Vita ya Azania na Tambaza (1993 - 1994)

Wewe upo sahihi ilikuwa ni nusu fainali ya jitegemee na st Anthony
Ndio zile vurugu serikali ikavunja o level ya tambaza.maana siku ya tukio nilikuwepo wale watoto watambaza kipinde bangi ziliwavuruga akili sana.

Walikuwa na viwembe wanachanga tu yaani sitasahau ile siku nilikimbia ile michanga ya taifa niliona kama lami.
 
Hizo shule ziliduma sana kwa ukorofi...
Walikua wanapewa chai na skonzi wanaoingia asubuhi wanakunywa na wababe wanaiba hizo skonzi wanaenda kuwauzia mamalishe.
Waliokua wanaingia mchana walikua wanachakula pia.
Kazi ikaja walokunywa chai na wanataka wale na mchana ambapo sio Chao Ili wawahi tution magomeni kwa MAKUMAKU.
Huyu mwl NYAU niliwahi kutana nae maeneo ya Sayansi kijitonyama saa nane usiku anapiga mishe za dereva Taxi nilishangaa!
 
Hapa umeleta chai,Matiko Matale aliofanya harakati zake 1990 wakati huo rais ni Aly Hassan Mwinyi,wakati huo Nyerere alishastaafu.Matiko Matale alikuwa mkuu wa shule ya Beroya huko Songea na alikuwa mwenyekiti wa Chadema kanda ya huko huko Songea.
 
Hapa umeleta chai,Matiko Matale aliofanya harakati zake 1990 wakati huo rais ni Aly Hassan Mwinyi,wakati huo Nyerere alishastaafu.Matiko Matale alikuwa mkuu wa shule ya Beroya huko Songea na alikuwa mwenyekiti wa Chadema kanda ya huko huko Songea.
Haroo! muraaa umekurupuka unachua kure Nchini Mara kure, kina Matiku Joseph Mantare!! (siyo Matale! umeitaja kipare) wako ni wengiii sana tena sana!!...wanakura kichure kya Pure!

Wamesoea kubhita tiricha wanaingia taracha!! huyo Mkuu wa shule ya msingi sijui wapi huko...ni wa kwenu huko huko!!Mwamba huyu hapa
 
Hii nimeipenda, kwAni humu jamvini hakuna aliyesoma kino muslimu? Atupe fidibaki
 
Enzi hizo hakukuwa na social media...na hata TV zilikuwa bado Sana....ugomvi ilikuwa njia ya kuwa z popular among vijana....TV zikaja na bongofleva halafu social media zikaja ikabaki history tu
 
hao jamaa watakuwa watu wazima sasa - miaka 50+; sasa sijui washapata busara kwa umri huo.
 
Zamani walikuwa wana soma wazee sana kabisaaa! kutoka kijijini huko mikoani hasa Kanda ya ziwa !!
unakuta jamaa kidevu kimekomaa kwa kukwangua ndevu 😀 😀 ngoma form II
 
unakuta jamaa kidevu kimekomaa kukwangua ndevu 😀 😀 ngoma form II
Zamani acha kabisa mkuu,jitu linaanza primary lina miaka 18 linafika O level uso umekomaa,ana bonge la nyayo mguuni kiatu namba 46,ndevu mpaka kifuani alafu shingoni bonge la kolomeo kama balbu zile za zamani,hapo ndo unaambiwa mwamba yupo form 2[emoji125][emoji125][emoji125][emoji125]
 
Smaki umetisha!!!
 
unakuta jamaa kidevu kimekomaa kwa kukwangua ndevu 😀 😀 ngoma form II
Miaka ile ukichaguliwa form one, shule za serikali mweee!! wengi walikuwa wazee! shikamoo zinashuka kabisaa! Mfano Li-Kiranja la Bwalo/Mkuu/Kilimo/Sijui- Ulinzi, mawee!...

yalipanda hewani, msuri wa nguvu utadhani dume, ofisi kalii! safiii!! halafu limekomelea suti!...sasa siku ya kudeki Bwalo ndo kichekesho!....Turuhaga Babishakirao!! uko wapi kwanza! lkn uliwasaidia sana vijana!

Njoo hapa ule kiti moto!
 
Halafu kinakuja shule hiyo hiyo ki form one kina miaka 13!!
 
Azania Tambaza vita yao ya miaka mingiiii..
Shida Tambaza huwa wanajiona wao wazaliwa wa mjini Azania wengi kutoka mikoani…
Hata Zanaki na Jangwani ni yale yale
Zanaki wanajiona wazaliwa wa mjini wanaona Jangwani washamba wa mikoani wengi….Enzi zetu tuliwanyoosha Zanaki (soft soft yao walijua hawajui)
 
Umepiga ule mmea mwingi Sana tata
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…