Vituko: Taja tukio /kituko ulichofanya ukiwa mdogo ambacho ukikumbuka sasa unajiona mjinga

Wewe nawe mama akaamua akuache akili ikae sawa.. 😂😂
 
😂🤣🤣🤣 Mbavu zangu leo zinachomoka. !!
 
[emoji23]🤣🤣🤣 Mbavu zangu leo zinachomoka. !!
Utoto huu, acha tu mkuu kuna siku pia mama kaenda sokoni katuacha home na Mdogo angu ,ilinyesha bonge la mvua na radi za kuogopesha yaani, nikafunga mlango nikaanza kulia "Mdogo angu leo tunakufaaa mamaa weee" ikabidi Dogo ndye anibembeleze sister ake kwamba tutulie tu radi zitaisha[emoji3] [emoji3].huwa ananicheka hadi Leo eti nilikua kajinga jinga
 
Daah huyo mama atakuwa aliona aibu sana
 
Ha ha ha nimependa uoga wako😜😉
 
Nakumbuka wakati niko na miaka 10 hivi mama yangu wa kambo akanipa nguo za Mzee nifue na box kubwa la sabuni ya unga .Nikatia sabuni kiasi nikaanza kufua, wakati operation inaendelea akaja kukagua huku analalamika nimeweka sabuni kidogo nguo hazita takata.

Nikajiongeza nikawea box lote aisee,kusuuza mpaka sabuni iishe nilitumia maji pipa zima na kipindi hicho maji ya shida nilikua nachota mbali hatari,, .Kichapo cha kumaliza sabuni pia kilinihusu .
 
Mambo ya utoto ndo kama hivo kichapo huwa chakufikia tu
 
Hahaaa, ulijikomoa aisee poleee ,umenikumbusha siku nimeoshea vyombo sabuni ya kuogea(Geisha) vyombo vinanukia hivyo kama vimetoka bafuni kuoga[emoji3] [emoji3] mother alikasirika huyoo akanidunda na nikaambiwa nikarudie kuviosha Kwa sabuni ya kawaida[emoji3]
 
Wewe ulikuwa noma kweli sabuni ya kuogea tena hahah! Ila utoto bhana raha sana.
 
Wewe ulikuwa noma kweli sabuni ya kuogea tena hahah! Ila utoto bhana raha sana.
Acha tuu, kuna matukio hadi najishangaa[emoji3] [emoji3]yaani nilikua na maamuzi ya faster nimalize kazi niliyopewa nikacheze, so sikuona sabuni ya kuoshea, nikapata wazo si zote ni sabuni bana nikabeba ya kuogea[emoji3] [emoji3]
 
Kwangu nitaendelea kuita kauoga ka ki financial services [emoji6][emoji6].. itakuwa vyema kama umeiprove maana utanitoa mbavu[emoji23][emoji23]
[emoji3] [emoji3] ,ningekupa Nyingine ila naogopa ntakuua mbavu zakoo
 
[emoji3][emoji1][emoji3][emoji13],utoto shida,.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…