Vituo vya habari vyapigwa rungu na TCRA kwa kurusha maudhui katika muda ambao watoto hawapaswi kuangalia ama kusikiliza

Vituo vya habari vyapigwa rungu na TCRA kwa kurusha maudhui katika muda ambao watoto hawapaswi kuangalia ama kusikiliza

Lisu alisema wakitumaliza sisi wanakuja kwenu. Na hapa bado kama hatukwenda kujikomboa
 
3: Kituo cha #EastAfricaRedio kimekutwa na hatia ya kurusha maudhui yenye kukashifu utendaji wa Serikali katika uteuzi wa mdhibiti na mkaguzi mkuu wa hesabu za Serikali (CAG) na kupewa onyo kali pamoja na kutozwa faini ya Shilingi milioni 3.
Mkuu,tunakoelekea ni full kusifia,Nchi imekuwa ya ovyo sana,juz makonda kawazalilisha mdee na Bulaya na vyombo vingi vikarusha uzalilishaji huo,
 
MAMLAKA ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imevitoza faini ya Sh milioni 30 vyombo vya habari sita, kwa kukiuka kanuni na maadili ya utangazaji ikiwamo redio ya Clouds FM kuzungumzia supu ya pweza kuimarisha tendo la ndoa katika muda ambao wasikilizaji wanaweza kuwa watoto.

Mbali ya Clouds FM, vyombo vingine vilivyoadhibiwa ni East Africa Radio, na televisheni za Star, Sibuka, na Global Tv na Duma Tv.

Akisoma uamuzi huo jana jijini Dar es Salaam, Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Maudhui ya TCRA, Joseph Mapunda alisema vyombo hivyo vilikiuka kanuni za mawasiliano kwa nyakati tofauti.

Mapunda alisema redio ya Clouds FM kupitia kipindi chake cha Jahazi, walihamasisha vitendo vya ngono, kwa kutumia supu ya pweza katika kuimarisha tendo la ndoa kwa muda ambao wasikilizaji wanaweza kuwa watoto.

Alisema baada ya kusikiliza utetezi wao, wanatozwa faini ya Sh milioni saba na kupewa onyo kali baada ya kuwatia hatiani kwa kosa hilo.

Katika shauri lingine, kituo cha Duma TV kimetozwa faini ya Sh milioni saba na kufungiwa kuchapisha maudhui kwa muda wa mwezi mmoja ili wajipange na kuzifahamu kanuni na kuzingatia weledi na maadili ya utangazaji.

Mapunda alisema Duma ilikutwa na hatia ya kukiuka kanuni kwa kuchapisha na kutangaza maudhui yenye lugha isiyo na staha na iliyo na udhalilishaji wa kijinsia kwa wanaume na wanawake.

Alisema redio ya East Africa imetozwa faini ya Sh milioni tatu na kupewa onyo kali kwa kukiuka kanuni hiyo, kwa kurusha maudhui ya kukashifu utendaji wa serikali kupitia uteuzi wa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) na kutumia lugha ya kashfa dhidi ya utendaji wake.

Vilevile Global Tv imetozwa Sh milioni saba na kupewa onyo kali, baada ya kupatikana na hatia ya kuchapisha picha ya mnato na kutangaza maudhui yasiyokuwa na lugha ya staha na yenye kushabikia vitendo vya mahusiano ya kimapenzi ya jinsia moja.

Mapunda alisema maudhui hayo, yangeweza kuwaumiza na kuwakwaza waumini wa dhebebu la Anglikana na Watanzania kwa ujumla. Pia, alisema Sibuka Tv inatozwa faini ya Sh milioni tatu baada ya kupatikana na hatia ya kushabikia mauaji ya kutisha katika muda, ambao watoto wanaweza kuwa sehemu kubwa ya watazamaji.
Aisee wanakaba mpaka penalti.
 
3: Kituo cha #EastAfricaRedio kimekutwa na hatia ya kurusha maudhui yenye kukashifu utendaji wa Serikali katika uteuzi wa mdhibiti na mkaguzi mkuu wa hesabu za Serikali (CAG) na kupewa onyo kali pamoja na kutozwa faini ya Shilingi milioni 3.
Kuna tofauti kati ya neno kukashifu na kukosoa. Kilichofanywa hapa ni kukosoa ingawa kwa mazingira ya sasa kukosoa kunachukuliwa kama kukashifu ama uchochezi.
 
Gadna Jihabash wa Jahazi apunguze maneno ya matusi na masihara.
Otherwise ni mtangazaji nzuri Sana.

2020
 
Waondoe na tangazo la TIGO linalomwonyesha mwanaume zuzu aliyeacha sh.10,000.00 siku ya kukumbuka kufungwa kwa ndoa yao alafu anakuta mzigo wa 50,000.00, mwishoni kabisa mwa tangazo ni aibu tubu, waliondoe.
 
Safi sana TCRA komesha kabisa hizo vuvuzela za ccm
 
Vipi TBC 1 haipo?
Hiyo sidhani hata watoto wa chekechea huwa wanaangalia wakati wowote wakiwa nyumbani au popote. Watangazaji na wanaotangazwa wote hawana mvuto kwa wasio wanachama wa CCM wakiwemo watoto.

TBC ilikuwa ya wakati ule hata Media za kimataifa sasa hazichukui watangazaji toka huko. BBC, VOA, DW na zingine za Kiswahili wanachukua toka Kenya au Rwanda.
 
Kwenye suala la mizania TBC nawapa heko, Taarifa ya Habari eti ni PG 13 [emoji15][emoji848][emoji87]
Mtoto anayeangalia katuni na hajafika la saba habari inamsaidia nini?
 
Waondoe na tangazo la TIGO linalomwonyesha mwanaume zuzu aliyeacha sh.10,000.00 siku ya kukumbuka kufungwa kwa ndoa yao alafu anakuta mzigo wa 50,000.00, mwishoni kabisa mwa tangazo ni aibu tubu, waliondoe.

hilo tangazo si lilisifiwa humu, nilijua lapendwa na wengi 😄😄😄🤣
 
3: Kituo cha #EastAfricaRedio kimekutwa na hatia ya kurusha maudhui yenye kukashifu utendaji wa Serikali katika uteuzi wa mdhibiti na mkaguzi mkuu wa hesabu za Serikali (CAG) na kupewa onyo kali pamoja na kutozwa faini ya Shilingi milioni 3.
Serikali hii ina mapeaa mengiiiiiiii.

Mniombee.
 
Back
Top Bottom