Viwanda vya kusafisha mafuta Barani Ulaya vyafungwa kwa sababu ya ushindani kutoka kwa kiwanda cha Dangote

Viwanda vya kusafisha mafuta Barani Ulaya vyafungwa kwa sababu ya ushindani kutoka kwa kiwanda cha Dangote

Strong ladg

Senior Member
Joined
Jul 15, 2021
Posts
170
Reaction score
445
Viwanda vya kusafisha mafuta ( oil refineries) vya barani Ulaya vimeanza kuonja joto la jiwe baada ya kiwanda cha kusafisha mafuta cha Dangote kuanza kufanya kazi.

Kiwanda hicho cha Dangote ambacho ni miongoni mwa viwanda vikubwa zaidi vya kusafisha mafuta duniani kimesababisha viwanda vya mafuta vya Ulaya vilivyokuwa vikitegemea soko la Afrika hasa Afrika magharibi kukosa soko kutokana na ushindani ulioletwa na kiwanda cha Dangote .

Viwanda hivyo ambavyo vingi vilikuwa vinazalisha mafuta yaliyo chini ya viwango vinavyokubalika barani Ulaya vimekumbwa na hali mbaya na hata baadhi yake kufungwa baada ya bidhaa zao kukosa soko.

Mfano, mnamo tarehe 25 Novemba 2024, kiwanda cha kusafisha mafuta cha Gunvor Rotterdam Refinery cha nchini Uholanzi kilifungwa kwa sababu ya kujiendesha kwa hasara.

Soma Pia: Dangote aeleza alivyonyimwa Mafuta na Nchi yake Nigeria. Hata alipotaka kuagiza ya nje alinyimwa kibali

Pia, waendeshaji wa kiwanda cha kusafisha mafuta cha Grangemouth cha Scotland ambao ni PetroIneos wameeleza kuwa watakifunga kiwanda hicho ifikapo mwakani 2025 . Sababu iliyotajwa na waendeshaji hao ni ushindani mkali ulioletwa na viwanda vingine vya usafishaji mafuta.

Uanzishwaji wa kiwanda cha kusafisha mafuta cha Dangote ulitarajiwa kuleta mabadiliko makubwa kwenye biashara ya mafuta kati ya Ulaya na Afrika hasa Afrika magharibi.

Vyanzo/Sources:
Business NG
Vanguard
Thisdaylive
Reuters


"Nigeria's Dangote oil refinery could accelerate European sector's decline | Reuters" https://www.reuters.com/business/en...celerate-european-sectors-decline-2024-03-27/
 
Kama Africa watajitolea kucopy , kuedit na kupaste anachofanya Alhaji Aliko Dangote ,itakuwa ni kuliinua bara la Africa. Fikiria Nigeria kutoka kuagiza mbolea ,na sasa wao ndiyo wanauza mbolea Marekani na Brazil. Hapo washavuka kuagiza sukari . Tukija kwenye hiki kiwanda kilichomchukua Dangote zaidi ya miaka 8 kupigania ujenzi na vibali , kimeleta ukombozi wa kuchakata mafuta wanayochimba ndani na kupata petrol,diesel n.k kimesaidia kupata mafuta yenye ubora, bei nafuu na kupandisha Naira dhidi ya dola.
 
Ndio maana Dangote alianza kupigwa viuta kali sana kuzuia kiwanda chake kisianze kazi. Kweli waafrika ni tumbili yaani tulikuwa tunatumiwa kumkandamiza mwaafrika mwenzetu kwa faida ya mkoloni?
Kabisaa. Wanasiasa wa Nigeria walikuwa wanatumika. Ndio maana viwanda vya kusafisha mafuta vya serikali vilifungwa bila sababu za msingi . Mafuta ya Nigeria yakawa yanaenda Ulaya halafu Nigeria wanaishia kupata mafuta ya viwango vya chini wakati nchi yao ina utajiri wa mafuta
 
Kama Africa watajitolea kucopy , kuedit na kupaste anachofanya Alhaji Aliko Dangote ,itakuwa ni kuliinua bara la Africa. Fikiria Nigeria kutoka kuagiza mbolea ,na sasa wao ndiyo wanauza mbolea Marekani na Brazil. Hapo washavuka kuagiza sukari . Tukija kwenye hiki kiwanda kilichomchukua Dangote zaidi ya miaka 8 kupigania ujenzi na vibali , kimeleta ukombozi wa kuchakata mafuta wanayochimba ndani na kupata petrol,diesel n.k kimesaidia kupata mafuta yenye ubora, bei nafuu na kupandisha Naira dhidi ya dola.
Shida kuna baadhi ya viongozi ni vibaraka. Hawatakubali haya maendeleo
 
Ulaya gani hiyo wanayofunga refineries kisa kakiwanda kamoja ka Dangote kanakopatikana Nigeria na katakaozalisha mapipa 650,000 kwa siku at maximum capacity?

Yani Dangote akiuza mafuta yake yote kwa Algeria bado hawajitoshelezi sembuse Ulaya nzima yenye viwanda na matumizi makubwa ya nishati. Wabongo bwana!
 
Ulaya gani hiyo wanayofunga refineries kisa kakiwanda kamoja ka Dangote kanakopatikana Nigeria na katakaozalisha mapipa 650,000 kwa siku at maximum capacity?

Yani Dangote akiuza mafuta yake yote kwa Algeria bado hawajitoshelezi sembuse Ulaya nzima yenye viwanda na matumizi makubwa ya nishati. Wabongo bwana!
Kuna vyanzo vya habari nimeweka hapo. Kama huamini unaweza wewe mwenyewe kuingia Google ukajionea. Karne hii hakuna kudanganyana kila kitu kipo wazi na kila mtu anaweza kujionea. Halafu kiwanda cha Dangote kiko Top 3 ya viwanda vikubwa vya kusafisha mafuta duniani. Usiite kakiwanda ndugu yangu. Hela iliyowekezwa hapo sio mchezo. Ingia online ujionee kila kitu mwenyewe
 
Dangote ni moja ya waafrika WA kipekee..Ni bahati kuishi nchi moja na watu WA mfano wake.....Hapa Tz Magu alimpa Bahresa mashamba na uwezo WA kuzalisha sukari kupitia Viwanda.....Kuna bomba linakaribia kukamilika la kusafirisha crude oil Kutoka Uganda mpaka Tanga chongoleani.....Na Zaidi Uganda yupo karibu na south sudani Kwa hio bomba Hilo Hilo linaweza kuungwa mpaka south sudani yenye hazina kubwa ya crude oil....Sasa na Sisi WA tanzania tuache upumbaf badala ya kusafirisha hio crude kwenda ulaya na uchina Bahresa (au matajiri wengine WA kuaminika) apewe kibali kingine cha kutengeneza refinery pale tanga tuachane na ujinga mtupu wa kuagiza white products ambazo zimekuwa refined ulaya...
Kwa sababu crude ina thamani kubwa na ndani yake unapata Diesel,,, petrol,,kerosene,,,jetA1,,hfo,,lhfo,,meroxite,,,LPG na lami...Au ikishindikana kwa matajiri wa hapa tz aitwe Dangote Tu.
 
Dangote ni moja ya waafrika WA kipekee..Ni bahati kuishi nchi moja na watu WA mfano wake.....Hapa Tz Magu alimpa Bahresa mashamba na uwezo WA kuzalisha sukari kupitia Viwanda.....Kuna bomba linakaribia kukamilika la kusafirisha crude oil Kutoka Uganda mpaka Tanga chongoleani.....Na Zaidi Uganda yupo karibu na south sudani Kwa hio bomba Hilo Hilo linaweza kuungwa mpaka south sudani yenye hazina kubwa ya crude oil....Sasa na Sisi WA tanzania tuache upumbaf badala ya kusafirisha hio crude kwenda ulaya na uchina Bahresa (au matajiri wengine WA kuaminika) apewe kibali kingine cha kutengeneza refinery pale tanga tuachane na ujinga mtupu wa kuagiza white products ambazo zimekuwa refined ulaya...
Kwa sababu crude ina thamani kubwa na ndani yake unapata Diesel,,, petrol,,kerosene,,,jetA1,,hfo,,lhfo,,meroxite,,,LPG na lami...Au ikishindikana kwa matajiri wa hapa tz aitwe Dangote Tu.
Uganda wanajenga refinery kule kwao. Nadhani huo mradi wa Refinery ndio ule unaoitwa Kingfisher. Wanajenga bomba la kusafirisha Crude Oil na wanajenga Refinery ambapo hiyo tenda ya refinery kapewa mwarabu kutoka UAE
 
Uganda wanajenga refinery kule kwao. Nadhani huo mradi wa Refinery ndio ule unaoitwa Kingfisher. Wanajenga bomba la kusafirisha Crude Oil na wanajenga Refinery ambapo hiyo tenda ya refinery kapewa mwarabu kutoka UAE
Uganda wametumia akili,,,,ninatamani na Sisi Tutumie hicho kitonga tuwe independent na Sisi la sivyo Kwa hela ya Uganda ilivyo chini Zaidi ya shilingi yetu hatutashangaa malori Kutoka Uganda kutuletea mafuta Safi huku kwetu kutokana na usingizi...Kumbuka wakati Tipper ikiwa refinery Lita ya petrol ilikuwa TSH 180 Tu.....Kama bomba limekuja mpaka sebuleni kwetu tutabidi tujiulize tumekanyaga nini kama hatutajenga refinery yetu...
 
Uganda wametumia akili,,,,ninatamani na Sisi Tutumie hicho kitonga tuwe independent na Sisi la sivyo Kwa hela ya Uganda ilivyo chini Zaidi ya shilingi yetu hatutashangaa malori Kutoka Uganda kutuletea mafuta Safi huku kwetu kutokana na usingizi...Kumbuka wakati Tipper ikiwa refinery Lita ya petrol ilikuwa TSH 180 Tu.....Kama bomba limekuja mpaka sebuleni kwetu tutabidi tujiulize tumekanyaga nini kama hatutajenga refinery yetu...
Hapo sasa itategemea na maono ya viongozi wetu wa juu,kama wakiendekeza mlungula tutabakia pale pale
Nakumbuka kipindi fulani nyuma mafuta yalikuwa sh 500,dah wenye magar enzi walipiga sana misele,msimbazi tu una cruise ile mbaya
 
Hapo sasa itategemea na maono ya viongozi wetu wa juu,kama wakiendekeza mlungula tutabakia pale pale
Nakumbuka kipindi fulani nyuma mafuta yalikuwa sh 500,dah wenye magar enzi walipiga sana misele,msimbazi tu una cruise ile mbaya
Mkuu tukiwa na refinery itarahisisha maisha Sana...Hata Hii LPG inayotumika kupikia inakuwa bei rahisi Sana..Mtungi Mdogo bei ni 24,000/-lakini unaweza kuuzwa hata elfu8 au elfu 9kama tunayo refinery yetu binafsi....Leo ukiwa na gari na usipokuwa na bajeti ya kueleweka ya mafuta utaliona gari ni mzigo na liability...... Viongozi wetu wawaze kuyafanya maisha yawe marahisi kwa kutumia watu matajiri tulio nao Tanzania
 
Hilo pungasese achana nalo,
Kuna vyanzo vya habari nimeweka hapo. Kama huamini unaweza wewe mwenyewe kuingia Google ukajionea. Karne hii hakuna kudanganyana kila kitu kipo wazi na kila mtu anaweza kujionea. Halafu kiwanda cha Dangote kiko Top 3 ya viwanda vikubwa vya kusafisha mafuta duniani. Usiite kakiwanda ndugu yangu. Hela iliyowekezwa hapo sio mchezo. Ingia online ujionee kila kitu mwenyewe
npunga
 
Mkuu tukiwa na refinery itarahisisha maisha Sana...Hata Hii LPG inayotumika kupikia inakuwa bei rahisi Sana..Mtungi Mdogo bei ni 24,000/-lakini unaweza kuuzwa hata elfu8 au elfu 9kama tunayo refinery yetu binafsi....Leo ukiwa na gari na usipokuwa na bajeti ya kueleweka ya mafuta utaliona gari ni mzigo na liability...... Viongozi wetu wawaze kuyafanya maisha yawe marahisi kwa kutumia watu matajiri tulio nao Tanzania
Kweli kabisa tatizo kubwa ni ubinafsi,viongozi wanaangalia maslahi yao na familia zao ndio maana wakichukua mlungula tu wengine mtajijua,lkn ukiwa kiongozi mwenye maslahi mapana kwa taifa na kwa wananchi wako hakika utafanya maamuzi ambayo yatafanya maisha ya wananchi wako yawe nafuu na yenye furaha

Naamini kabisa Afrika tunaweza kufanya mambo makubwa lakini bado tuna mentality za kusubir wazungu watufanyie mambo kisha sisi tuwe soko tu
 
Kweli kabisa tatizo kubwa ni ubinafsi,viongozi wanaangalia maslahi yao na familia zao ndio maana wakichukua mlungula tu wengine mtajijua,lkn ukiwa kiongozi mwenye maslahi mapana kwa taifa na kwa wananchi wako hakika utafanya maamuzi ambayo yatafanya maisha ya wananchi wako yawe nafuu na yenye furaha

Naamini kabisa Afrika tunaweza kufanya mambo makubwa lakini bado tuna mentality za kusubir wazungu watufanyie mambo kisha sisi tuwe soko tu
Nilikuwa nasoma jinsi taasisi zinazohusika na sekta ya nishati Nigeria zilivyokuwa zinampiga vita Dangote,,,mpaka unadhani sio mnigeria mwenzao,,,mara mafuta yana content nyingi ya sulphur,,,mafuta yako chini ya kiwango na pia wakamwekea kiwango cha kuuziwa crude...basi nikajiuliza kumbe hata nigeria wanaendekeza siasa hadi kwenye mambo ya kutumia akili..Na wale viongozi wakubwa wako kimya kama hawaoni.....Ubinafsi wanauweka mbele halafu wanafanya maamuzi ya kipuuzi ya mda mrefu kiasi yanakuja kuwaathiri hata wao wanaporudi mtaani....Na hata kama walipata maslahi ni ya kuwasaidia wao binafsi kwa mda mfupi..
 
Kuna vyanzo vya habari nimeweka hapo. Kama huamini unaweza wewe mwenyewe kuingia Google ukajionea. Karne hii hakuna kudanganyana kila kitu kipo wazi na kila mtu anaweza kujionea. Halafu kiwanda cha Dangote kiko Top 3 ya viwanda vikubwa vya kusafisha mafuta duniani. Usiite kakiwanda ndugu yangu. Hela iliyowekezwa hapo sio mchezo. Ingia online ujionee kila kitu mwenyewe
Refinery ya Dangote inazalisha BPD ngapi na Ulaya inatumia BPD ngapi?

Dangote akizalisha mafuta at maximum capacity, achana na sasa bado hajakamilisha. Akizalisha at full capacity mafuta yake hayaitoshi Algeria ikiwa peke yake.
Sasa anawezaje fanya Ulaya wafunge refineries? Ulaya since hata Dangote hajaanza kujenga refinery wako kwenye decline ya uzalishaji na matumizi ya mafuta, kuna nchi Ulaya hapo mafuta waliyokuwa wanatumia early 2000s ni mengi kuliko sasa.

Mafuta ya Dangote yote hayazidi 30% ya matumizi ya Ujerumani peke yake. Dangote anaweza teka soko la West Afrika kama Ghana akawauzia na akafanya vizuri sana kwa Nigeria ila sio kufanya refineries za Ulaya kufungwa. Hata asingejenga bado zingefungwa zaidi na zaidi na sio kisa yeye.

Ulaya refining capacity wengine sio wachimbaji, gharama kubwa meli kubeba crude kupeleka Ulaya yasafishwe kisha yaende sokoni, Ulaya consumption inapungua, COVID-19 iliua sana biashara, Urusi ina vikwazo, Middle East ndio kabisa wanajitegemea. Dangote anakuja kwa mbali
 
Nilikuwa nasoma jinsi taasisi zinazohusika na sekta ya nishati Nigeria zilivyokuwa zinampiga vita Dangote,,,mpaka unadhani sio mnigeria mwenzao,,,mara mafuta yana content nyingi ya sulphur,,,mafuta yako chini ya kiwango na pia wakamwekea kiwango cha kuuziwa crude...basi nikajiuliza kumbe hata nigeria wanaendekeza siasa hadi kwenye mambo ya kutumia akili..Na wale viongozi wakubwa wako kimya kama hawaoni.....Ubinafsi wanauweka mbele halafu wanafanya maamuzi ya kipuuzi ya mda mrefu kiasi yanakuja kuwaathiri hata wao wanaporudi mtaani....Na hata kama walipata maslahi ni ya kuwasaidia wao binafsi kwa mda mfupi..
Viongozi wa hizo taasisi walikula Rushwa. Wengine walikuwa wanamiliki Refineríes zinazotengeneza mafuta ya viwango vya chini huko Ulaya halafu wanayauza Nigeria.Walihofia soko lao. Mafuta yanayotoka kwa Dangote yanafikia viwango vya juu zaidi vinavyohitajika na EU yaani mafuta ya Dangote yanauzika POPOTE DUNIANI. Tangu dunia iumbwe ndio kwa mara ya kwanza Nigeria wananunua mafuta yénye viwango vya juu. Siku zote walikuwa wanauziwa yale makapi kutoka Ulaya.
 
Back
Top Bottom