Ghazwat
JF-Expert Member
- Oct 4, 2015
- 23,718
- 66,267
Naaam...bila shaka wote hamjambo kabisa, na nasema Amani iwe kwenu Mungu Awatangulie..!
Ni Jumamosi nyingine ya February 15, 2020 ambapo nyasi kwenye viwanja mbalimbali kuwaka moto katika patashika ya Ligi Kuu Tanzania Vodacom Premier League (VPL).
Kwenye Uwanja wa Samora mkoani Iringa, Wenyeji Lipuli FC, Wanapaluhengo, Wanamkaribisha Mfalme wa Nyika, Mnyama Mkali Kuliko Wote Mwituni, Simba SC, mchezo ambao unatabiriwa kuwa mkali na wa kusisimu kwa muda wote wa dakika 90, kusaka alama tatu muhimu ili kujiweka katika mazingira mazuri katika msimamo wa VPL.
Kocha wa Lipuli FC Julio Helieza amesema wanaiheshimu Simba SC ni timu kubwa na zoefu, lakini wakiwa nyumbani wamejiandaa kwa lengo la kupambana kwa nguvu zote kuona wanaibuka na ushindi.
Naye Kocha wa Simba SC, Sven Vanderbroeck, amesema lazima wacheze mchezo katika kila hali ambayo wanakutana nayo, hivyo wamejiandaa vya kutosha kwa hilo kuhakikisha wanafanya vizuri, kila mchezaji yupo tayari kwa mchezo.
Nani kuibuka na furaha ya ushindi?Tusubiri dakika 90 za mchezo..Kumbuka mchezo ni kuanzia saa 10: 00 jioni, Usikose Ukaambiwa.
Ni Jumamosi nyingine ya February 15, 2020 ambapo nyasi kwenye viwanja mbalimbali kuwaka moto katika patashika ya Ligi Kuu Tanzania Vodacom Premier League (VPL).
Kwenye Uwanja wa Samora mkoani Iringa, Wenyeji Lipuli FC, Wanapaluhengo, Wanamkaribisha Mfalme wa Nyika, Mnyama Mkali Kuliko Wote Mwituni, Simba SC, mchezo ambao unatabiriwa kuwa mkali na wa kusisimu kwa muda wote wa dakika 90, kusaka alama tatu muhimu ili kujiweka katika mazingira mazuri katika msimamo wa VPL.
Kocha wa Lipuli FC Julio Helieza amesema wanaiheshimu Simba SC ni timu kubwa na zoefu, lakini wakiwa nyumbani wamejiandaa kwa lengo la kupambana kwa nguvu zote kuona wanaibuka na ushindi.
Naye Kocha wa Simba SC, Sven Vanderbroeck, amesema lazima wacheze mchezo katika kila hali ambayo wanakutana nayo, hivyo wamejiandaa vya kutosha kwa hilo kuhakikisha wanafanya vizuri, kila mchezaji yupo tayari kwa mchezo.
Nani kuibuka na furaha ya ushindi?Tusubiri dakika 90 za mchezo..Kumbuka mchezo ni kuanzia saa 10: 00 jioni, Usikose Ukaambiwa.