Vitumbua hivi nashindwa kuvisahau

Vitumbua hivi nashindwa kuvisahau

The Boss

JF-Expert Member
Joined
Aug 18, 2009
Posts
49,282
Reaction score
117,244
Miaka kama sabna iliyopita nilikuwa kwenye mizunguko city center mara kufika mtaa wa Lumumba CRDB kuna mtaa wenye ofisi za TRA hapo kulikuwa na kimgahawa cha watu wenye asili ya kiarabu.

Nikaingia nikaagiza chai ya maziwa na vitumbua viwili na katlesi mbili dah... Vitumbua vyake kwanza kwa macho tu vilikuwa tofauti

Vilikuwa vikavu kabisa.....kwa kawaida vitumbua huwa na mafuta lakini vya kwake vilikuwa vikavu...nikaanza kula dah.. vilikuwa laaini na vitamu ajabu...

Nimetembea kuanzia Zanzibar hadi Tanga sijawahi kula vitumbua kama hivi...ikawa kila nikienda City center napitia hapo

Siku moja kwenda pale nikakuta vutumbua tofauti nikauliza hivi vitumbua mbona sio vile vya siku zote
wakaniambia yule mpishi wa mwanzo kaondoka...duh.. nikauliza namba yake ya simu ili nijue kahamia mgahawa gani hawakunipa...

Mpaka leo navikumbuka vitumbua vile....yaani.....
 
mmh wapenda kula eeh?kama hupendi mafuta mkate wa chila unakufaa pia maana hauna mafuta na taste yake haina tofauti sana na vitumbua.ukimpata mpishi mzuri huu mkate huwa laini kabisa
 
mmh wapenda kula eeh?kama hupendi mafuta mkate wa chila unakufaa pia maana hauna mafuta na taste yake haina tofauti sana na vitumbua.ukimpata mpishi mzuri huu mkate huwa laini kabisa

vitumbua vile vilikuwa tofauti sana..na ladha yake pia..
 
farkhina unaweza pika vitumbua vikavu lakini laini?
 
Last edited by a moderator:
Hivyo vitakua vitumbua vya mayai vya mama nuru shekhe wangu,viko soft sana
 
Mkuu nenda Iringa mjini pale barabara ya uhindini karibu na Bar ya sterio kuna mama moja pale anapika vitumbua vizuri mno
Bila shaka utavipenda
 
Mkuu nenda Iringa mjini pale barabara ya uhindini karibu na Bar ya sterio kuna mama moja pale anapika vitumbua vizuri mno
Bila shaka utavipenda

Pale habari nyingine aiseee ni vitamu sana
 
FaizaFoxy labda anapajua hapo

Hiyo mitaa ulivyoielekeza naijuwa, huo utakuwa mtaa wa Kipata lakini hicho kihoteli na hivyo vitumbuwa sivijui, si unajuwa mitaa hiyo siku nyingi sana sijaitembelea, toka wajenge maghorofa kule kuna zahma hapapitiki.
 
Back
Top Bottom