Uandishi wa ovyo kweli nahisi utakuwa umeokolewa na mafuriko huko mto msimbazi akili bado haijatulia.
Mbeya hatuhangaiki na mambo ya milo ni common tunakula kila tunachotaka.Watoto wetu wanakula wanashiba hadi chupi zinahamia tako moja.Watoto wa mbeya hata chokolaa wanakula mlo kamili bila tunda hawezi kula ndizi,parachichi ,nanasi.
Tuna warembo wenye nguvu akina atuganile,ngukusekela wana makalio ya asili siyo ya sindano kama akina chausiku,mwanaidi wa huko kwenu.
Njoo mbeya uone wanawake walivyopendeza bila mkorogo.Jamani hii mbeya ndiyo israel ya afrika kijani mwaka mzima.Hatujui kiangazi.
Ukitaka joto unasogea kyela nusu saa umefika,ukitaka baridi kali unasogea uyole dakika kumi,ukitaka vuguvugu unasogea mbozi nusu saa.
Ukitaka kwenda marekani kwa Trump unaenda Tunduma saa moja boarder ya akili tanzania nzima afrika mashariki na kati hakunaga kama tunduma.
Ukiwa mbeya unakuwa tayari upo malawi,zambia na msumbiji hivyo ndiyo afrika ya Tanzania.
Msioijua mbeya njooni muone raha ya kuishi mbeya.
Kama uliko maisha yamekupiga na huna mtaji kula shida njoo mbeya mji wa maziwa na asali.
Karibu mbeya ufurahie uwepo wa dunia.Utaliii wa kutosha.Utauona mto utoao maji ya moto kila siku,utakutana na ziwa la ajabu ziwa gosi.Njoo uone daraja la Mungu.
Ukichoka tunakupeleka sumbawanga ukafurahie maisha na utalii wa maana .Utayaona maporomoko ya kalambo falls 300m falling down hadi maji yanageuka kuwa mvuke na yanapotakiwa kutua ni pakavu kabisa unaweza kukaa,maajabu hayo.
Jamani acheni kabisa huku ni raha tu utaona mazoezi ya usafiri wa anga uwapo mbeya au rukwa bila malipo yoyote.
Karibuni mbeya na swanga kwa maisha bora na ya amani.
Karibuni wote mje kujionea uhondo wa mbeya na rukwa.