KERO Vocha za mitandao tofauti Kagera zauzwa bei ya juu

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua

Nkarahacha

Member
Joined
Oct 3, 2023
Posts
17
Reaction score
38
Kwa Sasa watumiaji wa simu za mkononi mkoani Kagera wamekumbana na tatizo la baadhi ya wafanyabiashara kupandisha bei ya vocha za simu za mikononi.

Vocha ya 500 Sasa inauzwa 600 na vocha ya 1000 Sasa inauzwa 1200 kwenye baadhi ya maduka huku baadhi ya wafanyabiashara wakidai mawakala nao wamepandisha bei za jumla.

Ninachojiuliza serikali inalifahamu hili? Je,Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania TCRA wanalifahamu hili? Je,makampuni ya simu za mkononi yanalifahamu hili?

Mamlaka ziingilie kati maana watumiaji wa simu za mkononi wanapitia wakati ngumu!

Pia soma > Tatizo la bei za vocha latua TCRA



Pia soma:
 
who cares..? nobody cares this country is πŸ˜€πŸ˜€πŸ˜€
 
Kagera ni kubwa mkuu... Ni duka la nani au wakala yyupi kuwa specific
 
Hasa pale Rusumo
 
ndugu yangu yupo mkoa wa songwe tangu kitambo ananunua hizo bei, yaani raisi na genge lake la watumishi njaa wameshindwa kuwadhibiti wafanyabiashara kupandisha bei holela jamani....wapo bize tu kusema chagua ccm
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…