Nyie@Vodacom Tanzania
1. Muanzishe kifurushi cha wiki cha University offer (CHEKA YA CHUO) kama ndg zenu Tigo na Airtel. Sie wanachuo hatuna hela za kuunga kila siku; sehemu ni vyuo vikuu vyote , Tanzania.
2. KUHAMISHA SALIO: Tatzo liko kwenye kuhamisha salio kutoka mtu mmoja voda kwenda mwingine voda. Mnakata tozo (ada) na hela (salio) then salio halimfikii mlengwa, huku mmeisha lamba hela. Bolesheni system ya Me2u. Tz nzima.
3. M-PESA: Kwasababu product ya M-PESA, ni leading Mobile Money Transfer Agent in Tanzania. Nawaomba muanzishe No (For calling, free of charge) special kwa ajili ya huduma ya Miamala iliyo kosewa (kutuma/kupokea) pesa. Huwa mna ile 100, iko too busy sana. Wajanja wa hapa town ukikosea tu dk1 washa kuliza na line-tupa kule.
4. Muwe na Customer Service Officers walio somea IT jameni, achaneni na warembo wanao paka lipstick na rangi hadi kwenye meno, huku wakiwa wamesoma, Bachelor of Arts in Education (Geography&Kiswahili).Hawajui kitu wala kutatua tatizo hawawezi. Nafahamu hapa ni vigumu kunielewa kwani ni vitowewo vyenu-ila jaribuni!!
5.SWITCHING MOBILE PHONE OFF WHILE SERVING: Ni vyema mkawa na muda wa kuchat na Simu ofisini either Tea Break or Lunch time (uwepo lakini) kwani nyie mnatuhamasisha Tujismartphonishe, na kuzima simu wahudumiapo. HIZI SIMU ZA DIGITAL NI HATARI KWA MUDA WA KAZI. Na hawa warembo-nilio wataja hapo(4), ni mabingwa wa kupiga picha na kupost nguo zake zote za kabatini, huwa wanatumia masaa 2 kati 8 ya kazi (Working hours ) kuchati. Either Akiwa anapost picha au ana Tag picha au ana LIKE au ana COMMENT au akiwa ana SEMA Ahsante kama kasifiwa, hadi amalize ndio akusikilize. Hii pia itawasaidia BENKI mbalimbali nchi Tz, kwa ufanisi bora.
Feedback kwangu ni jambo nalo lipa kipaumbele, kila la kheri ktk kuijenga Tz nyenye ufanisi.
Ni hayo tu mura, mjipange!!!