Vodacom Premier League 'VPL Uwanja wa Uhuru Dar: Simba SC 0 - 1 JKT Tanzania

Hili la fraga ni goli halali, sema kwasababu waamuzi wetu wameshabaa ndio maana hizi blanda haziwezi kuisha.
 
Reactions: Lee
59' Luis kwake Kahata, kwake Luis tena anapigaaaa shutiii njee daah ilikuwa hatari

Wakati huo huo JKT wameanza kupoteza muda mchezaji mmoja yupo chini
 
63' John Bocco ameingia kuchukua nafasi ya Ajibu

Fraga ametoka na ameingia Claotus Chama, upande wa Simba
 
Luis anafanyiwa faulo, eneo hatari sana ni free kick kuelekea JKT

Chama anapigaaa Bocooo golikipa anadaka bila wasiwasi
 
Narudia tena. Miaka ya nyuma vilabu hivi vikubwa Simba na Yanga vilikua na kasumba ya kuchukua wachezaji kutoka Afrika Magharibi. Nilikua naona wanakosea sana kwani mchezaji wa kiwango kutoka upande huo wa Afrika hawezi kuja Tz kucheza soka la hali ya juu. Ama atakwenda Ulaya au hata Asia au Afrika ya Kaskazini

Nikawa nashauri kua kuna wachezaji kutoka DRC na Burundi wana viwango vikubwa sana na ni cheap lakini ilichukua muda hadi miaka ya hivi karibuni ndio viongozi wa vilabu vyetu wamegundua hilo

Ujinga mwingine upo kwenye kuamini makocha wa kizungu kuwa wana viwango vizuri. Ni kweli lakini sio makocha wote hasa hawa wanaokuja kufundisha Tanzania.

Kama kuna kosa Simba walilifanya ni kumuondoa Masoud Djumaa. Nadhani ipo siku watakuja kugundua kosa lao na pengine yaweza kua too late
 
Mpira unapigwa kwake Boccoooo laaaaaaaaaa, mpira unapaa juu ya lango, wakati huo huo golikipa yupo chini.

Wanapoteza muda wameridhika na bao moja

Simba SC 0-1 JKT
 
Yupo chini tena golikipa wa JKT muda mchache baada ya kutibiwa hiii ni mbinu ya kupoteza muda
 
Tuongee ukweli wana simba, mwenendo wa timu yetu uwanjani hauridhishi hata kama tunashinda. Yaani inakuwa nyepesi sana kufungika, ukweli lazima usemwe.
Uko sahihi! Kuna tatizo mahali
 
Golikipa wa JKT ametolewa nje na machela yaonesha hawezi Kuendelea na mchezo

Naam ameingia golikipa mwingine
 
89' Kagere anakosa kumalizia krosi ya Chama, ilikuwa nafasi bomba kwa Simba kusawazisha

Simba 0-1 JKT
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…