Vita ya DC Ubungo na Makahaba: Mgongano wa sheria, haki na maadili

Vita ya DC Ubungo na Makahaba: Mgongano wa sheria, haki na maadili

Joined
Apr 8, 2023
Posts
30
Reaction score
23
Najua kwa sasa hoja na habari kuu ni "Mauaji ya Asimwe" na nitakuja kusema kuhusu hili, lakini kwa vile sikupata fursa ya kutoa maoni yangu kuhusu suala la DC Ubungo kukamata watu na kuwaweka ndani kwa kosa la "kufanya ukahaba", tena kwenye siku ya siku kuu huku akiagiza mara baada ya siku kuu wafikishwe mahakamani na mahakama ichukue hatua za kisheria, naomba mnivumilie niulize maswali machache ya mantiki na ufahamu.

Kwanza ni namna "ukamataji" ulivyofanyika. Mheshimiwa DC amekwenda na askari na vyombo vya habari kuwakamata "watuhumiwa wa ukahaba". Kweli ukahaba ni kosa kwa sheria za Tanzania na hata kwa maadili yetu tu, si jambo linalokubalika; lakini nilidhani kwa misingi ya kisheria, mtuhumiwa anazo haki zake zinazopaswa kulindwa hadi anapothibitika kuwa na hatia! Kama tumemuweka "mtuhumiwa" mbele ya vyombo vya habari kwa "tuhuma", tukamshikilia mahabusu kwa saa 24, na kisha mahakama ikamkuta "hana hatia" baada ya kumsikiliza na kugundua huenda alikuwa 'anapita tu njia na akawa anasalimiana na mtu wakati DC na kikosi kazi nao wanafika "kukamata", tunamfidiaje huyu kwa udhalilishaji na madhara yaliyotokea kwenye jamii kwake na kwa familia yake!!? Kwanini tumemhukumu (kwenye media/public) kabla mahakama haijatoa hukumu!!? Tumetaka kuonyesha tu kwamba tunakamata "makahaba" bila kulinda haki za kisheria za watu kwa sababu gani!!?

Kisha kuna suala la "ushahidi". Hivi tunao ushahidi wa kutosha kuthibitisha "pasipo kuacha shaka yoyote" kwamba wafu wale tuliowakusanya kwa mtutu wa bunduki, mbele ya wanahabari, na kuwaweka rumande kwa tuhuma za "kufanya ukahaba" walikuwa kweli "wakifanya ukahaba" kwenye eneo lile!!? Tunaweza kuthibitisha hili kwa kujibu wa sheria tena pasina kuacha shaka, au tumewakamata na kuuambia umma kwamba ni "makahaba" lakini tutatafuta shitaka litakalofaa kwa mazingira yale ili tuweze kuwafikisha mahakamani kwalo!!? Busara hapa ya Mheshimiwa DC na Mwanasheria wa Halmashauri zinatuelekezaje!!? Au ndiyo tumeamua we are "all in one" yaani wapelelezi ni sisi, wakamataji ni sisi, washitaki ni sisi, mahakimu ni sisi, wazee wa baraza ni sisi, mabwana jela ni sisi sisi!? Nawaza tu!

Hivi sheria ya Tanzania inasemaje kuhusu "ukamataji" wa makosa ya jinai!!? Tunakamata ndipo tuanze upelelezi au tunapeleleza, tunapata ushahidi, ndipo tunakamata ili tushitaki!!? Kama ni kamata kwanza, peleleza baadaye, tunajiepushaje na mashtaka yatakayofuatia kushindwa kesi hizi (jambo ambalo naona kama ushahidi wa "ukahaba" wa makahaba wetu hawa utakuwa mgumu)!!?

Anyway, aliwahi kusema Mwalimu Nyerere kwamba "sheria na haki ni mawili tofauti" na sasa nadhani naanza kuelewa.

Wasalaam!!!

PIA SOMA
- Tetesi: - Waliokamatwa kwa tuhuma za kununua Makahaba Ubungo kumburuza mahakamani Mkuu wa Wilaya kwa kudhalilishwa! Wadai walifuatwa Guest!

- Kuna kesi ya udhalilishaji kama wale walioonekana kwenye video ya kukamata makahaba watapata mwanasheria mzuri

- Vigezo gani anavitumia DC wa wilaya ya Ubungo, Hassan Bomboko kuvamia kumbi za starehe na nyumba za wageni kukamata watu anaodai ni makahaba?
 
Ndo kero kubwa sana inawezekana ndo maana kaweka nguvu uko , itakuwa akuna matatizo mengine
 
Najua kwa sasa hoja na habari kuu ni "Mauaji ya Asimwe" na nitakuja kusema kuhusu hili, lakini kwa vile sikupata fursa ya kutoa maoni yangu kuhusu suala la DC Ubungo kukamata watu na kuwaweka ndani kwa kosa la "kufanya ukahaba", tena kwenye siku ya siku kuu huku akiagiza mara baada ya siku kuu wafikishwe mahakamani na mahakama ichukue hatua za kisheria, naomba mnivumilie niulize maswali machache ya mantiki na ufahamu.

Kwanza ni namna "ukamataji" ulivyofanyika. Mheshimiwa DC amekwenda na askari na vyombo vya habari kuwakamata "watuhumiwa wa ukahaba". Kweli ukahaba ni kosa kwa sheria za Tanzania na hata kwa maadili yetu tu, si jambo linalokubalika; lakini nilidhani kwa misingi ya kisheria, mtuhumiwa anazo haki zake zinazopaswa kulindwa hadi anapothibitika kuwa na hatia! Kama tumemuweka "mtuhumiwa" mbele ya vyombo vya habari kwa "tuhuma", tukamshikilia mahabusu kwa saa 24, na kisha mahakama ikamkuta "hana hatia" baada ya kumsikiliza na kugundua huenda alikuwa 'anapita tu njia na akawa anasalimiana na mtu wakati DC na kikosi kazi nao wanafika "kukamata", tunamfidiaje huyu kwa udhalilishaji na madhara yaliyotokea kwenye jamii kwake na kwa familia yake!!? Kwanini tumemhukumu (kwenye media/public) kabla mahakama haijatoa hukumu!!? Tumetaka kuonyesha tu kwamba tunakamata "makahaba" bila kulinda haki za kisheria za watu kwa sababu gani!!?

Kisha kuna suala la "ushahidi". Hivi tunao ushahidi wa kutosha kuthibitisha "pasipo kuacha shaka yoyote" kwamba wafu wale tuliowakusanya kwa mtutu wa bunduki, mbele ya wanahabari, na kuwaweka rumande kwa tuhuma za "kufanya ukahaba" walikuwa kweli "wakifanya ukahaba" kwenye eneo lile!!? Tunaweza kuthibitisha hili kwa kujibu wa sheria tena pasina kuacha shaka, au tumewakamata na kuuambia umma kwamba ni "makahaba" lakini tutatafuta shitaka litakalofaa kwa mazingira yale ili tuweze kuwafikisha mahakamani kwalo!!? Busara hapa ya Mheshimiwa DC na Mwanasheria wa Halmashauri zinatuelekezaje!!? Au ndiyo tumeamua we are "all in one" yaani wapelelezi ni sisi, wakamataji ni sisi, washitaki ni sisi, mahakimu ni sisi, wazee wa baraza ni sisi, mabwana jela ni sisi sisi!? Nawaza tu!

Hivi sheria ya Tanzania inasemaje kuhusu "ukamataji" wa makosa ya jinai!!? Tunakamata ndipo tuanze upelelezi au tunapeleleza, tunapata ushahidi, ndipo tunakamata ili tushitaki!!? Kama ni kamata kwanza, peleleza baadaye, tunajiepushaje na mashtaka yatakayofuatia kushindwa kesi hizi (jambo ambalo naona kama ushahidi wa "ukahaba" wa makahaba wetu hawa utakuwa mgumu)!!?

Anyway, aliwahi kusema Mwalimu Nyerere kwamba "sheria na haki ni mawili tofauti" na sasa nadhani naanza kuelewa.

Wasalaam!!!

PIA SOMA
- Tetesi: - Waliokamatwa kwa tuhuma za kununua Makahaba Ubungo kumburuza mahakamani Mkuu wa Wilaya kwa kudhalilishwa! Wadai walifuatwa Guest!

- Kuna kesi ya udhalilishaji kama wale walioonekana kwenye video ya kukamata makahaba watapata mwanasheria mzuri

- Vigezo gani anavitumia DC wa wilaya ya Ubungo, Hassan Bomboko kuvamia kumbi za starehe na nyumba za wageni kukamata watu anaodai ni makahaba?
⚖️Justice for Asimwe#
 
Uzururaji pia ni uzushi kwasababu kama umemkamata mtu mchana wa jua kali utasemaje kuwa alikuwa anazurura. Ushahidi wa uzururaji pia ni mgumu, wanaweza wakawashitaki kwa kuwaonea tu
Ndio maana hata mimi nikauliza huo uzururaji ni upi yani kama umemkamata mtu saa 2 usiku kwamba alikuwa anazurura ni uhuni tu
 
Utasema mtu anazurula na je akisema anafanya utalii wa ndani utamshitaki vipi
 
Najua kwa sasa hoja na habari kuu ni "Mauaji ya Asimwe" na nitakuja kusema kuhusu hili, lakini kwa vile sikupata fursa ya kutoa maoni yangu kuhusu suala la DC Ubungo kukamata watu na kuwaweka ndani kwa kosa la "kufanya ukahaba", tena kwenye siku ya siku kuu huku akiagiza mara baada ya siku kuu wafikishwe mahakamani na mahakama ichukue hatua za kisheria, naomba mnivumilie niulize maswali machache ya mantiki na ufahamu.

Kwanza ni namna "ukamataji" ulivyofanyika. Mheshimiwa DC amekwenda na askari na vyombo vya habari kuwakamata "watuhumiwa wa ukahaba". Kweli ukahaba ni kosa kwa sheria za Tanzania na hata kwa maadili yetu tu, si jambo linalokubalika; lakini nilidhani kwa misingi ya kisheria, mtuhumiwa anazo haki zake zinazopaswa kulindwa hadi anapothibitika kuwa na hatia! Kama tumemuweka "mtuhumiwa" mbele ya vyombo vya habari kwa "tuhuma", tukamshikilia mahabusu kwa saa 24, na kisha mahakama ikamkuta "hana hatia" baada ya kumsikiliza na kugundua huenda alikuwa 'anapita tu njia na akawa anasalimiana na mtu wakati DC na kikosi kazi nao wanafika "kukamata", tunamfidiaje huyu kwa udhalilishaji na madhara yaliyotokea kwenye jamii kwake na kwa familia yake!!? Kwanini tumemhukumu (kwenye media/public) kabla mahakama haijatoa hukumu!!? Tumetaka kuonyesha tu kwamba tunakamata "makahaba" bila kulinda haki za kisheria za watu kwa sababu gani!!?

Kisha kuna suala la "ushahidi". Hivi tunao ushahidi wa kutosha kuthibitisha "pasipo kuacha shaka yoyote" kwamba wafu wale tuliowakusanya kwa mtutu wa bunduki, mbele ya wanahabari, na kuwaweka rumande kwa tuhuma za "kufanya ukahaba" walikuwa kweli "wakifanya ukahaba" kwenye eneo lile!!? Tunaweza kuthibitisha hili kwa kujibu wa sheria tena pasina kuacha shaka, au tumewakamata na kuuambia umma kwamba ni "makahaba" lakini tutatafuta shitaka litakalofaa kwa mazingira yale ili tuweze kuwafikisha mahakamani kwalo!!? Busara hapa ya Mheshimiwa DC na Mwanasheria wa Halmashauri zinatuelekezaje!!? Au ndiyo tumeamua we are "all in one" yaani wapelelezi ni sisi, wakamataji ni sisi, washitaki ni sisi, mahakimu ni sisi, wazee wa baraza ni sisi, mabwana jela ni sisi sisi!? Nawaza tu!

Hivi sheria ya Tanzania inasemaje kuhusu "ukamataji" wa makosa ya jinai!!? Tunakamata ndipo tuanze upelelezi au tunapeleleza, tunapata ushahidi, ndipo tunakamata ili tushitaki!!? Kama ni kamata kwanza, peleleza baadaye, tunajiepushaje na mashtaka yatakayofuatia kushindwa kesi hizi (jambo ambalo naona kama ushahidi wa "ukahaba" wa makahaba wetu hawa utakuwa mgumu)!!?

Anyway, aliwahi kusema Mwalimu Nyerere kwamba "sheria na haki ni mawili tofauti" na sasa nadhani naanza kuelewa.

Wasalaam!!!

PIA SOMA
- Tetesi: - Waliokamatwa kwa tuhuma za kununua Makahaba Ubungo kumburuza mahakamani Mkuu wa Wilaya kwa kudhalilishwa! Wadai walifuatwa Guest!

- Kuna kesi ya udhalilishaji kama wale walioonekana kwenye video ya kukamata makahaba watapata mwanasheria mzuri

- Vigezo gani anavitumia DC wa wilaya ya Ubungo, Hassan Bomboko kuvamia kumbi za starehe na nyumba za wageni kukamata watu anaodai ni makahaba?
Kwa Tanzania kuna "makosa" ya aina mbili inabidi wakamataji/wanaohusika watumie mbinu mbadala kuyamaliza, nayo ni:-

1. Ukahaba na ushoga, hawa watu ukitumia njia "halali" za kisheria badala ya kuwamaliza utajikuta unawapa air time ya bure na kupromote biashara hiyo bila wewe mwenyewe kudhamiria. Mahakamani ni vigumu sana sana kuwakuta na hatia hivyo lazima jamuhuri itoke mahakamani kichwa kikiwa chini


2. Panya road na vibaka wa mtaani/wakabaji, hawa nao wasipombambikiziwa vidhibiti mara nyingi mashahidi hawajitokezi mahakamani hivyo mahakama huwaachia huru halafu wakirudi jamii iliyoshindwa kwenda kutoa ushahidi wanaanza kulalamikia vyombo vya dola

Namna ya kumaliza matatizo haya

Njia ni moja tu, kiundwe kikosi kazi maalumu ambacho kitaapa kabisa kabisa kutenda haki (sio haki ya kisheria) kwa watakayethibisha beyond reasonable doubt wanamalizana naye mtaani kimya kimya

Makahaba wanajulikana mtaani, mashoga wanajulikana mtaani, panya road/vibaka/wakabaji wanajulikana mtaani na makundi yote haya polisi kwasababu ya doria zao nao wanawafahamu kwa sura, kwa majina, nyumba wanazoishi. Polisi wanachokosa tu (ambacho ni kugumu sana) ni ushahidi wa kuithibitishia mahakama kuwa huyu kweli ni mkosaji kwasababu ya aina ya makosa yao

Mbinu ya "kumalizana nao" kimya kimya ikitumika ujumbe utafika kwa haraka zaidi na taratibu vitendo hivi vitakoma na hatimaye kuisha kabisa kwenye jamii kwasababu hakuna anayependa kumalizwa kimya kimya.

Siku hizi mitaa mingi ya uswahilini sehemu zenye guest house ukipita jioni giza utasikia "shemeji njoo nikwambie kitu" hii sio sawa
 
Back
Top Bottom