Vitendo SACCOS - kukopeshana bila riba



Kuna tofauti kubwa sana. Kwenye mikopo ya Islamic banking, utalipa gawio la faida pale tu biashara inapopata faida. Kukiwa kuna hasara basi hulipi kitu. Kwenye mikopo ya kawaida, utalipa riba hata kama biashara imepata hasara.
 

Dhamana inawekwa kwenye mikopo ya Kiislam.


Hizi ni aina kuu za huduma za mitaji kwa kutumia mfumo wa kiislam:


Mudarabah ni mkataba wa ushirikiano wa biashara (Pertnership) ambapo mmoja anatoa pesa ya mtaji wa biashara kwa asilimia 100 na mwingine anawekeza mda na ujuzi wake katika kuendesha na kusimamia biashara kisha wawili hawa wanagawana faida na hasara itakayopatikana kwenye biashara hiyo kwa asilimia walizokubaliana kwenye mkataba. Mara nyingi inakuwa ni 50:50 au 60:40.


Murabahah ni makubaliano kati ya mtoa pesa na mpokeaji ambapo mtoa pesa ananunua kitu na kisha anaongeza faida yake na gharama zingine zinazoendana na kukipeleka na kukitunza kitu kilichonunuliwa kwa mpokeaji. Mtoa pesa hawezi kudai zaidi ya malipo yaliyopo kwenye makubaliano hata kama mpokeaji anachelewa kufanya malipo kama makubaliano yanavyohitaji. Kitu hicho kinakuwa ni dhamana ya mkopo husika mpaka pale ambapo mtoa pesa amelipwa hela yake yote kama makubaliano yanavyotaka.


Musharakah ni mkataba wa watu wawili au zaidi kuchanga mtaji kwa ajili ya kuwekeza kwenye biashara kisha kugawana faida ya mradi kutegemea na mchango wa kila mtu kwenye mradi husika.
 
Je hakuna namna ya kuonana ana kwa ana kwajili ya kupeana elimu zaidi juu ya mfumo huu pamoja na malengo na mikakati yake pasipo kusibiri mpaka kikao kitangazwe?
Mimi ni mkazi wa kibaha na ningependa kuonana na wewe tupeane elimu zaid.


Karibu sana wakati wowote, kwetu ni Misugusugu shule ya msingi, mtaa wa vitendo.

Asante.

Abdul
0625249605
 
Wadau wote,

Wote watakaojiandikisha uanachama wa saccos yetu mpya kabla ya kusajiliwa rasmi watajulikana na kutambulika katika chama kama "waanzilishi" na records zote za chama zitaonesha hivyo.

Nawapa hongera mliokwisha jiunga kwa sasa hadi hapo tutakapopata usajili rasmi kwani nyote ni waanzilishi.
 
Wadau wote,

Ninafuraha kubwa kuwajulisha kuwa jana tumeandikisha mwanachama mpya wa SACCOS yetu mpya. Ingawa tumeshaandikisha wanachama wengi wapya kabla yake lakini huyu imebidi niiweke bayana furaha yangu kwa kujiunga kwake nasi.

Si mwingine bali ni Bi Thureya Mohamed Sheikh wa Vitendo, Misugusugu. Bi Thureya ni mwanamama mmoja shupavu sana, aliyejitolea maisha yake yote ya ujana kuwakomboa watoto na vijana wasio na bahati.

Hapa kwetu Misugusugu Bi Thureya ni maarufu sana kwa ujasiri wake, moja katika sifa zake ni anapokuta mtoto hana malezi mazuri basi hufanya kila jitihada kuwajua wazazi wake na kuanza kuwaelekeza kuwasomesha na ikishindakana wazazi kubadilika basi huwachukua hao watoto na kuwalea yeye kwenye kituo chake.

Mpaka sasa Bi Thureya ameweza kuwasomesha watoto wengi sana kwenye shule za malipo ambazo kwa wengine huwa ni ndoto tu, ameweza ku lob, kupigana na hatimae kupatiwa nafasi za masomo kwa watoto wasio na bahati.

Hivi karibuni ameweza kupigania mpaka ameweza kujengesha shule ya chekechea na msingi usoni mwa nyumba yake.

Kituo cha Bi Thureya ni tofauti na vituo vingine vyote nilivyowahi kuviona vya kulelea yatima na watoto wasio na bahati, ukifika kituo chake utakuta yeye mwenyewe anaishi nao hao watoto hapo hapo akihakikisha wanapata "close nurturing" kama wanawe mwenyewe ambao nao wanaishi wote hapo hapo. Shule wanazosoma wanawe ndizo shule hizo hizo wanaenda watoto na vijana anaowalea hapo.

Bi Thureya ni mchapa kazi, mwanaharakati na mama mwenye huruma kubwa na mwenye uchungu sana na maendeleo ya jamii.

Binafsi humuita Bi Thureya "commando" maana ayafanyayo ni ukomando kweli kweli na si rahisi kwa mtu asiye na moyo wa kikomando kama Bi Thureya.

Kuna mengi sana mema ya kuuelezea wasifu wa Bi Thureya lakini ipo siku tutaandika wasifu wake kwa kina, kwa leo niishie hapo kwa kuiweka furaha yangu bayana kwa uwepo wake kwenye sacos yetu mpya.

Hakika ni mwanamke shupavu.

Tuna furaha kubwa kuwa nae katika saccos yetu mpya, tuna mengi sana ya kufaidika nayo kutoka kwake.
 
Napenda kuwajulisha wadau wote kuwa Vitendo SACCOS (SACCOS Bila Riba) ipo njiani kusajiliwa.

Wahi kujiandikisha uwe kati ya wanachama waanzilishi.
 
Will join you soon...I hope sijachelewa


Haujachelewa na ukijiandikisha mapema, kabla hutajasajiliwa rasmi unakuwa ni "mwanachama mwanzilishi".

Kujiunga nasi kwa sasa ni TZS. 10,000 tu. Unatuma kwa Mpesa 0756803528, na unatutumia majina yako matatu kwa whatsapp 0625249605, ili tukusajili.

Karibu sana.
 
HISA zinauzwa kwa bei gani?, zitahitajika ngapi ili mtu aweze kukopeshwa?

Napenda kukufahamisha ndio kwanza tuna andaa masharti ya ushirika wetu, ukijiunga sasa (kabla ya usajili rasmi kisheria) utakuwa mmojawapo wa "wanachama waanzilishi", kwa maana hiyo, utakuwa na fursa ya kutoa mawazo na kufanya maamuzi ya mambo kama hayo ya hisa.

Kwa sasa tunajadili aidha tuwe na hisa za kuanzia million moja na kila hisa iuzwe kwa elfu moja au tuwe na hisa million mbili na kila hisa iuzwe kwa mia tano. Target ni ku raise TZS Billion moja.

Licha ya hisa, pia tutakuwa na akiba Ukiwa na akiba utakopeshwa paka mara mbili au tatu ya akiba yako (haijaamuliwa kwa sasa).

Ukiwa na hisa kuna uwezekano mkubwa ukaendesha baadhi ya miradi ya saccos kama mmiliki chini ya usimamizi wa wanahisa wengine.

Karibu sana.
 
Daah mpango huu nimzuri hata mm nipo mbioni kujiunganao

Kujiunga nasi kwa sasa ni TZS. 10,000 tu. Unatuma kwa Mpesa 0756803528, na unatutumia majina yako matatu kwa whatsapp 0625249605, ili tukusajili.

Karibu sana.
 
bi zainab asalam aleyqum..swali langu je sisi tunaoishi zanzibar tunaweza kujiunga na hiyo saccos ?asante
 
nataka kujiunga ili nahitaji maelezo kidogo natuma hiyo elfu kumi zeni maelezo mengine vipi
 
bi zainab asalam aleyqum..swali langu je sisi tunaoishi zanzibar tunaweza kujiunga na hiyo saccos ?asante


Kabisa tena. Unaweza kujiunga nasi popote ulipo.

Hivi sasa tayari tuna wanachama Watanzania wanaoishi nje ya Tanzania (diaspora) wamejiunga.

Karibu sana.
 
nataka kujiunga ili nahitaji maelezo kidogo natuma hiyo elfu kumi zeni maelezo mengine vipi

Maelezo yote kiukamilifu utapatiwa kadiri ya yaliokuwepo.

Kwa ufupi, ni saccos mpya na ya kipekee jinsi itakavyoendeshwa.

Kujiunga ni 10,000 halafu kutakuwa kuna hisa ambazo zitatangazwa kwa wanachama wote mara tu baada ya kusajiliwa rasmi. Utanunua hisa kadiri ya uwezo wako. Kutakuwa pia kuna uwezekano wa kuweka akiba yako. Kutakuwa na miradi ya maendeleo itayolenga kuendeleza wanachama kimaendeleo na jamii kwa ujumla. Kutakuwa pia na mikopo kwa walioweka akiba isiyokuwa na riba.

Toka tulipoitisha mkutano wa kwanza kwa kutoa nia ya kuanzisha saccos hii, tumeweza ku attract wanachama wa kila kada, tumeweza kunzisha "pilot test projects" kwa dhamira ya kuendeleza wanachama.

Tupo njiani kumalizia "draft" ya masharti ya ushirika wetu ili tuigawe kwa wanachama waanzilishi waipitie na kuijadili na kuirekebisha inapobidi ili tujiandikishe rasmi.

Kama kuna chochote utakacho kufahamishwwa zaidi tafadhali usisite kuuliza.

Karibu sana.

Abdul
0625249605
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…