Vodacom Tanzania: Support thread (Maswali, malalamiko na Ushauri)

Mimi ni mwez sasa. Nawaripoti TCRA
 
Ni aibu kubwa kwa mtandao mkongwe kama Vodacom katika huduma yake ya MPESA kutokuwepo na menu ya kumuwezesha mteja kurequest statement ya mwezi, miezi mitatu na miezi sita eti mpaka uende physically VODASHOP, This is ridiculous, yaani kwa karne hii kweli bado mmeshindwa kuwa wabunifu mkaweka hii huduma kwenye menu ya simu au la mmeshindwa kabisa tuwekeeni hiyo huduma kwenye website yenu. Watu wenu wa IT sijui wanafanya kazi gani??? La mmeshindwa igeni kwa wenzenu "tigo jihudumie" huduma bora kabisa iliyoko kwenye tigopesa.

Mimi ni mhasibu wa kikundi ambacho members hutuma michango yao...yaani members wakituma fee zao kupitia MPESA ni sheeeda, sometimes hata meseji haziji unakuta lumpsum, mpk uende vodashop kufuatilia statement ndo ujue nani walituma.....its bulsheet. INAKERA SANA.

Pili meseji inayokupa taarifa ya kiasi gani umetuma na balance gani imebaki haisemi kiasi gani mmekata kwa huduma husika kama wenzenu wa tigopesa wanavyofanya.

Tatu menu ya mpesa au sub menu zenu hazina option ya kurudi nyuma one step au kurudi menu kuu.....ukitaka kurudi nyuma mpk upige upya aidha *150*00* au ni kifurushi *149*01#....igeni wenzenu wa tigo ukishabofya *150*01# ukaingia kwenye submenu unaweza anza kurudi nyuma kwa kubofya 99.

Nimeripoti hili swala several times customer care...but hola...hamna utekelezaji....msitulazimishe tupige kampeni members wetu waache kutuma kwa mpesa.

Nawasilisha.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Daah yan mkuu umeongea kitu cha maana saana yan voda kwenye huduma za kifedha wanasumbua saana.

Kama ulivyosema menu hazina option za kurud nyuma aaf pia kuna kitu kina ni kera kweli yan hapa TANZANIA benki ya NMB ndo benki inayoongoza kwa kuenea zaid lakini mpesa hawajaweka huduma zao kule.ukitaka kuchukua cash au float kutoka nmb huwez pata kupitia mpesa ni tigo na Airtel nk.

Hata namba za miamala niza ajab ajab wanajifanya unique kwa upuuz wakati had Airtel waliwaiga Tigo mfumo wa namba za miamala.
Yan actually ukiwa unafanya huduma za kifedha kupitia Tigo mtu unakua more comfortable, unlike Vodacom. [emoji57][emoji57][emoji57]

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wajipange upya

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Binafsi nina mashaka na vodacom.

Tarehe 8/9/2017, nilikua natoa pesa kutoka kwa wakala mwenye no. 367544 wa babati Manyara, kwa bahati mbaya nikakosea kuandika namba ya wakala na pesa ikatoka kwa wakala mwingine anaitwa Wariankira Ezekiel mndeme simfahamu huyu, na serio no ya muamala nilioufanya ni 4I89TZTHJF.

Nilipiga simu kwa voda huduma kwa Wateja nilichojibiwa... Sina hamu hata leo.

Eti huyo wakala hana Salio hivyo basi tena huwezi pata hiyo pesa.

Vodacom kama mlinzi na anayejali usalama wa pesa za Wateja wake kama yeye anavyojinadi, leo ananijibu hivyo!!?

Kwa nini tunasajili line za simu na mawakala?

Ni kweli huyu mtu hawezi kupatikana na akarudisha pesa ya watu?

Vodacom. Nilirudishieni 30,000/- yangu
 
Kwa kwel huu mtandao wa vodacom kuna muda unakera sana haiwezekan kwa muda wa siku 2 intaneti inakuwa ovyo kabisaa

Mnajua wengine kazi zetu zinategemea internet sasa mnapodhoofisha huduma yenu mnajua ni hasara kiasi gan tunayopata?

Jana nilinunua kifurushi cha masaa 24 ambacho leo ndio kitaisha lakin hadi kinaelekea kuisha nadhan hata mb 200 sijatumia... Yan hata kufungua nyuz za JF inakuwa ngumu

Ningependa kuyaomba makampuni ya simu endapo kuna itirafu au matengenezo yoyote ya mitambo yenu muwe mnatupa taarifa mapema wateja wenu ili tuchukue hatua mbadala
 
True that. Me inasoma 3G but speed ni ya kobe. Nmeswitch to tgo 4g will be back later
 
Mitabdao ipo mingi ikizingua hamia kwingineko huzuiwi wacha kulalamika umefunga nao ndoa ya maisha
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…