therocky
Member
- Jul 30, 2015
- 13
- 8
Habari wana jamvi Kuna hili swala ambalo najua sio geni miongoni mwenu na pia nimelisikia kwa muda toka muda mrefu achilia mbali kulishuhudia.
Ni kuhusu mama mjamzito anapopata tu hiyo mimba basi anakuwa na tabia tofauti na alizokuwa nazo awali, mathalani kupenda chakula cha aina fulani au kuchukia kitu au vyakula fulani(ambavyo kabla alivipenda sana) na mambo mengine mengi.
Sasa concern yangu hapa ni kuwa mimi mke wangu wiki hii anatimiza miezi mitatu ya ujauzito wake(ni wa kwanza) lakini mpaka sasa simuoni kama kawa na tabia yoyote mpya na pia sioni kama kabadili sana vyakula alivyokuwa anakula zaidi tu ya kusema anajisikia uchovu wa hapa na pale na kulala sana na kichefuchefu kiasi.
Sasa kwa nini sioni hizo tabia au vituko hivyo? Au kuna miezi kadhaa akifikia ndio huwa hivyo? Naombeni msaada hapo, kwa ma-daktari au wenye uzoefu na haya mambo.
Asanteni.
Ni kuhusu mama mjamzito anapopata tu hiyo mimba basi anakuwa na tabia tofauti na alizokuwa nazo awali, mathalani kupenda chakula cha aina fulani au kuchukia kitu au vyakula fulani(ambavyo kabla alivipenda sana) na mambo mengine mengi.
Sasa concern yangu hapa ni kuwa mimi mke wangu wiki hii anatimiza miezi mitatu ya ujauzito wake(ni wa kwanza) lakini mpaka sasa simuoni kama kawa na tabia yoyote mpya na pia sioni kama kabadili sana vyakula alivyokuwa anakula zaidi tu ya kusema anajisikia uchovu wa hapa na pale na kulala sana na kichefuchefu kiasi.
Sasa kwa nini sioni hizo tabia au vituko hivyo? Au kuna miezi kadhaa akifikia ndio huwa hivyo? Naombeni msaada hapo, kwa ma-daktari au wenye uzoefu na haya mambo.
Asanteni.