Vitendo vya baadhi ya matrafiki vinatia doa Jeshi la Polisi

Vitendo vya baadhi ya matrafiki vinatia doa Jeshi la Polisi

Nsimbinso

JF-Expert Member
Joined
Dec 15, 2020
Posts
407
Reaction score
431
Habari wadau.

Imekuwa kawaida kusimamishwa na Askari wa barabarani kwa ajili ya ukaguzi. Huu ni moja kati ya wajibu wao wa msingi kwa ajili ya kuhakikisha usalama wetu watumia vyombo vya usafiri pamoja na wote wanaotumia barabara au wenye shughuli zao pembezoni mwa barabara.

Baadhi ya askari wanatekeleza wajibu huu kwa weledi mkubwa, kiasi kwamba wanapokagua gari lako unaona fahari. Kuna baadhi yao mimi huwa siwaelewi kabisa.

Tucheki kwa pamoja baadhi ya matukio niliyokutana nayo ambayo binafsi nakosa jina la kuyapa.

1. Nishawahi kukaguliwa na askari, kaomba fire extinguisher nikampatia, akaikagua ikawa poa. Akaomba reflector triangle nikampatia. Akaniambia niwashe taa za parking, zikawaka. Akaniambia nikanyage break akague taa za break. Sikuwa mbishi, nikakanyaga. Akanifuata na machine yake ya kukagulia gari akaniambia taa za break haziwaki. Akaanza kuandika fine. Nikamwomba asubirie.

Nikamwomba abiria aje akanyage pedal ya break nikazunguka kukagua mwenyewe. Cha ajabu nikakuta taa zinawaka. Nikamuita askari, eti akaanza kushangaa na kujiapia kuwa hazikuwa zinawaka. Nikasepa bila kuandikiwa fine.

2. Tukio lingine ambapo niliandikiwa fine nilikuwa nyuma ya semi trailer. Barabara ilizuia ku-over take. Ni sahihi kabisa.

Palikuwa na mpando ambao haukuzuia dereva wa nyuma kuona mbele. Nilitembea nyuma ya hii semi trailer kwa kilometer kadhaa. Hofu ikawa ni mwendo na uimara wa gari lililokuwa mbele yangu kwani niliona lilivokuwa linapanda kile kilima kwa tabu. Nikalipita...

Bahati mbaya askari huyo. Swali likawa kwanini nime-over take mahali pale. Nilimjibu kuwa tumezuiwa ku-over take pale sababu ya usalama... Ila usalama ni uko wapi, kukaa nyuma ya ile semi ambayo mwendo na aina ya mzigo iliyobeba vinaonekana ku-fail na kunikandamiza hapo nyuma muda wowote.

Busara ni kubaki hapo au kusaka usalama zaidi hata kama ni kwa kukiuka baadhi ya sheria za barabarani ambazo hazina madhara kwa mazingira husika, akaniambia nisimfundishe kazi, akanilima fine.

3. Tukio jingine ambalo mpaka muda huu naliwaza; mwezi uliopita nilipata ajali, Gari yangu iliharibika, waliofika eneo la tukio wakafuata process za kipolisi, wa gari garage. Kwa vile uchumi si rafiki kipindi hiki nikaomba gari ikae garage mpaka nitapojikusanya na nitapotoka hospitali. Kulikuwa na penalty ambayo baada ya ajali nilikaa hospitali siku kadhaa hivyo muda ukapita ikawa imeongezeka. Cha ajabu traffic police wakawa wanapita kwenye ma-garage kukagua madeni. Wakakuta gari langu limebondeka halifai na lina penalty ipo pending.

Chap wale askari wakanipigia nikawaeleza ndo nimetoka hospitali na sipo vizuri kiuchumi, ndio maana gari bado haijaanza kurekebishwa. Yule askari aligoma kuelewa, akaita breakdown wakabeba gari kutoka garage kwenda polisi huku akisema Serikali inataka mapato na nitafute pesa ya kulipia fine na pesa ya breakdown. Hao wakaburuza gari tena wakisababisha damages mpya ambazo zitanicost pesa zaidi wakati wa kutengeneza gari.

Haya ni baadhi ya matukio ambayo yamenifanya niwatafakari baadhi ya hawa watanzania wenzetu waliopewa dhamana ya kusimamia usalama wetu barabarani na kuniacha na maswali kadhaa.
 
Hawa jamaa ni wasumbudu sana. Binafsi siwapendi hata kidogo. Ni wachache sana kati yao ndiyo waungwana. Wengi wao ni wapuuzi na wenye uelewa mdogo.
 
lilivokuwa linapanda kile kilima kwa tabu. Nikalipita...
Ngoma ilikuwa kwenye low range half exelerator

Tanzania ndio yenye Trafiki kero na ni wengi kuliko Nchi yoyote ya Afrika Mashariki na kati

Mimi taa yangu( Brake light)ya Trela ilikuwa imeungua Rwanda trafiki akanikagua na kunipa Warning kuwa next time niwe natembea na Balbu ili niwe napachika
 
Lengo la sheria lilikuwa jema ila wao wanaitumia kujikusanyia pesa. Badala ya kuwa msaada inakuwa kero. Gari likiwa bovu, ukawapa pesa, wanaruhusu uendelee na safari. Gari zima usipowapa pesa, watatafuta sababu. Hawa watu taabu Sana.
 
Lengo la sheria lilikuwa jema ila wao wanaitumia kujikusanyia pesa. Badala ya kuwa msaada inakuwa kero. Gari likiwa bovu, ukawapa pesa, wanaruhusu uendelee na safari. Gari zima usipowapa pesa, watatafuta sababu. Hawa watu taabu Sana.
Ningetamani sana kuona hili jeshi la polisi na hasa hiki kitengo cha usalama barabarani kikifumuliwa chote! Maana kinanuka kwa rushwa!

Kuanzia kwenye tochi ni rushwa! Kwenye 50/kmph ni rushwa, makosa ya kuelekezana tu, wanataka rushwa! Ukikataa, unaandikiwa faini! Yaani wenye magari kwa sasa ni sawa tu na ng'ombe wa maziwa wa hawa viumbe walafi!
 
Baadhi ya traffic police wanatafuta makosa kwa juhudi kubwa sana hata kama huna. Imagine anakuja na kile kidubwasha cha kutolea receipt macho pima utadhani ni lazima uwe na makosa.

Ndio maana mimi huwaona kama majambazi wanaoiba mchana kweupe pee wakiwa wamevaa mavazi meupe na bila silaha.

Afadhali Mama aliwaambia kuwa wasifanye tena faini zikawa ni mojawapo ya chanzo cha mapato.


Kwa Tanzania nzima sehemu hatarishi kwa kukamatwa mara kwa mara ni mkoa wa Arusha.

Hata kama walikuwa wamepewa maagizo maalumu na Mwendazake ila utekelezaji wake ni wa kiuonevu sana.

Unaweza kuandikiwa makosa manne ila lengo hasa ni ili upigwe 20,000.

Kuna kiwango maalumu wanapangiwa kazini waingize ila na wao wana michezo yao ya kupeana pesa kila siku (kibati) na lazima ufikishe lengo la kazini na la kikundi.

Wanaoumia ni sisi.
 
kila siku huwa nawaambia ukiona kila siku sehemu hiyo hiyo wanakusumbua wee pia una silaha wanyanganye tuu silaha zao!!afu unatembea zako upotee kabisa nchi hii maana wakikudaka pepsi utaita fefshi
 
Hawa jamaa ni wasumbudu sana. Binafsi siwapendi hata kidogo. Ni wachache sana kati yao ndiyo waungwana. Wengi wao ni wapuuzi na wenye uelewa mdogo.
Wengi wao "hujitahidi kujenga uadui na wenye magari au kutengeneza mianya ya rushwa kama sio kukomoana!" Kile kifungu cha "kuonya" hakipo bali kutoa adhabu (faini) tu. Na kibaya zaidi wengi wao wanamiliki magari mabovu!!!
 
Ngoma ilikuwa kwenye low range half exelerator

Tanzania ndio yenye Trafiki kero na ni wengi kuliko Nchi yoyote ya Afrika Mashariki na kati

Mimi taa yangu( Brake light)ya Trela ilikuwa imeungua Rwanda trafiki akanikagua na kunipa Warning kuwa next time niwe natembea na Balbu ili niwe napachika
Magufuli aliwapenda sana askari wa barabarani. Nakumbuka aliwaalika kunywa nao chai ikulu wakati wa msiba wa ajali ya M.V Ukara.

Bila shaka alikuwa anawaambka "nawategemeeni katka kukusanya mapato huko barabarani" na tangu hapa ikawa ni mwendo wa kutangaza makusanyo ya mabilioni ya shilingi kutokana na fine kwa makosa ya usalama barabarani kila mwezi.

Hatari sana.
 
Back
Top Bottom