Vladimir Putin amewataka wanajeshi wa Ukraine wajisalimishe wenyewe

Hata cuba ni taifa huru, lakini walikaribisha Russia military base , marekani atavamia haraka sana
 
Nimechoka kusikia kila mmoja anaongea lake,natamani sehemu ambayo nitapata kujua nini kiini hasa cha mgogoro huu!

Sina upande sipendi vita!
 
Watu wanashabikia tu,hawajui vita haina macho
 
Ukraine ilipinduliwa mwaka 2014,marekani wakaweka watu wao ukraine ikawa vasaal state wa US.
Lengo la Russia ni kuirudisha ukraine kwenye sphere of influence yake kama zilivyo, Beralus na Kazakhstan
 
Yule Zelensky ni myahudi kichaa, amegoma kukimbia kiev na kavaa combart, Yuko front
 
Lakini umejiuliza kwa Nini ameamua kuchukua maamuzi ya kijinga hivyo?? Je kwa taifa lake hakuna faida??, Je kiusalama alikuwa na hatari gani??. Pia kumbuka USA na huwa anafanya hivyo kwenye interest za taifa lake.
 
Kiusalama je..?? Hujui alikuwa hatarini Sana Kama ukrein ingejiunga na Nato pamoja na Eu
 
Majimbo hayajajitenga leo, lakin huyu Rais hajaridhia kujitenga huko, bado anawaona kama waasi.
 
They are clearly already prepared for any sanction they could face, they wouldn't have invaded if sanctions would bring them down
 
Tatzo humu ndani watu wanamlaumu putin bila kujua sababu..
Afu nmegundua watz wengi hawajui vitu vingi wao kazi yao ni kusoma vichwa vya habar ya ulaya na us na kumlaum putin bila kujua hata chanzo ni nn...
Safi sana Putin.. wao si wahuni tuone sasa
We unaejua hebu tiririka basi.Hakuna haki ya kumuua binadamu mwenzako tafuta kote kwenye vitabu vya Mungu na sheria za nchi
 
Lakini umejiuliza kwa Nini ameamua kuchukua maamuzi ya kijinga hivyo?? Je kwa taifa lake hakuna faida??, Je kiusalama alikuwa na hatari gani??. Pia kumbuka USA na huwa anafanya hivyo kwenye interest za taifa lake.
Ok, let me put it exactly. Ukraine si tishio kwa Urusi kama nchi bali ni tishio kwa aina ya utawala wa Putin. Labda kwa anayeona kuwa Putin ndiyo Urusi na Urusi ni Putin! Haina silaha za nyuklia wala jeshi kubwa kama la Urusi. Si mwanachama wa NATO. Ombi lake halijakubaliwa.

US nayo sio mfano mzuri. Uvamizi mwingi waliofanya ni wa kihuni kwa maslahi ya watu binafsi km ule wa Iraq, kukalia Afghanistan hata vita ya Vietnam. Zote zilikuwa na uongo mwingi tu.

Putin ni absolute dictator. Hakuna mtu wala mhimili wa kudhibiti maamuzi yake. Anaendesha nchi kwa mkono wa chuma. Yeye pekee ndiye anayejua “maslahi na mustakabali wa Urusi”! Private sector inamilikiwa na oligarchs - wawekezaji wanaotegemea fadhila za Putin kufanya biashara.

Ukraine ni nchi ya kidemokrasia inayofuata mfumo wa kisiasa na kiuchumi wa magharibi (USA na EU). Uchumi wake ni more modern na unakua kwa kasi. Raia wake wana uhusiano wa karibu na kindugu na raia wa Urusi. Warusi wengi wanapinga uvamizi huu.

Nchi ya aina ya Ukraine kuwa mpakani mwa Urusi ni tishio kubwa kwa utawala wa Putin asiye na mpango wa kuachia madaraka - sio tishio kwa Urusi. Raia wa Urusi wanaona na wanavutiwa na Ukraine. Upinzani kwa Putin unaongezeka. Rejea raia wa iliyokuwa East Germany walivyokuwa wakitorokea West Germany enzi za cold war na ukuta wa Berlin.
 
Marekani anaitaka Ukraine ili awe karibu kum-control Putin na Urusi, anautumia mwavuli wa NATO ili apate access kamili na Ukraine... Shida ya Putin siyo kuiongoza Ukraine ila kuzuia isijiunge na NATO ikawa lango la USA kuwa karibu na kuibomoa URUSI.

Marekani anachokifanya ni kugeuza Nchi za watu wengine ni Uwanja wa VITA zake na maadui wake, ndo maana kapigana vita nyingi lakini zote hajapigana kwake kwahiyo hayo maneno yake matamu ya kutaka DEMOKRASIA ni ya kinafki tu.....

Kwahiyo URUSI na USA wanapigania maslahi yao tu hapo lakini UWANJA wa vita ni UKRAINE.
 
Sio kweli. Fuatilia maoni ya Putin kuhusu makosa yaliyosababisha kuvunjika kwa USSR ndio utajua kero yake kubwa na harakati zake za kutaka kuifufua himaya ya Urusi kama ilivyokuwa. Ukraine ni moja ya jamii muhimu sana za taifa la Urusi.

Urusi sio tishio kubwa tena kwa Marekani. Silaha za nyuklia wote wanazo, kiuchumi Urusi imeshuka. China ndio tishio kubwa hata katika teknolojia zote inakuja kwa kasi zaidi wakati Urusi inachechemea.

Tangu kuisha kwa Cold War, Marekani imepunguza harakati zake Ulaya na kuwaachia EU na NATO. Inajishughulisha zaidi na masuala ya alqaeda na ISIS na inaumiza kichwa zaidi kuhusu China.

Of course Marekani imefanya ujinga mwingi katika kuvamia iraq, Afghanistan na hata zamani zile Vietnam. Lakini haijawa tatizo kwa Urusi huko Ukraine. Hilo ni zigo alilojitwisha Putin mwenyewe.
 
Namkubali Sana putin.huo ndo uanaume ,story kidogo ukiendelea kujifanya mjuaji action!!
 
Mlisema hawezi leo umejuaje, tulieni mnyolewe, Babu yenu Biden anaongea Kama anamafua
Ni kweli Urusi ina Nguvu kubwa Sana za Kijeshi Tena Sana. Lakini hawezi hata siku moja kuthubutu kutumia kombola la Nyuklia kwenye Vita. Kombola la Nyuklia ni kwa ajili ya Duterrence(Kutishia). Kinachosababisha mpaka Sasa NATO washindwe Kuingia vitani kuisaidia Ukraine ni kwasababu Russia ana Nyuklia Waepons ambazo zikitumika Basi NO WINNER,All are LOSSERS.

Urusi ina Makombora 7500 ya Nyuklia kwa takwimu za NIT. Makombora 2500 yako tayari kufyatuliwa kuelekea Endeo lolote Lile Duniani litakapotumwa. Marekani ina Miji mikubwa 358 na Majimbo 54. Kombora Moja linaugeuza mji kuwa Majivu kabisa. Kama Mrusi akituma Makombora yote 2500 kuelekea Marekani,Basi ndani ya dakika 30 hakutakuwa na USA Duniani.

Kwa Upande Mwingine,Marekani ina Makombora ya Nyuklia 6800. Kati ya hayo, 3500 yako tayari kufyatuliwa ndani ya Dakika 5 wakipokea Order na Direction ya kuyafurumusha. Urusi ina Miji mikubwa 43. Endapo USA akiona Russia kashatuma Makombora Yake kuelekea Marekani na hakuna jinsi Basi ndani ya Dakika 5, Makombora 3500 ya Marekani yatakuwa njiani kuelekea Urusi kuteketeza Miji 43,Ndani ya Nusu saa hakutakuwa na Urusi Tena. Hiyo inaitwa MUTUAL ASSURED DESTRUCTION(MAD).

Haya Sasa,Tuseme wewe ni Raisi wa Russia,utarusha hayo Makombora kuelekea Marekani au utafanya juhudi za majadiliano?

Mwishoni mwa Vita baridi kabisa (1988) Nchi za Marekani na Urusi Zilikuwa na Akiba ya Makombora 127,000 (Laki moja na elfu ishirini na Saba). Kati ya hayo, 58,000 ya Urusi na 69,000 ya USA. Embu fikilia. Kombora Moja linafuta mji mmoja wa Dar. Je,Dunia ina Miji 127,000? Jibu ni Hapana.

Kwahiyo ndugu yangu usiwe na tempa unapokuwa unachangia hizi maada,tumia Logic utaelewa tu.

Urusi na Marekani wanajuana,wakikutana Anga Furani Kila mmoja anaangalia Nani anamaslahi makubwa na anamwachia ili kuepusha Vita.

Georgia Mwaka 2008 Marekani hakuingiza mguu kusaidia Nchi hiyo dhidi ya Uvamizi wa Russia kwasababu Marekani anajua hapo Russia ana maslahi Makubwa.

Iraq mwaka 2003 Russia hakutia Mguu kwasababu Marekani alikuwa na Maslahi Makubwa.

Libya mwaka 2011 Russia hakutia Mguu kwasababu USA alikuwa na Maslahi Makubwa.

Venezuera Marekani aliogopa Msululu wa wakimbizi kumiminika nchini Marekani hata Kama angeliamua Vita Urusi angelipisha Coz pale ni Maslahi Makubwa ya kiusalama kwa USA.

Syria pale Wote Urusi na USA wanamaslahi na ndio maana mpaka Sasa wameigawana kijanja. Urusi inamhitaji Assad kwasababu Anamdai pesa ndefu. Marekani anahitaji Mafuta ndio maana mpaka leo Majeshi ya Marekani yapo Syria kulinda Visima vya Mafuta.

Kuhusu Ukraine,hata Marekani anajua kabisa Maslahi ya Urusi ni Makubwa kwahiyo lazima akae pembeni. Atashiriki tu kijanja lakini sio moja kwa moja.

Kuhusu NORTH KOREA,Yeye Ana Mabomu 10 TU ya Nyuklia kwahiyo hata akiacha atupe Mabomu yake Marekani atateketeza Miji 10 ya Marekani Kati ya 358. Kwa upande mwingine,NORTH KOREA ana miji 7 Mikubwa. Marekani akituma Makombora Yake ya Nyuklia 3500 nadhani unaona kabisa Makombora Mengine hayana pa Kupiga kabisa.

MTz 255Dar.
 
Shukran kwa kuongeza elimu hii muhimu. Kuna wengi hapa wanafikiri hii ni mechi ya mpira kati ya US na Urusi.

Inatakiwa wajue hii miamba inavyopima mambo yao. Putin angekuwa na UHAKIKA kuwa akivamia Ukraine basi US nao wanaingia vitani kikamilifu asingethubutu kuanzisha vita hiyo. Ingekuwa ni midahalo hadi kesho kutwa. Sasa anajua Marekani hawamtilii maanani kiasi hicho. Wamemuacha ajidunishe mwenyewe na watu wake hadi watie akili.
 
Akili ya wasiwasi hii
Kama wewe ni msomi ndg yangu...nenda kaanze tena kg one
Dah......
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…