VOA: Zaidi ya Wanajeshi 80 wa Burkina Faso wauawa na Wanajihadi. Rais Traore akimbia Ikulu na kujificha ikihofiwa Uasi wa Jeshi

Kaka unaweza kufafanua maana ya ubepari na maana ya ujamaa kinachotokea sasa hivi ni utofauti wa viwango vya kuaply hizo sera hakuna taifa linalo operate fully Capitalism ama Socialism
Tofautisha capitalism na free market economy,free market economy ipo kitambo, capitalism ni wenye pesa kuilekeza serikali Cha kufanya,ndiyo ilivyo marekani,ndiyo maana palikua na maandamano juzi kati ya wamarekani kuitaka nchi yao toka kwa matajiri ambao ni 1% ya wamarekani
Kamari zilikuwepo wakati wa Nyerere,watu hawakukamatwa uzururaji Bali walikamatwa Kodi,kipindi hicho huruhusiwi kufanya biashara na kazi ilikua kuajiriwa taasisi za serikali na kilimo,kilimo hufanyika masika iweje ukamate watu uzururaji kiangazi!?..ukishaweka soko huria huo siyo ujamaa Tena hata Kama utauita ujamaa, shilling yetu kutoachwa mbali na Dola si kwa sababu ya uimara wa uchumi,wajamaa serikali hudhibiti thamani ya pesa pia,ndiyo maana ya centralized economy,kila kitu ni serikali kuu,hayo mazao ya biashara tulouza nje hayakua ya watu binafsi Bali umma,katani na kahawa
 
Hakuna wamajihadi hapo wewe Pro US, hao ni 'vijana' wa kazi waliasisiwa na kuwezeshwa na US, France
 
huduma za kijamii nyingi zilipatikana kwa uhakika.
Huduma za kijamii kwako ni nini?

Wakati wa Nyerere kulikuwa na barabara za lami?
Wakati wa Nyerere raia wangapi walikuwa na maji ya bomba?
Wakati wa Nyerere kulikuwa na Hospitali za Wilaya hata za serikali?
Wakati wa Nyerere raia wangapi walikuwa wanapata huduma za simu?
Wakati wa Nyerere wastani wa maisha ya mtanzani ulikiwa miaka mingapi?
 
Yani kwa dunia ya leo afrika inaamka kutoka kwenye usingizi wa utumwa na kumnyenyekea mnyonyaji lakini kuna mazombie bado wanamdifia mmarekani fuuh tutafika tukiwa tumechoka sana😂🚮
 
Acha porojo nyingi, "Nordic model" ni mfumo wa welfare capitalism na sio huo ukomunisti wa zamani wa China, USSR na ujamaa wa Nyerere.
 
Wegner hawezi kumlinda siku zote, pia wegner siyo wengi wakiweza kukabiliana na uasi wa jeshi
Hakuna Uasi burkinafaso muasi ni marekani na ufaransa na hawaja ondoka bali wamejificha vichakani wanahitaji kurudi kwa njia nyingine amkeni afrika ni yetu mzungu anakwao mbn mnashsbikia movie eti mmarekani ni noma? Mnasahau uhalisia wa maisha ya waafrika?
 
Hivi vikundi vinavyojunasibu ni vya kiislamu huwa vinapigania nini hasa??
Naanza kuamini kua hawa ni vibaraka wanaotumia uislam vibaya.
Ubaya zaidi unakuja pale mamlaka za kiislam hazikemei ujuha huo na kuonekana wanaunga mkono.

Huko Palestine waislam karibu dunia nzima ni #nasimamanapalestine ila hizi jihad za hao waovu hatuoni wakizikemea, imekaaje hii??
 
Hayo mataifa ya Burkina Faso, Mali na Niger kama wamemuondoa Mfaransa kusudi wafanye sub kwa kumuingiza Mrusi basi wanajidanganya sana.

Huwezi ukawa na Mrusi kisha ukapata maendeleo hilo halijawahi kutokea na halitakaa litokee kwani hakuna taifa lolote linaloweza kuwa karibu na Russia kwa kuachana na nchi za magharibi likapiga hatua yoyote ya kimaendeleo, hakuna.

Yale mataifa ya Ulaya mashariki yaliyokuwa chini ya USSR yalikuwa ni choka mbaya hadi yalipo achana na Russia na kujiunga na kambi ya Marekani na washirika wake ndio sasa hivi wanapiga hatua kimaendeleo.

Russia sio taifa la kukaa naye karibu na hao akina Burkina Faso, Mali na Niger wajiandae kwa mapinduzi mengine wananchi wao hawatakubali ushirika wa kuwanufaisha waroho wachache kwa kisingizio cha kuzichukia nchi za magharibi.
 
Sasa kumkataa Mmarekani/Mfaransa kisha unamkubali Mrusi sasa hapo akili iko wapi..😛😛😛
 
Huyo uliyemqote ni chawa maarufu humu wa yule bibi mtembeza bakuli na anayependa kuwakamua wanainchi kwa matozo yasiokuwa na kichwa wala miguu..... kwa hiyo usitegemee ataona jema Kwa bwana Ibrahim Traore maana akilini mwake kiongozi mzuri ni yule anayewalamba makalio wazungu na kuwapa rasilimali kiholela hole kwa kigezo cha kuimarisha demokrasia.
 
Kwamba waendelee kubaki kwenye makucha ya mmarekani kuliko kuwa huru???

Waafrika wenye akili na mindset kama yako ni sababu kubwa kwanin hili bara litaendelea kuwa maskini na kutawaliwa mpaka kiama.
 
Kwamba waendelee kubaki kwenye makucha ya mmarekani kuliko kuwa huru???

Waafrika wenye akili na mindset kama yako ni sababu kubwa kwanin hili bara litaendelea kuwa maskini na kutawaliwa mpaka kiama.
Hili bara litaendelea kutawaliwa mpaka kiama baada ya waafrika kuachana na utamaduni wao na kukumbatia tamaduni za kigeni wanazodanganywa kwamba ni dini.

Waafrika wamerubuniwa hadi kujiita majina ya mabwana zao waliowapeleka utumwani na kudanganywa kwamba ndio majina takatifu na ya dini. Bure kabisa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…