Mosi, Watanzania fanyeni kazi kwa bidii kila mmoja kwa nafasi yake, ili kwanza kupata maendeleo binafsi kiuchumi...
Pili, Watanzania wa kada zote epukeni kuendekeza rushwa na ubadhirifu wa fedha za umma, waliopewa nafasi ya kuwa wafanyakazi kwenye taasisi za umma wamegeuka kuwa wala fedha na wabadhirifu waliopindukia...
Tatu, Watanzania wengi wangali wajinga wasioweza kutumia hata 3% ya ubongo ambao wamepewa bure kabisa na Mungu. Watanzania walio wengi kwa makusudi kabisa wamekuwa ni watu wa kukiuka taratibu za kimaendeleo zilizoanishwa wazi na hata ambazo hazipo wazi (zinazohitaji common sense) na ndio maana utaona Watanzania wanaharibu miundombinu kama ya barabara, wanajenga nyumba kiholela tu, mambo ya kipuuzi yana wafuasi wengi kuliko mambo ya maana n.k