Vitambulisho vya Taifa: Maoni ya Mchungaji

1. KWANINI WABARA HAWATAKIWI KUMILIKI ARDHI ZANZIBAR? wakati wazanzibar
wanamiliki ardhi Bara? [/QUOTE


KAMA UNASHIDA NA ARDHI NENDA MOROGORO KUNA MISITU NA ARDHI YA KUTOSHA! WACHA KULILIA KAARDHI KADOGO KA WAZENJI AMBAO HATA WAO WENYEWE HAIWATOSHI! NAHAKIKA WEWE NI MCHAGGA NA KAWAIDA YENU WACHAGGA HUWA MNATATIZO LA ARDHI NA UGOMVI WA VIHAMBA LAKINI ALIEKUWA RAIS WA AWAMU YA PILI MZEE RUKSA ALIPOKUJA KILIMANJARO MIAKA YA 90 ALIWAOMBA WOTE WENYE SHIDA NA ARDHI BASI WAHAMIE MOROGORO NA BAADHI WALIHAMIA HUKO NA SASA MAMBO YAO MAZURI.

ILA UNAPOLILIA KUPEWA ARDHI ZANZIBAR UNANITIA SHAKA KIDOGO NA KUANZA KUJIULIZA HUYU MCHAGGA ANATAKA ARDHI ZANZIBAR ILI AKAFANYE NINI HUKO? NA JIBU LA HARAKAHARAKA NI KUWA LABDA UNATAKA UPEWE ARDHI HALAFU UJENGE BAR NA DANGURO KWA KUUZA MBEGE NA BIA NA KWA MILA ZA WAZENJI HAYO NI HARAMU SASA MIMI NAKUSHAURI UENDE MIKOA MINGINE YA BARA NA HUKO KUNA POSIBILITIES NYINGI TU ACHANA NA ZENJI NDUGU YANGU BAA LAKO LITALIPULIWA BURE NA UPATE HASARA!!
 
ni kweli kabisa maana Wabara kule zenji wanaitwa ni makafiri..duh eti tuko nchi moja, yaani sioni hata huo umhimu wa huo muungano kabisa...
 
Hapa hakuna cha serikali tatu wala mbili kila mmoja ashike hamsini zake na nchi yake, wazanzibari wale halua na tende na TZ bara waendelee na bata kivyao.

Mmmmh lakini Tz bara jina mshachakachua from Tanganyika sijui mtaliitaje maana ukiweka Tanzania zenji ipo
 
Serikali tatu za nini si ndio itakuwa bado ni yale yale mambo ya longolongo!!
Bora kila taifa libaki na utaifa wake kama ilivyokuwa kabla ya kuungana!!!
Wazanzibar wanazidi kuleta stori kuzingua na kujionesha kwa mtzbara kuwa wao ndio waswahili halisi wazanzibaris na nchi yao!!! Wanaongelea sana kuwa wageni wengi wasiowafahamu wamevamia katika nchi yao na wageni wengine sio hata watanganyika wameamua kuilaumu serikali ya tzbara...sasa ndio vile wanaona muungano hauna faida yeyote na taifa lao isipokuwa unazidisha matatizo mengi kwao kama vile ujambazi na kudumiza uchumi wao usiende mbele na kuuharibia utamaduni wao!!!!
 

ha haha ha haaaaaaa

umeniacha hoi kabisa ila mimi simo sijui hakika haya unayosema
 

jibu dogo tu ni kuwa zenj ni kijimkoa cha bara kilichojitangazia dola. Tukiwaacha wajitawale tutashuhudia infux ya mamluki ambao wengi wao ni waarabu. Wataisonga sana bara na eac. Zenj ni toto tundu tu so waache wajigalagaze watakavyo maadam hawana madhara
 

Kwa hiyo namba moja fuatilia kanda za Saa ya Ukombozi za Rev. Mtikila amelielezea vizuri sana . i.e. Kuna kiongozi aliwaambia wazenji njoni huku kuna ardhi wasaa ..
 
Tusipigizane kelele bure, vile vitambulisho vinaitwa "Kitambulisho cha Mzanzibari Mkaazi", vikiwa na maana kuwa vinawahusu wale wanaokaa Zanzibar, si lazima hata kuwa mzaliwa wa Zanzibar.

Ile ilikuwa dili yenye faida mbili kwa CCM Zanzibar. Kwanza, kama mradi wa mabilioni ya fedha, wapo waliofaidika na wanaoendelea kufaidika pale. Msisahau kasheshe alilozua Masha wakati wa dili la vitambulisho Tanzania Bara.

Pili, ilikuwa janja ya CCM Zanzibar ya kuchakachulia kura. Vile vitambulisho wanavyo hata Wana Msumbuji wengi ambao hata hawakai ZNZ, huja pale kupiga kura halafu wanarejea kwao. Watanzania Visiwani hutumia vitambulisho vile mara moja tu kila baada ya miaka 5.

Jengine muhimu la kuzingatia ni kuwa katika kitambulisho chochote kila kunakuwa na maelezo binafsi na kumbukumbu za mhusika, ikiwemo JINA KAMILI, TAREHE NA MAHALI PA KUZALIWA. Hili linaonekana hata katika paspoti za Watanzania, kwa mfano. Kwa hiyo hata kama Watanzania Visiwani watapewa vitambulisho vya Tanzania, kumbukumbu zitaonesha anatoka wapi.
 

tatizo la watanganyika ni kuukataa "utanganyika" na hii ni laana ambayo haitatupa raha milele... Kwanza tukubali kama sisi ni watanganyika , baadae ndio tuwalaumu wazanzibari... Utanzania ni sawa na "fake identity".
 
Hute na wanaJF,

Tunapoleta mada ,tujikite kwenye mada hiyo, vyenginevyo inakuwa ni kupigishana kelele na kutoka nje ya mada,pia nje ya mjadala. Mada imeanza kama "Wanzanzibar na vitambulisho vya Utz au Uzenj!

Halafu kwenye maelezo umesheheneza(shehena) umebambikiza haya;

1. KWANINI WABARA HAWATAKIWI KUMILIKI ARDHI ZANZIBAR? wakati wazanzibar
wanamiliki ardhi Bara? haya matatizo ya muungano hadi lini?
2. Kwanini kusiwe na vitambulisho vya uTanganyika, Uzanzibar na Utanzania?

3. Wabara waruhusiwe kumiliki ardhi zanzibar kama wanzanzibari wanavyomiliki hapa

4. Kuna Umuhimu wa kuanzisha selikali tatu awamu hii?


Jee nia hapa ni kujadili mada kama "great thinkers" au nia ni kuamsha hamasa na hasama?
Kupandikiza chuki?

Au, simply ,tunataka kutengeneza mandhari ya soko la Kariakoo,shimoni, au twaswira ya kwenye minada ya soko la samaki? Na hivyo kuumizana na kuumishana vichwa na kuichafua JF?


Ukweli unabaki, vitambulisho vina maana gani? Kwa nini tunahitaji vitambulisho?
Nini madhumuni ya vitambulisho hivyo?


Kazi ya kitambulisho ni kutoa utambulisho. Tanzania tuna utaifa unaoitwa Utanzania. Kama lengo ni kumtambulisha kila raia wa Tanzania basi kila raia, na ujumla wake kila mwenye sifa ya kupewa, apewe kitambulisho hicho bila kujali anaishi sehemu ipi ya Tanzania.


Kule Zanzibar wametoa vitambulisho vya mzanzibari kukidhi matakwa ya ushiriki katika chaguzi za Zanzibar. Ninavyofahamu mimi ni hivyo. Sio kila mtanzania anasifa ya kushiriki chaguzi za ZEC,kuchagua rais wa zanzibar au Wawakili ambao wataingia baraza la wawakilishi kule Zanzibar.
Kuna watu wenye asili ya Tanzania bara (Tanganyika) baada ya kuwa wakaazi huko Zanzibar na kupata sifa ya kupewa kitambulisho cha mzanzibari basi amepatiwa kitambulisho hicho. Vyengenevyo huwa anashiriki katika Chaguzi za NEC tu.


Kwa muundo wa Muungano uliopo leo kila mzanzibari mwenye sifa ya kupiga kura ana haki ya kushiriki chaguzi za Jamhuri ya Muungano. Kungekuwa na chaguzi zinazoihusu Tanganyika pekee basi wanzanzibari wangekosa sifa ya kushiriki chaguzi hizo. Wale tu ambao wangekuwa na vitambulisho vya utanganyika ndio wangefanya hivyo.
Matatizo yapo kwenye Muundo wa Muungano wetu na mapungufu katika sheria za uchaguzi.


Niishie hapa katika mchango wangu kuhusu vitambulisho. Kama una nia njema ya mijadala, basi lete hizo mada nyengine katika threads nyengine tujadiliane kistaarabu, bila ya chuki , kukoroga hisia za watu, na kuwapandisha mizuka.


Kwani mtu anapojadili mada kwa hasira, ushabiki au hamasa, kuna uwezekano mkubwa ku-block his/her reasoning power! Badala yake akawa anatapika pumba tu.


Hoja ziwe msingi wa majadiliano yetu. Nguvu za hoja zichukue nafasi yake.

Ukileta hilo la ardhi kwenye new thread nitapenda kutowa mawazo yangu huko.
 
Tunataka vitambulisho vya Utanzania mara moja, lakini wazanzibari wapewe vitambulisho hivyo vikiwa na note kuwa, huyu ni Mtanzania lakini pia ni Mzanzibari.

Na kwa ajili ya Wabara kuwa na note kuwa, huyu ni Mtanzania lakini pia ni Mtanzania Bara!
 
namuunga mkono mchungaji Mtikila yeye haitambui tanzania, anaitambua Tanganyika
 
bado una ulazima? kwasababu wenzetu wanatukataa sisi tunaulazimisha kwa nguvu.

tatizo tuna ukataa "UTANGANYIKA" ndio wazenji hawatuelewi... wao wanatujua kama sısı watanganyika lakini sisi hatutaki ukweli uliyo wazi....
 

hakuna mipaka kati ya tanzania na zanzibar...kuna mipaka kati ya tanganyika na zanzibar
 

kabla ya kupiga kelele juu ya uwezekano wa kupatikana mafuta zanzibar . Wewe kama mtanganyika hizo mali ambazo zinapatikana hapa tanganyika wewe umefaidika nazo kitu gani ? Dhahabu, tanzanite,almasi na mawe mengine...
Au upo hapa kuengeza wingi tuu?
 

hıvyo huta wafanyia haki wanzanzibar... KWANINI UONE AIBU KUITWA MTANGANYIKA? KWANINI HII NI NGUMU SANA KUKUBALI KAMA MTU WA BARA NI MTANGANYIKA? kwahiyo kitambulisho kiandikwe KAMA HUYU NI MTANZANIA LAKINI VILE VILE NI MTANGANYIKA...NA HUYU NI MTANZANIA LAKINI VILE VILE NI MZANZIBARI, hapa kuna makosa?
 
'Kwangu mimi, uhuru unamaanisha kusafiri'--airtel. Hivi kwa Tanzania uhuru wa watu unamaanisha nini? Au labda niulize wanajamvi misingi ya taifa kama Tanzania ni ipi? Majuzi tulisikia kuwa vitambulisho vitasaidia katika maendeleo ya Tanzania. Uhuru wa Manamba! Kwangu mimi haya ni maajabu kabisa; nyumba imara huwa inajengwa kwenye msingi, sasa kama ajira milioni hazikuongeza makusanyo ya kodi vitambulisho vitayaongezaje?
 


Kwa bongo uhuru unamaanisha kutembea kifua wazi usiku kucha, kunywa bia mpaka asubuhi. Hakuna maana nyingine inayoweza kuleta tafsiri sahihi.
 
Kwa Tanzania uhuru ni Chukua Chako Mapema; bahari inaendelea kufaidia maji ya vijito....
 
Nilichokiwa namaanisha,ni kuhusu kitendo cha Serikali kutambua ongezeko la ajira zaidi ya milioni, bila kodi kuongezeka na hata Ndugu Rais alipoisifia TRA, ilikuwa kwa ufanisi wa kiutendaji na Wizara ya fedha haikutoa bajeti tofauti(utegemezi wa Wafadhili bado ni uleule-tofauti kidogo sana) kwa maneno mengine ongezeko la ajira halikuzaa matunda hazina!
Kimsingi mambo haya(ID na ajira) ni tofauti--Vitambulisho vinagusa uhuru wa mtu moja kwa moja hata kama vitambulisho vingelikuwa ni vya hiari ya mtu. Tanzania na Afrika kwa ujumla Uhuru ni miongoni mwa misingi yetu, misingi ina miiko yake na miiko hii hubeba ukweli,tukitaka kujinasua lazima tuheshimu ukweli wetu; ukweli wetu siyo sawa na ukweli wa utamaduni wa sehemu nyingine--tunaweza kukopa na kuhemea kujikimu, kuendelea kuna maanisha kufuata misingi na zaidi ya yote kufuata ukweli na hali halisi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…