DOKEZO Vocha za Mitandao ya simu zadaiwa kupandisha bei kiholela Mbozi

DOKEZO Vocha za Mitandao ya simu zadaiwa kupandisha bei kiholela Mbozi

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'

BigTall

JF-Expert Member
Joined
Mar 9, 2022
Posts
525
Reaction score
1,257
WhatsApp Image 2024-05-06 at 12.39.43_c59858c7.jpg

Wafanyabiashara katika Mji wa Mlowo, Mbozi wamedaiwa kupandisha vocha za mitandao ya simu toka bei halisi na kuongeza kiwango kati ya shilingi 100 hadi 200 kutokana na eneo hali ilioibuka malalamiko kwa watumiaji wa mitandao ya simu.

Wakiongea malalamiko yao mbele ya mwandishi wetu wamedai imekuwa ni kawaida ya wafanyabiashara kupandisha vocha hasa kipindi hiki cha kuelekea katika bajeti.

"Tunaomba serikali iwachukulie hatua na kuwatia hatiani baadhi ya wafanyabiashara ambao sio waamini mfano vocha ya 500 tunanunua 600 na vocha ya 1000 tunanunua 1200 sasa huku ni kutuumiza jamani" alisema John Milango mkazi wa forest.

Akiongea mmoja wa wafanyabiashara wa vocha ambae aliomba jina lake lihifadhiwe alidao nao wamekumbana na ongezeko la bei toka kwa wafanyabiashara wa jumla wa vocha wamewapandishia bei ya vocha hivyo imepekea nao kupandisha.

Chanzo: habarijamiitanzania

===========


Nimeona hii taarifa nikaamua kushea hapa, ukweli ni kuwa Wananchi wengi tunaumizwa na hiki kitu, TCRA na TCRA CC mkoa wapi raia tunaumizwa.

Dunia ya Digitali bado upatikanaji wa vocha ni changamoto.

Pia soma - Serikali yaiagiza TCRA kufatilia wanaouza vocha tofauti na bei elekezi
 
Wanunue kupitia mpesa, tigo pesa et al....

Ila mara nyingi analaumiwa mfanyabiashara au mwenye mtandao kumbe serikali ndio kisababishi kwa matozo yao

 

Wafanyabiashara katika Mji wa Mlowo,Mbozi wamedaiwa kupandisha vocha za mitandao ya simu toka bei halisi na kuongeza kiwango cha shilingi 100 hadi 200 kutokana na eneo hali ilioibuka maswali kwa mitandao ya simu.

Wakiongea malalamiko yake mbele ya mwandishi wetu amedai imekuwa ni kawaida ya kutuma maombi ya kipindi hasa kuelekea katika malipo.

"Tunaomba serikali iwachukulie hatua na kuwatia hatiani baadhi ya ambao sio waamini mfano vocha ya 500 tunanunua 600 na vocha ya 1000 tunanunua 1200 sasa huku ni kutuumiza jamani" alisema John Milango mkazi wa forest.

Akiongea mmoja wa kutuma wa vocha ambae aliomba jina lake lihifadhiwe alidao nao wamekumbana na toleo la bei toka kwa jumla wa vocha wamewapandishia bei ya vocha hivyo imepekea nao kupandisha.

Chanzo: habarijamiitanzania

============


Nimeona hii taarifa nikaamua kushea hapa, ukweli ni kuwa Wananchi wengi tunaumizwa na hiki kitu, TCRA na TCRA CC mkoa wapi raia tunaumizwa.

Dunia ya Digitali bado upatikanaji wa vocha ni changamoto.
Hata kijijini kwetu katika mkoa wa Iringa watu wanauziwa vocha kubwa vocha ya sh 500 wanauziwa sh 600 na vocha za sh 1000 wanauziwa sh 1200.
Nesikia taarifa kuwa na mwanza hii tabia imeanza kwa baadhi ya wafanya biashara
 

Wafanyabiashara katika Mji wa Mlowo,Mbozi wamedaiwa kupandisha vocha za mitandao ya simu toka bei halisi na kuongeza kiwango kati ya shilingi 100 hadi 200 kutokana na eneo hali ilioibuka malalamiko kwa watumiaji wa mitandao ya simu...
Si waweke kwenye akaunti wanunue kwa bei ya kawaida.

Kwanza hizo karatasi zinachafua mazingira tu.
 
Vocha zimepanda bei Kila mahali wauzaji WA vocha walikua wananua kwa sh 950 kwa jumla inamaana vocha za 10,000 unapata faida ya 500 ikapanda bei ikaenda 960 na maana vocha za 10,000 faida yake ikawa 400 na sasa imepanda Tena na kufikia 970 ina maana vocha za 10,000 unapata faida ya sh 300 na vocha za 100,000 unapata faida ya 3000 hii ndio inayopelekea wafanyabiashara kuuza hiyo bei za 600 na 1200 kutoka na jinsi wanavyonunua.
 
Hivi hii inshu ya kupandisha bei za vocha huku mitaani kwa 10% katika kila thamani ya vocha wahusika wenyewe hawajaliona hili au wameamua kuwa “BUSINESS PARTNER” na akina Manki huko madukani?
6DBDC210-AF31-4162-9B40-9E684CDDD917.jpeg
 
Back
Top Bottom