Vodacom acheni utapeli kwenye huo mchezo wa Tusua Spoti

Acehood

JF-Expert Member
Joined
Oct 1, 2018
Posts
1,653
Reaction score
2,792
Wakuu iko hivi kuna siku rafiki yangu aliitumia simu yangu kunielekeza mchezo wa tusua spoti unaochezeshwa na Vodacom, na wakati wa kufanya hivyo tiketi moja yenye mechi 14 ilikamilika na tulikata bila kulipia. Baada ya wiki moja niliweka vocha ya 1000 na walikata 500 nikapewa ujumbe kuwa nimelipia ile tiketi.

Ilikuwa jana zikiwa wiki zaidi ya 2 toka wakate ile 500, nimeweka vocha ya 2000 ili niunge bando la 2000 lakini cha kushangaza sikufanikiwa, kuja angalia salio nilikuta ipo 1500. Hivyo nikaunga bando la 1000 ikabaki 500.

Leo nimeweka vocha ya 500 ili itimie 1000 ukijumlisha na ile niliyoiacha jana, same old shit sikufanikiwa tena kuunga bando la 1000 na baada ya kuangalia salio nakuta ipo 500.

NB: sijawahi kupewa ujumbe wakati wa makato ya jana na leo mpaka nilipowasiliana na huduma kwa wateja kwa njia ya email. Majibu yao yalikuwa haya.




 
duh! Kwa upande wangu nilijaribu kununuwa ile inaitwa jimixe dah sikupata sms uthibitisho na hela yangu500 ikaenda.Sijanunuwa tena ingawa wanatuma sana sms zao.
 
Ukitaka upagawe na hao jamaa jiunge na songesha mimi nilisanda.
Niliwapiga kwenye Mpawa inatosha.
Niliwakopa songesha Hadi 53,000 halafu nikatoa line Yao. Kuna siku nilijisahau nikarudisha line na kuweka laki kwenye simu. Walikata 53000 Yao na kuniondoa kkwenye huduma ya songesha.
Mpawa wapole Sana. Ukifika laki nne jiondoe taratiiibu.
 

Jimixe cielewag.Na makato ya songesha ya riba kubwa hatari.
 
Tafuta Hela kijana
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…