Ghazwat
JF-Expert Member
- Oct 4, 2015
- 23,718
- 66,267
Patashika ya Ligi Kuu Kuendelea kupigwa leo Juni 22 2021, ambapo Mabingwa wa Nchi wanawakabili Mbeya City Uwanja wa Benjamin Mkapa Jiji Dar es salaam.
Mchezo huu unatarajiwa kuwa mkali na wakusisimua kwa muda wote wa dakika 90 huku kila timu ikihitaji alama tatu muhimu ili kuweza kujiweka sawa kwenye msimamo wa VPL.
Simba SC ambao ndo Vinara wa VPL wakiwa na alama 70 wanawakabili Mbeya City waliopo nafasi ya 13 wakiwa na alama 36 ambapo leo City wanaingia dimbani wakiwa na kumbukumbu ya kupoteza mchezo wa mkondo wa kwanza wa 1-0 kwenye Uwanja wa Sokoine.
Je Simba SC ataendeleza ubabe wake au Mbeya City atakataa uteja? Dakika 90 kuamua. Kumbuka mchezo ni kuanzia saa 1:00 Usiku Usikose Ukasimuliwa.
Kulitaka Mwana Kulipewa Mwana
..... Ghazwat......
================
Timu zipo uwanjani zikifanyiwa ukaguzi salamu pamoja na kupiga picha za kumbukumbu. Kuashiria kuanza kwa Kandanda.
00' Naaaam mpira umeanza dakika 90 za jasho na damu Uwanja wa Mkapa | Simba SC 0-0 Mbeya City
05' Hakuna timu imeona lango la mwenzake huku Simba SC wakikosa nafasi ya kufunga baada ya Miquissone shutiiiiii lake kutoka nje na kuwa goal kick.
15' Simba wamepata Kona mbili ambazo haikuzaa matunda baada ya mabeki wa City kuokoa hatari zote hivyo kuweka ugumu wa mchezo huu | Simba SC 0-0 Mbeya City.
20' Mchezo ni mkali kosa za hapa na pale huku Simba wakimiliki zaidi mpira kuliko Mbeya City | Simba SC 0-0 Mbeya City
30' Bwalya Goooooooooaaal Goooooooaaal
Rally Bwalya anaipatia Simba SC bao la kwanza kwa shutiiiiii kali likimuacha golikipa Mandanda akiruka bila mafanikio | Simba SC 1-0 Mbeya City.
Simba SC walisakama lango la Mbeya City huku City wakizuia lango.
Anakwendaa Miquissone anapiga shutiiiiii Goooooooooaaal Goooooooaaal
Luis Miquissone anaipatia Simba SC bao la pili kwa shutiiiiii | Simba SC 2-0 Mbeya City.
Mbeya City wanamjaribu Kakolanya kwa shutiiiiii kali mbali, lakini anadaka.
Kapombe yupo chini baada ya kupata rabsha ameinuka mpira unaendelea.
45+2' Kuelekea kuwa mapumziko Uwanja wa Mkapa. Naaaam mpira ni mapumziko ambapo Simba wapo mbele kwa mabao mawili kwa bila.
VPL, HT: Simba SC 2-0 Mbeya City
Kipindi cha lala kwa buriani kimeanza huku kukiwa hakuna mabadiliko kwa pande zote mbili.
46' Goooooooooaaal Goooooooaaal Bocco anahesabu bao la tatu akipokea pasi murua kutoka kwa Hussein | Simba SC 3-0 Mbeya City.
City wanajenga mashambulizi kuelekea Simba hatariiiiiii
50' Goooooooooaaal Goooooooaaal. Pastory Athanas, anaipatia Mbeya City bao la kwanza baada ya mabeki wa Simba SC kushindwa kumzuia.| Simba SC 3-1 Mbeya City.
City wameamka kipindi hiki cha pili huku wakipata Kona mbili ambazo haikuzaa matunda.
60' Ametoka Bwalya na ameingia Chama upande wa Simba SC huku Sangija akionyeshwa Kadi ya Njano
Athanas anaonyeshwa Kadi ya Njano baada ya kumdanganya refa eneo la 18
65' Ametoka Bocco na ameingia Kagere upande wa Simba SC. Huku City wakikosa nafasi ya kufunga.. ilikuwa hatari sana mpira wa piga nikupige.
78' Simba SC wanaongoza huku City wakijaribu kutafuta bao la pili.. Mabadiliko upande wa Simba, ameingia Mzamir nafasi ya Morrison.
85' Chama Goooooooooaaal Goooooooaaal.
Mpira mrefu uliopigwa na Nyoni unamkuta Kapombe na kutoa pasi murua kwa Clatuos Chama na kuandika bao la Nne | Simba SC 4-1 Mbeya City.
90+3' Kuelekea kumalizika kwa mchezo, huku Onyango akionyeshwa Kadi ya Njano
Nafasi ya kurudisha mabao yote kwa City yanazidi kufifia.
Naaaam umekwishaaa ambapo Simba SC wameibuka na ushindi mnono wa mabao manne kwa moja dhidi ya Mbeya City, hivyo kuelekea kunusa harufu ya Ubingwa.
FT, VPL: Simba SC 4-1 Mbeya City.
.... Ghazwat....
Mchezo huu unatarajiwa kuwa mkali na wakusisimua kwa muda wote wa dakika 90 huku kila timu ikihitaji alama tatu muhimu ili kuweza kujiweka sawa kwenye msimamo wa VPL.
Simba SC ambao ndo Vinara wa VPL wakiwa na alama 70 wanawakabili Mbeya City waliopo nafasi ya 13 wakiwa na alama 36 ambapo leo City wanaingia dimbani wakiwa na kumbukumbu ya kupoteza mchezo wa mkondo wa kwanza wa 1-0 kwenye Uwanja wa Sokoine.
Je Simba SC ataendeleza ubabe wake au Mbeya City atakataa uteja? Dakika 90 kuamua. Kumbuka mchezo ni kuanzia saa 1:00 Usiku Usikose Ukasimuliwa.
Kulitaka Mwana Kulipewa Mwana
..... Ghazwat......
================
Timu zipo uwanjani zikifanyiwa ukaguzi salamu pamoja na kupiga picha za kumbukumbu. Kuashiria kuanza kwa Kandanda.
00' Naaaam mpira umeanza dakika 90 za jasho na damu Uwanja wa Mkapa | Simba SC 0-0 Mbeya City
05' Hakuna timu imeona lango la mwenzake huku Simba SC wakikosa nafasi ya kufunga baada ya Miquissone shutiiiiii lake kutoka nje na kuwa goal kick.
15' Simba wamepata Kona mbili ambazo haikuzaa matunda baada ya mabeki wa City kuokoa hatari zote hivyo kuweka ugumu wa mchezo huu | Simba SC 0-0 Mbeya City.
20' Mchezo ni mkali kosa za hapa na pale huku Simba wakimiliki zaidi mpira kuliko Mbeya City | Simba SC 0-0 Mbeya City
30' Bwalya Goooooooooaaal Goooooooaaal
Rally Bwalya anaipatia Simba SC bao la kwanza kwa shutiiiiii kali likimuacha golikipa Mandanda akiruka bila mafanikio | Simba SC 1-0 Mbeya City.
Simba SC walisakama lango la Mbeya City huku City wakizuia lango.
Anakwendaa Miquissone anapiga shutiiiiii Goooooooooaaal Goooooooaaal
Luis Miquissone anaipatia Simba SC bao la pili kwa shutiiiiii | Simba SC 2-0 Mbeya City.
Mbeya City wanamjaribu Kakolanya kwa shutiiiiii kali mbali, lakini anadaka.
Kapombe yupo chini baada ya kupata rabsha ameinuka mpira unaendelea.
45+2' Kuelekea kuwa mapumziko Uwanja wa Mkapa. Naaaam mpira ni mapumziko ambapo Simba wapo mbele kwa mabao mawili kwa bila.
VPL, HT: Simba SC 2-0 Mbeya City
Kipindi cha lala kwa buriani kimeanza huku kukiwa hakuna mabadiliko kwa pande zote mbili.
46' Goooooooooaaal Goooooooaaal Bocco anahesabu bao la tatu akipokea pasi murua kutoka kwa Hussein | Simba SC 3-0 Mbeya City.
City wanajenga mashambulizi kuelekea Simba hatariiiiiii
50' Goooooooooaaal Goooooooaaal. Pastory Athanas, anaipatia Mbeya City bao la kwanza baada ya mabeki wa Simba SC kushindwa kumzuia.| Simba SC 3-1 Mbeya City.
City wameamka kipindi hiki cha pili huku wakipata Kona mbili ambazo haikuzaa matunda.
60' Ametoka Bwalya na ameingia Chama upande wa Simba SC huku Sangija akionyeshwa Kadi ya Njano
Athanas anaonyeshwa Kadi ya Njano baada ya kumdanganya refa eneo la 18
65' Ametoka Bocco na ameingia Kagere upande wa Simba SC. Huku City wakikosa nafasi ya kufunga.. ilikuwa hatari sana mpira wa piga nikupige.
78' Simba SC wanaongoza huku City wakijaribu kutafuta bao la pili.. Mabadiliko upande wa Simba, ameingia Mzamir nafasi ya Morrison.
85' Chama Goooooooooaaal Goooooooaaal.
Mpira mrefu uliopigwa na Nyoni unamkuta Kapombe na kutoa pasi murua kwa Clatuos Chama na kuandika bao la Nne | Simba SC 4-1 Mbeya City.
90+3' Kuelekea kumalizika kwa mchezo, huku Onyango akionyeshwa Kadi ya Njano
Nafasi ya kurudisha mabao yote kwa City yanazidi kufifia.
Naaaam umekwishaaa ambapo Simba SC wameibuka na ushindi mnono wa mabao manne kwa moja dhidi ya Mbeya City, hivyo kuelekea kunusa harufu ya Ubingwa.
FT, VPL: Simba SC 4-1 Mbeya City.
.... Ghazwat....