Vita ya Ukraine, Hamas na Gaza, vimewaondoa Democrats madarakani

Vita ya Ukraine, Hamas na Gaza, vimewaondoa Democrats madarakani

Huyu anaenda kushughulika na mzizi, ataukata. IRAN, Iran, Iran umeandaliwa mitego mitatu

1. Kujaribu kumuua rais mteule wakati wa kampeni. Utajibu.
2. Kuifurumishia maroketi ya kivita Israel
3. Kufadhili na kujificha nyuma ya vikundi vya wapiganaji kuishambulia Israel. Mpaka mwaka 2025 uishe utawala wa Ayatoallah hautakuwepo Iran.
Lakini hata Trump hawezi kuwasulubu Iran, sana sana ataishia kutishia na kuwatukana,
 
Huo ndio ukweli mkuu vita ya Ukraine na gaza imeigharimu Demokratic
Hisia siyo lazima iwe uhalisia.

Kwa Marekani imekuwa jambo la kawaida vyama kupokezana madaraka.

Republican, chini ya Trump, walivyoshindwa uchaguzi, kulikuwa na vita ya Ukraine au Gaza?

Tena huko Gaza, Trump ana msimamo mkali zaidi. Alikwishawahi kusema kuwa kwa kile walichofanyiwa Israel na Hamas mwakajana, yeye angekuwa Rais wa Israel angefanya zaidi ya alivyofanya Netanyahu, ila aliwalaumu Israel kwa kuonesha picha. Akasema Israel ilitakiwa kuwaangamiza Hamas bila ya kuonesha maangamizi wanayoyafanya.

Huko Ukraine alisema kuwa yeye akiwa Rais ataimailiza hiyo vita mara moja, alipoulizwa ni kwa namna gani, alisema hawezi kufafanua zaidi, ila atawapa Russia chaguo, wakikataa, msaada wa USA kwa Ukraine hautakuwa wa kugusagusa, bali utakuwa ni msaada kamili wa ushindi.

Sasa tusubiri tuone huo mpango wake ni upi. Ufahamu kuwa Trump, ni miongoni wa wale watu wenye misimamo mikali, akifanya uamuzi wake, hajaribishi bali ni full force.
 
Lakini hata Trump hawezi kuwasulubu Iran, sana sana ataishia kutishia na kuwatukana,
Kwa ufupi, utawala wa akina Ayatollah hautakiwi. Zaidi ya Iran nani analeta kero kwa mtoto pendwa wa USA na Ulaya Magharibi.

Iran hamalizi miaka minne Trump bila kiangukia pua.

Iran angependa sana Kamala ashinde. Ila sio mapenzi ya Allah, lazima aende ili mashoga yavuke mto frat kwenda mashariki😂🤣. Ni suala la kutimiza unabii
 
Pia upigaji ulizidi kiwango na sera za kuidhoofisha kiuchumi China ambao magari yao ya umeme yakawekewa ushuru mkubwa kuwakomoa.

Tusishahu tishio la BRICS na ngojea kuona raisi mtarajiwa Trump atalikabili vili suala la BRICS maana Uturuki nao keshajiunga.
Falsafa kuu ya Trump ni “America First” na hasimu wake mkuu ni China (kiuchumi na kijeshi).

Tunasubiri tu jina atakaloibatiza hiyo BRICKS, kama kawaida yake.
 
Huyu anaenda kushughulika na mzizi, ataukata. IRAN, Iran, Iran umeandaliwa mitego mitatu

1. Kujaribu kumuua rais mteule wakati wa kampeni. Utajibu.
2. Kuifurumishia maroketi ya kivita Israel
3. Kufadhili na kujificha nyuma ya vikundi vya wapiganaji kuishambulia Israel. Mpaka mwaka 2025 uishe utawala wa Ayatoallah hautakuwepo Iran.
Alijaribu kufanya hivyo alivyokua rais kuanzia 2016-2020 ila akaangukia pua.
Unadhani Iran ni nchi nyepesi!??
Tupo hapa.
 
Back
Top Bottom