Ghazwat
JF-Expert Member
- Oct 4, 2015
- 23,718
- 66,267
Patashika ya ligi kuu Tanzania Vodacom Premier League VPL kuendelea kupigwa tena leo February 7, 2020 ambapo Mnyama Mkali, Simba SC, wanawakabili JKT Tanzania.
Patashika hii ya aina yake ikiwa ni mzunguko wa pili, inatarajiwa kuwa kali na ya kusisimua kwa muda wote wa mchezo.
Simba SC kwenye mzunguko wa kwanza ameshinda mechi 16, akitoka sare 2 na kupoteza 1 huku JKT Tanzania akishinda michezo 7 sare 6 na akiwa amepoteza michezo 6.
Nani kuanza na furaha kwa duru hili la pili la VPL? Dakika 90 kuamua..Kumbuka mchezo kuanzia saa 10: 00 jioni, Usikose Ukaambiwa.
=====
Simba imepoteza mchezo wa pili msimu huu Ligi Kuu Bara baada ya kukubali kichapo cha bao 1-0 dhidi ya JKT Tanzania kwenye Uwanja wa Uhuru, Dar
Bao pekee la ushindi limefungwa na Adam Adam dakika ya 24 ya kipindi cha kwanza ambalo limedumu mpaka mwisho wa kipindi.
Nyota wapya wa Simba, Luis na Shiza Kichuya wameanza leo kwa mara ya kwanza.
Mchezo wa kwanza walipokutana Simba ilishinda mabao 3-1 na leo kisasi kimelipwa kwa JKT kushinda bao 1-0.
Patashika hii ya aina yake ikiwa ni mzunguko wa pili, inatarajiwa kuwa kali na ya kusisimua kwa muda wote wa mchezo.
Simba SC kwenye mzunguko wa kwanza ameshinda mechi 16, akitoka sare 2 na kupoteza 1 huku JKT Tanzania akishinda michezo 7 sare 6 na akiwa amepoteza michezo 6.
Nani kuanza na furaha kwa duru hili la pili la VPL? Dakika 90 kuamua..Kumbuka mchezo kuanzia saa 10: 00 jioni, Usikose Ukaambiwa.
=====
Simba imepoteza mchezo wa pili msimu huu Ligi Kuu Bara baada ya kukubali kichapo cha bao 1-0 dhidi ya JKT Tanzania kwenye Uwanja wa Uhuru, Dar
Bao pekee la ushindi limefungwa na Adam Adam dakika ya 24 ya kipindi cha kwanza ambalo limedumu mpaka mwisho wa kipindi.
Nyota wapya wa Simba, Luis na Shiza Kichuya wameanza leo kwa mara ya kwanza.
Mchezo wa kwanza walipokutana Simba ilishinda mabao 3-1 na leo kisasi kimelipwa kwa JKT kushinda bao 1-0.