikundi vya dini kilichofanyika katika Ofisi ya UKWATA maarufu kama Chemba ya UKWATA. Viongozi waliohudhiria kikao kile walitoka ASA, UKWATA, TYCS, JUWAKWATA na DAMUSA. Pamoja na kutaka kuweka mikakati ya kuzuia vita, endapo tutavamiwa niliazimia kutumia kikao kile kuwashawishi wenzangu ili waumini wetu wasipigane.

Tukafikia muafaka wa kupeleka mapendekezo yetu kwa Mkuu wa Shule. Tulimshauri yeye aongee na Mkuu wa Shule ya Tambaza ili kiitishwe kikao cha viongozi wa vikundi vya dini na Serikali za Wanafunzi kutoka Shule zote mbili kwa majadiliano.

Wakati tukiwa katika Ofisi ya Shule, kijana mmoja wa Tambaza alipiga simu ya Shule akisema Jeshi lao liko njiani kuja kuivamia Azania. Kama kijana yule alitumia simu ya Shule au ya nyumbani kwao hatujui. Ingawa Kuna uwezekano alikuwa Mkazi wa Muhimbili Hivyo uwezekano mkubwa alitumia simu ya nyumbani kwao!

Baada ya taarifa ile, nilitoka nje na baada ya dakika 10 hivi, niliona utitiri wa vijana wa Tambaza wapatao 200 au hata 300 wakiibukia kutokea eneo ambalo sasa imejengwa MOI kile Muhimbili!

Safari hii, Tambaza walikuwa wanapambana bila kuwa na mmoja wa makamanda wao aliyeitwa Puza ambaye alifariki dunia miaka miaka mitatu nyuma kwa kunywa sumu. 'Jenerali Okelo' alikuwa mstaafu kwani alimaliza Shule mwaka 1989 au 1990.

Msela Shetani alikuwa amesahaulika katika Jeshi la Tambaza. Kikosi chake cha Tambaza International Smokers Association (TISA) kiliendelea kuwepo ingawa muda huo kilikuwa kimeanza kizidiwa umaarufu na Kikosi cha Nyau. Hata hivyo, kikosi cha Nyau hakikuwa na uwezo wa kupambana na Azania kwa sababu kilikuwa kimeandaliwa mahususi kwa ajili ya kupigana na makondakta wa daladala.

Mimi nilijitosa na nilikuwa mstari wa mbele katika kuongoza Jeshi la Uokozi kutoka Azania ambapo tulifanikiwa kuuzima moto ule kwa kutumia mchanga ndani ya dakika 10 tu pasipo kuleta madhara ye yote. Kutokana na ugeni wa mazingira, wapiganaji wa Tambaza walikwama katika uzio wa Jangwani walipotaka kukimbia. Majeshi ya Azania yalitumia kuni za kupikia zilizokuwa katika Bwalo la Shule kama silaha.

Mimi niliendelea kuwa mstari wa mbele katika mapambano yale nikifanya kazi ya kuwaokoa vijana wa Tambaza waliokuwa wamezidiwa ili wasiuliwe au wasiumizwe. Kwa kuwa nilikuwa Kiongozi wa Dini pale Azania, vijana wa Azania kila waliponiona na kusikia sauti yangu waliona aibu na hivyo waliacha kuwaumiza vijana wa Tambaza. Lile ni moja ya matukio ya kutisha ambayo kamwe sitayasahau maishani.

Vilevile, mimi naliona tukio lile kama moja ya matukio ambayo Mungu alinitia ujasiri kuwa mtetezi hata kwa adui. Ninaamini kuwa Mungu alianza kuniandaa tangu zamani kwa ajili ya wajibu huu wa utetezi ninaoufanya sasa!

Je, ni kitu gani kilchokushangazs kuhusiana na tukio lile? Je, wewe ni miongoni mwa watu walioshiriki katika mapigano yale? Je, wewe ni miongoni mwa watu walioshuhudia kwa mbali? Je, unakumbuka nini kuhusiana na vita ile?

Je, ulikuwa unajua kuwa vita ile ndio ambayo iliyosababisha Serikali kuifunga kabisa Shule ya Tambaza na Wanafunzi wake kuhamishiwa Shule nyingine za Serikali ikiwemo Kwiro? Baadaye Serikali ikaifanya Tambaza kuwa High School na kuwa mchanganyiko. Ilipofunguliwa wakaletwa wanafunzi wapya wa Kidato cha Tano na kuongezwa michepuo ambayo huko awali haikuwepo ya HGL, HGK, EGM, CBG, nk.

Wakati Tambaza inafungwa, wanafunzi wa Kidato cha Sita waliokuwepo waliruhusiwa kumalizia pale pale Tambaza. Walikuwa wakisoma michepuo ya PCM na PCB na kulikuwa na wasichana wachache. Wanafunzi wote wa O' Levels walihamishwa.

Hakika tunasafiri na tumetoka mbali sana katika maisha haya!

Mwana Kondoo Ameshinda! Tumfutate!
Askofu Emmaus Bandekile Mwamakula

Soma pia Ebu tujikumbushe enzi za tambaza na azania kabla tambaza kubadilishwa kuwa high school
 
Khaa; kumbe ndio wewe askofu! Asante sana kwa taarifa na kumbukumbu hi, nalikumbuka sna hili tukio hasa hao vijana waliokua wanatembea na bisi bisi kwa ajili ya kuwatoboa utumbo makonda wa daladala!
 
Vijana wa Tambaza walikuwa ni wa ajabu sana, nilikuwa Azania wakati huo form two na siku moja naelekea Manzese kwenye tuition mara paap naanza kushambuliwa kisa tu nimevaa uniform za Azania. Ile fujo iliwasambaratisha na wakatawanywa mikoani na Azania wakapoa na mzee Kwayu chini ya Mchwa mpaka discpline master.

Ajabu, matokea ya form form 4 kutoka tu, nikapangiwa Songea Boys, huko nikaa miezi miwili na headmaster wa pale akanihamishia Tambaza form 5 kisa tu eti pale Songea boys kulikuwa na vijana wa Tambaza wengi kitu ambacho headmaster hakupenda kuendeleza chuki. Nikarudi zangu form 5 hadi 6 kumalizia huko huko Tambaza... muda huo Ilikuwa tayari imefanywa mseto na hakuna tena fujo na inapokea form 5 na 6 tu.
 
Vijana wa Tambaza walikuwa ni wa ajabu sana, nilikuwa Azania wakati huo form two na siku moja naelekea Manzese kwenye tuition mara paap naanza kushambuliwa kisa tu nimevaa uniform za Azania. Ile fujo iliwasambaratisha na wakatawanywa mikoani na Azania wakapoa na mzee Kwayu chini ya Mchwa mpaka discpline master. Ajabu, matokea ya form form 4 kutoka tu, nikapangiwa Songea Boys, huko nikaa miezi miwili na headmaster wa pale akanihamishia Tambaza form 5 kisa tu eti pale Songea boys kulikuwa na vijana wa Tambaza wengi kitu ambacho headmaster hakupenda kuendeleza chuki... Nikarudi zangu form 5 hadi 6 kumalizia huko huko Tambaza... muda huo Ilikuwa tayari imefanywa mseto na hakuna tena fujo na inapokea form 5 na 6 tu...
Box 2 ni kweli wa Tambaza waliletwa pale,nadhani Headmaster ulimkuta Mbao au Kusilawe
 
Je, ulikuwa unajua kuwa vita ile ndio ambayo iliyosababisha Serikali kuifunga kabisa Shule ya Tambaza na Wanafunzi wake kuhamishiwa Shule nyingine za Serikali ikiwemo Kwiro?
Hamna bhana...

Vita ya kutisha ilikuwa ni dhidi ya Jitegemee! Kama kumbukumbu zangu zipo sawa, ilikuwa wakati wa michuano ya UMISETA ambapo Tambaza walikutana na Jitegemee... nadhani nusu fainali.

Wakati huo Jitegemee walikuwa wanapiga soka la kufa mtu!! Kwenye ile mechi , Tambaza walikuwa wameshajiandaa na ugomvi huko huko. Vurugu za kufa mtu pale Shamba la Bibi, enzi pakiitw Uwanja wa Taifa zilianza baada ya Tambaza kupigwa bao.

Vurugu zilikuwa kubwa kiasi kwamba Barabara ya Chang'ombe na Nyerere (enzi hizo ikiitwa Pugu) kuelekea K/koo ilikuwa full mtiti. Kufika mitaa ya Bora, machizi wakavamia daladala, sasa Konda si akataka kuleta ubabe kama ilivyokuwa makonda wa enzi zile.

Konda kapanda zake juu kwenye career lengo lake akachukue silaha... wahuni wamamporoposha huko huko, kufika chini, akagombaniwa kama mpira wa kona hali iliyopelekea kifo chake.

Serikali hapo ndo wakaona hii sasa ishakuwa too much, ndipo shule ikapigwa makomeo na wanafunzi wote kuhamishiwa mikoani!!

Tambaza walikuwa na ugomvi usioisha dhidi ya Azania. Lakini katika utukutu wao kuna siku wakaenda kujichanganya kwa watoto wa Kinondoni Muslim! Hiyo siku Watoto wa Tambaza walipoteana pale Biafra manake kila mmoja aliingilia kwake!!

Kwa anaowajua Kinondoni Muslim ya wakati ule nadhani atanielewa manake majamaa yalikuwa yamepinda, hakuna tena!
 
Hamna bhana...

Vita ya kutisha ilikuwa ni dhidi ya Jitegemee! Kama kumbukumbu zangu zipo sawa, ilikuwa wakati wa michuano ya UMISETA ambapo Tambaza walikutana na Jitegemee... nadhani nusu fainali.

Wakati huo Jitegemee walikuwa wanapiga soka la kufa mtu!! Kwenye ile mechi , Tambaza walikuwa wameshajiandaa na ugomvi huko huko. Vurugu za kufa mtu pale Shamba la Bibi, enzi pakiitw Uwanja wa Taifa zilianza baada ya Tambaza kupigwa bao.

Vurugu zilikuwa kubwa kiasi kwamba Barabara ya Chang'ombe na Nyerere (enzi hizo ikiitwa Pugu) kuelekea K/koo ilikuwa full mtiti. Kufika mitaa ya Bora, machizi wakavamia daladala, sasa Konda si akataka kuleta ubabe kama ilivyokuwa makonda wa enzi zile.

Konda kapanda zake juu kwenye career lengo lake akachukue silaha... wahuni wamamporoposha huko huko, kufika chini, akagombaniwa kama mpira wa kona hali iliyopelekea kifo chake.

Serikali hapo ndo wakaona hii sasa ishakuwa too much, ndipo shule ikapigwa makomeo na wanafunzi wote kuhamishiwa mikoani!!

Tambaza walikuwa na ugomvi usioisha dhidi ya Azania. Lakini katika utukutu wao kuna siku wakaenda kujichanganya kwa watoto wa Kinondoni Muslim! Hiyo siku Watoto wa Tambaza walipoteana pale Biafra manake kila mmoja aliingilia kwake!!

Kwa anaowajua Kinondoni Muslim ya wakati ule nadhani atanielewa manake majamaa yalikuwa yamepinda, hakuna tena!

I second this...
Sababu nilikuwepo hiyo siku uwanja wa taifa....
 
MImi nilikuwa Mkoani huko, tuliwapokea watoto wa TAMBAZA kama 20 hv. Sa sijui ilikuaje niliishia kuwaona yori.... yori... tu
 
MImi nilikuwa Mkoani huko...... tuliwapokea watoto wa TAMBAZA kama 20 hv... sa sijui ilikuaje niliishia kuwaona yori.... yori... tu
Yaani umesema kweli,shule za mkoani Ni kiboko,Mimi nilisoma birding mkoani form 1na 2,Kuingia form 3 nikahamishiwa day shule ambayo ndio inaonekana ya kibabe,mi kufka pale nilishangaa Sana niliishia kuwaona yoriyori kisemo chako!nikawa mpoleee maana watukutu wenzangu siwaoni nikaishia kuwa msongo,Ni Mimi na vitabu
 
Zamani huu ubabe wa mashule
Mkiwa shuleni.... Sijui ulikuwa ushamba au

Ova
 
Zamani walikuwa wana soma wazee sana kabisaaa! kutoka kijijini huko mikoani hasa Kanda ya ziwa !! ubabe wa kishambaaa uliwajaa !! siku hizi mambo ni tofauti vitoto vinasoma vidogooo!! hata mkononi hakajai! yaani zamani zile ukienda form one kuna wengine ni umri wa Baba yako kabisaa!

walikuwa wana rudia mnooo!! miaka saba mtu anarudia shule yamsingi tu!...walikuwa na jeuri sana ya hata kumtia Rais jambajamba Ikulu, hasa enzi za Nyerere, na hata Mwinyi, maana walikuwa wanalingana kwa umri!! walikuwa wanaona Rais ni mwenzao tu!

Hadi kijana mmoja hivi!! ni marehemu sasa aliitwa Tuntemeke Sanga huyu bana alimwambia Nyerere ana taka cheo chake cha Urais sababu tu ni kuwa walilingana kiumri!!.....na huyu sanga alisoma kitabu kimoja cha mwandishi Camala Laye aka kimaliza chote!!

Basi akajiona Bonge la msomi shujaa!! harakati zenyewe alikuwa hajui halafu alikuwa muoga flani hivi!!..akamtisha nyerere sababu ya kulewa kiingereza!! alichokipata heee!!! hadi Mkewe alimkimbia!! yaani Zamani walikuwa na ubabe wa kishamaba sana!

Sasa leo katoto miaka 19 tu kana degree mbili!! katamdindishia Rais Samia???.....kwanza atakalaani tu kakafie mbele huko!! wala hasemi chochote haka hata kakisimama jukwaani kutkana na kutoa misimamo hakaonekani hakana kikoromo!

kuna jamaa moja la Musoma liliitwa Mantiku Mantale la Musoma huko miaka hiyo mwee!! liliandamana mpaka Ikulu...kumtishia Nyerere! Ajiuzuru!! akaliambia sawa anisubiri hapo!! Basi julius alitoka na viboko vyenye pilipili kumi kidogo!!! alilichapa lile jamaa heee!! then!

likarudishwa kijijini kwao faster na Land rover 109!! sasa kila siku likawa lina report kwa mkuu wa wilaya ya Musoma! likashika adabu mpaka lilipokufa halikunyanyuka tena!! ...kitu kikubwa kilichokuwa kinachangia migomo ni Huduma za kishule za bure

hizi walikuwa wakipatiwa wana funzi wa serikali bure kuanzia chakula, Malazi, Mavazi, Usafiri wa bure unatumia Government warrant kutoka kwenu mpaka shule kwenda na kurudi bure, pia vitabu vya ziada na kiada, Madaftri bureee! unapewa!

haya yoote ni kwa kuwa serikali iliwataka wakaitumikie!! na uhakika wa ajira ulikuwepo tena una chagua unakotaka weye mwenyewe!! sometimes unakwenda fanya Ikulu kabisaa ndo kina pinda hao! ..

lkn ktk hayo yoote kazi za Polisi, Jeshi, Ualimu, Magereza watu walivibeza wazi wazi eti ni kazi za hovyo! majasho, hazina heshima na walizikataa katakata hawakutaka hata kuzisikia, hata ukichaguliwa huko wanakudharau sana mitaani!

Vita ya Kagera watu hasa wa mikoa ya pwani walikuwa wana kataa tu maksudi!! wengine wanatoroka maksudi tu, wengine wanakaa upande waadui maksudi tu!! isipokuwa Wakurya, Wasukuma, Wahehe tu!!

hawa bana ndo walijitoa kwa moyo wooote bega kwa bega kutwangana na Idd Amini!.....ikibidi kavu kavu!! hawakujali kuvaa Buti! wala Combat! wao ilikuwa ni kusonga mbere tu! liwalo na liwe!....sometimes waliona buti ni nzito zinawachelewesha kufika Entebe.

haya yoote ni ili mradi tu!! Nyerere awe salama!...siyo hawa wa leo wana muacha jiwe anakufa kwa COVID! isiyo sema kirahisi tu!..eti wao wanabaki salama nyuma huku! naya semahaya mjue kuwa tulidhamilia!
 
Hamna bhana...

Vita ya kutisha ilikuwa ni dhidi ya Jitegemee! Kama kumbukumbu zangu zipo sawa, ilikuwa wakati wa michuano ya UMISETA ambapo Tambaza walikutana na Jitegemee... nadhani nusu fainali.

Wakati huo Jitegemee walikuwa wanapiga soka la kufa mtu!! Kwenye ile mechi , Tambaza walikuwa wameshajiandaa na ugomvi huko huko. Vurugu za kufa mtu pale Shamba la Bibi, enzi pakiitw Uwanja wa Taifa zilianza baada ya Tambaza kupigwa bao.

Vurugu zilikuwa kubwa kiasi kwamba Barabara ya Chang'ombe na Nyerere (enzi hizo ikiitwa Pugu) kuelekea K/koo ilikuwa full mtiti. Kufika mitaa ya Bora, machizi wakavamia daladala, sasa Konda si akataka kuleta ubabe kama ilivyokuwa makonda wa enzi zile.

Konda kapanda zake juu kwenye career lengo lake akachukue silaha... wahuni wamamporoposha huko huko, kufika chini, akagombaniwa kama mpira wa kona hali iliyopelekea kifo chake.

Serikali hapo ndo wakaona hii sasa ishakuwa too much, ndipo shule ikapigwa makomeo na wanafunzi wote kuhamishiwa mikoani!!

Tambaza walikuwa na ugomvi usioisha dhidi ya Azania. Lakini katika utukutu wao kuna siku wakaenda kujichanganya kwa watoto wa Kinondoni Muslim! Hiyo siku Watoto wa Tambaza walipoteana pale Biafra manake kila mmoja aliingilia kwake!!

Kwa anaowajua Kinondoni Muslim ya wakati ule nadhani atanielewa manake majamaa yalikuwa yamepinda, hakuna tena!
Chige, upo sahihi ingawa ilikuwa ni nusu fainali kati ya jitegemee na St Anthony's mbagala pale shamba la bibi uwanja wa taifa, kama sijakosea Tambaza walitaka timu ya St Anthony's mbagala washinde ili wakutane nao fainali katika umiseta. Jitegemee walitumia fursa ya kuwa na maaskari wao wajeda kudhibiti vurugu za vijana wa Tambaza, Kipindi hicho daladala zilikuwa ni chai maharage ( KIA ).

Uharibifu mkubwa sana ulifanyika ikiwemo kifo cha kondakta wa daladala, nakumbuka wanafunzi wa jitegemee walikuwa wakivua na kuficha nguo za sare za shule kuwahofia wenzao wa Tambaza.
 
Back
Top Bottom