Nimefanyiwa kitu cha hovyo na Vodacom sijui ni kwangu au na kwa wengine pia kama kinawatokea.
Nimeweka vocha naambiwa kuna tatizo la kiufundi na baadae naweka tena naambiwa vocha imetumika katika namba fulani ambayo ndio namba yangu lakini nikiangalia salio na kuta ni lile lile la jana.
Huu ni utapeli wa wazi na ukijaribu kuwatafuta inbox labda Facebook unapata majibu yale ya automatic lakini huduma hakuna.
Kwa hili tu naomba Halotel mnipokee sitaki huu upuuzi wa Voda tena kwanza MB ndogo dakika chache sms 30.
Nilinunua jana salio kwa MPESA wakakata hela Ila salio halijafika nikavunga, leo mchana wamenitumia text kuwa "tatizo limerekebishwa angalia salio" nimechek nakuta zero Ila nimevunga maana hamna msaada wowote naweza pewa na Voda.
Inshort Voda ni wababaishaji kwenye baadhi ya huduma zao.
Niliweka almost elfu4 ikaingia buku tu elfu3 nzima wamechukua kesho yake nikaongea nao kwa uhuduma kwa wateja wakaniambia eti wakati naweka data yangu ilikuwa on aisee wahongo nalafu anayeongea ivyo demu nikamwambia na diploma ya It najua data ikiwa on na off wamenipiga ile ela