Vita ya Diamond na Alikiba ilivyoua nyimbo kali za Bongo Fleva zilizotoka mwezi septemba

Rosh Hashannah

JF-Expert Member
Joined
Sep 13, 2017
Posts
3,415
Reaction score
2,043
Kuna msemo unasema mafahari wawili wapiganao ziumiazo nyasi, huu msemo naufananisha na upinzani wa kimuziki uliopo baina ya wasanii wakubwa wa muziki wa Bongo Fleva, nchini Tanzania, Alikiba na Diamond Platnumz.


Alikiba na Diamond Platnumz

Upinzani ambao kwa upande mwingine umekuwa na faida kubwa kwa wasanii hao kwani wamekuwa wakipata shows, Matangazo na kuuza nyimbo kwa wingi mitandaoni hayo yote ni matunda ya uhasimu uliopo kati yao.

Lakini upinzani huo kwa kiasi fulani umekuwa ukiwaathiri wasanii wengine wakubwa na wachanga ambao nao wanapambana kila siku kuweza kupenya kwenye soko muziki.

Nakumbuka kipindi nikiwa Dodoma nilipata bahati ya kuongea na Mbunge wa Mtama, Mhe Nape Nnauye na kwenye mahojiano yake alizungumzia bifu iliyopo kati ya Diamond na Alikiba akiifananisha na upinzani wa timu kongwe za mpira wa miguu hapa nchini Simba na Yanga.

Kwa sababu gani Mhe. Nape aliwafananisha Diamond na Alikiba kama Simba na Yanga?Jibu ni kwamba timu hizo ndio zenye mashabiki wengi nchini ambapo zaidi ya asilimia 98% ya Watanzania ni mashabiki wa timu hizo huku timu nyingine zikibangaiza mashabiki.

Kilichomsukuma Nape Kufananisha hivyo ukweli ni kwamba uwepo wa upinzani wa kimuziki kati ya Diamond na Alikiba umepelekea baadhi ya Wasanii kukosa kabisa kuwa na mashabiki damdam (Loyal Fans) na kujikuta mashabiki wengi wakijigawa katika pande mbili za uteam Diamond na Alikiba.

Sio mbaya sana kwenye muziki wetu lakini tukubali kuwa kuna wasanii wa kizazi kijacho ambao ni wakali na kwa sasa walitakiwa wapate sapoti kubwa kutoka kwa mashabiki ili kuonesha vipaji vyao ila wanakosa kuonekana.

Pia wapo wasanii wengine wakubwa na wametoa ngoma kali ila wameshindwa kusikilizwa na mashabiki hii yote ni kwa sababu kuna nyimbo mpya za Diamond na Alikiba zimetoka na mashabiki ndio wale wale wa Simba na Yanga ambao hawana muda kutazama mechi ya Ndanda FC vs Majimaji FC.

Hapa chini nimeorodhesha nyimbo 6 kali za wasanii wakubwa, ambazo zimetoka ndani ya mwezi septemba, lakini hazijapata mapokezi mazuri baada ya Alikiba kuachia wimbo wake wa Seduce Me na Diamond Platnumz kuachia wimbo wa ‘Zilipendwa’ akiwa na kundi zima la WCB na wimbo wake mpya wa Hallelujah aliowashirikisha Morgane Heritage aliouachia mwishoni wa mwezi septemba.

1-Me and You- Jay Moe.(wiki mbili views 67,653+)



2-MAKUzi By Nay wa Mitego.(Wiki mbili views 162,112+)



3-Kiutani Utani- Young Dee.(Wiki mbili views 202,124+)


4-Kihasara by Nikki wa Pili Ft Chin Bees.(Wiki moja na siku 5 ina views 100,433+)


5-Barnaba- Mapenzi Jeneza.(Wiki moja na siku mbili views 181,921+)

6-Ommy Dimpoz- Cheche(wiki moja views 384,311+)

Source: Bongo5.com
 
Ommy dimpoz naye alichochea bifu lakini wimbo wake umeenda na Maji .. tena baada ya halelujah cheche haijaongezeka views kabisaaaa ....
 
Nimekuwa nikifuatilia nyimbo mpya za Bongofkeva bila kuangalia majina, kwa sababu kuna watu hawana majina wanatoa nyimbo nzuri sana hawasikiki.

Shukurani kwa kuleta hii makala.
 
Hiyo ni kweli. It is too much now.
Kiufupi ni kwamba soko limeshikwa na WCB na wapingaji/ wanabifu wa WCB

So either uwe Wcb au uwe aduivwa wcb. Hata kiba asingekuwa na uadui asingesikika
 
Umeongea ukweli mkuu
 
hahahaha mnasahau alikujaga Darasa akafanya vizuri katikati yao sema tatizo lake hakujipanga akaishia pale pale akija mtu atoe wimbo mzuri zaid ataliteka soko na ataingia kwenye ushindani tatizo la hao wengine unakuta mtu anatia chembe chembe zakushabikia upande fulani wa kiba au diamond hapo na yeye anajifukia humo humo....
 
Acha maneno weka muziki
 
Hii post ni ukweli mtupu. Ukitaka kuthibitisha hilo angalia baadhi ya michango hapo juu badala ya kujadili soko la mziki, watu wanaleta u wcb.
 
Mwanaume pampu. Nasikia kuanzia leo asubuhi bei ya pampu za baiskeli zimepanda bei ghafla.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…