Viwanja vinavyomilikiwa na CCM

Viwanja vinavyomilikiwa na CCM

Kichuguu

Platinum Member
Joined
Oct 11, 2006
Posts
17,048
Reaction score
22,790
Kama kuna jambo linalokera sana ni pale viwanja vilivyokuwa vya umma kabla ya mfumo wa vyama vingi kuporwa na CCM ambayo imeshindwa kuviendeleza. Inaonekana kama wangekuwa na uwezo walitaka hata jengo la Ikulu liwe la CCM.

Natoa hoja kuwa viwanja vyote ambavyo vilikuwa vya umma kabla ya mfumo wa vyama vingi virudiswhe serikalini kama ilivyo uwanja wa Uhuru.

Mkwakwani, Amri Abeid, Kirumba, Ali Hassan Mwinyi, Nelson Mandela, Samora na vingine vingi virudishwe serikali mara moja; havikujengwa na CCM bali vilijengwa na wananchi wote. Uwanja wa Mkwakwani umekuwapo tangu wakati wa Ukoloni; uwanja wa Amri Abeid ulijengwa kabla hata CCM haijazaliwa; na hata vile vilivyojengwa baada ya CCM havikuwa vimejengwa kama vitega uchumi vya CCM bali vilijengwa kama viwanja vya burudani kwa wanachi wote.

Sijui kama nimeeleweka.
 
Naunga mkono hoja 100% ila hili suala ni gumu kutekelezwa bila msukumo wa kisheria na kijamii. Lakini una uhakika viwanja vyote ulivyotaja vilirudishwa serikalini? Mbona bado Kirumba unaitwa CCM Kirumba? Kuna ule wa CCM Liti upo Singida. Na serikali inapeleka fedha za umma kuviboresha.
 
Naunga mkono hoja 100% ila hili suala ni gumu kutekelezwa bila msukumo wa kisheria na kijamii. Lakini una uhakika viwanja vyote ulivyotaja vilirudishwa serikalini? Mbona bado Kirumba unaitwa CCM Kirumba? Kuna ule wa CCM Liti upo Singida. Na serikali inapeleka fedha za umma kuviboresha.
hukunielewa
 
Itakavyobadilisha ni either katiba mpya au chama kingine Kishinev hatamu
 
Ccm lazima itaondoshwa kwenye hivyo viwanja na baada ya hapo lazima wataburuzwa mahakamani ili walipe damages kwa muda wote ambao wamevitumia hivyo viwanja.
 
Back
Top Bottom