Bilionea wa India Ratan Tata ambaye amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 86 aliwahi kufichua kuwa alijaribu kupenda zaidi ya Wanawake wanne ambao alikaribia kuwaoa, lakini hakufanikiwa kwa kile alichodai kuwa ni kazi kuchukua sehemu kubwa ya muda wake pamoja na kufurahia uhuru wa kutokuwa na wasiwasi kuhusu hisia za mtu mwingine au mahangaiko ya mtu mwingine.
Tajiri huyo aliwahi kuhojiwa na CNN ambapo aliulizwa kwa nini hakuwahi kuoa na kufichua kuwa, “Msururu mzima wa mambo ulinizuia kuoa, muda, kazi kuchukua sehemu kubwa ya muda wangu kwa wakati huo. Nilikaribia kuoa wakati fulani, lakini haikuwezekana.”
“Kuna nyakati nyingi ambazo nilijihisi mpweke kwa sababu ya kutokuwa na mke au familia ingawa wakati fulani nilifurahia uhuru wa kutokuwa na wasiwasi kuhusu hisia za mtu mwingine au mahangaiko ya mtu mwingine” — alisema Tata alikiri kuwa kuwa kuna nyakati alikuwa mpweke kwa kukosa mke na familia.
Tata aliaga dunia siku ya Jumatano usiku baada ya kusumbuliwa ugonjwa wa muda mrefu. Alilazwa katika hospitali ya breach candy. Atapewa mazishi ya serikali na serikali ya Maharashtra.
Waziri Mkuu wa India Narendra Modi na pamoja na watu wengine mashuhuri kama Salman Khan, Ajay Devgn waliomboleza kifo cha Bilionea huyo.