Vodacom Tanzania: Support thread (Maswali, malalamiko na Ushauri)

Vodacom Tanzania: Support thread (Maswali, malalamiko na Ushauri)

Me pia ni mdau wa voda na mfanyabiashara ila kwenye hili wanafanya ujinga
Kama mtu amepiga sm kudai lain ifungwe ametuma kimakosa why wasinipigie na mm na kutuunganisha ukweli uwe wazi ndo wafunge line
Mijitu inaagiza mizigo mkoa inalipa na kupiga sm hela irudishwe voda wanakimbilia kufunga line
***** zenu
Nilipiga huduma kwa wateja nikaulizwa ulishawahi kuripot account yako ifungwe nikwaambia hapana,
Wakaniambia niende vodashop nikatumia nauli
Nafika pale naambiwa kuna mtu ali riport ifungwe na isifunguliwe bila kupigiwa yeye na kaweka namba yake hapo, haya mpigieni hapatikani, basi nipeni namba hawataki kutoa namba!! Who are these if not Kima kama Kima??
 
Ndugu mteja,

Una tatizo lolote unapotumia mtandao wetu? Una ushauri wowote ili tuiboreshe huduma yetu?

Tafadhali itumie mada (thread) hii ili tukusaidie kwa urahisi.

Unapokuwa na tatizo, ili tukusaidie kirahisi zingatia haya:

  • Ni tatizo gani? (M-PESA, SMS, Calls, Internet, usajili, kukatika kwa mawasiliano n.k)
  • Maeneo gani? (Tukifahamu location, inakuwa rahisi kukuelekeza wapi uende ili upate physical assitance toka kwa vendor wetu aliye karibu nawe)
  • Tatizo limeanza lini na limejirudia au kuendelea kuwa kero kwako kwa muda gani?
  • Kama ni ushauri, zingatia ya juu lakini tutafurahi tukijua kwanini unapendekeza unachopendekeza
  • Kama ni pongezi, zingatia ya juu na tungependa pia upendekeze lipi tufanye kuzidi kuiboresha huduma kwako.

Karibu

Vodacom Tanzania
Fanyeni mtu aweze kulipia kwa app za playstore automatically. Mpesa ya safaricom inahiyo huduma. Wakisema weka payment syastem kuwena option ya mpesa.
 
Hivi voda arusha mko wapi? Yaani olasiti mtandao wenu ni shida. Hasa upande wa data. Hebu fanyeni kitu,,tuone mabadiliko.
 
Nipo biharamulo kesho natupa laini yenu mmekuwa na tabia ikifika Saa moja jioni internet haifanyi kazi mpaka Saa tano usku Kila SKU sijajua lengo lenu ni nini mpaka sasa au mnataka tunaotoka makazini tustumie data zetu maana Saa tano mtu umeshalala kwaiyo muda wa kifurushi ukifjka mtu hujatumia data mpaka muda wa kuisha kinafika kesho natupa laini yenu na naenda kuifuta kabisa yangu na ya mke wangu
 
Kwa kweli naomba Vodacom muwafikirie Wateja wanaojiunga vifurushi mara kwa Mara wawe wanapunguziwa gharama na Sio kuongezewa gharama kama mnavofanya saizi!!!!!! HILO NDIO OMBI LANGU
 
Mnachofanya ni sawa na MTU mwenye Duka anampandishia Bei mteja mkuu sababu ananunua bidhaa zaidi ya wengine.

Wakati kiuhalisia angethaminiwa kwa kupunguziwa gharama na kupata offer zaidi.
 
Jamani ,jamani ,jamani.
Mbona katangazia Zanzibar? Ingekuwa enzi za Mwendazake,angetangazia Chato?
 
Huduma ya customer service ya voda ni mbovu kuliko maelezo, mtu unapiga simu umepoteza simu unapiga wafunge line eti wanakupa namba ya WhatsApp mchat au namba ya kawaida, huko nako hakuna msaada, si uhuni tu huu
 
Fanyeni mtu aweze kulipia kwa app za playstore automatically. Mpesa ya safaricom inahiyo huduma. Wakisema weka payment syastem kuwena option ya mpesa.
Siku mkipoteza pesa ndio ntajua umuhimu wa huduma hiyo..nilishawai kutuma laki 6 kimakosa nikawai na pesa yangu ikarudi isingekuwa hivyo pesa ingetolewa
 
Siku mkipoteza pesa ndio ntajua umuhimu wa huduma hiyo..nilishawai kutuma laki 6 kimakosa nikawai na pesa yangu ikarudi isingekuwa hivyo pesa ingetolewa
Kwani hawawezi kuzuia huduma ya M-pesa kwa laini husika bila kuifungia kabisa? Mbona baadhi ya mitandao wanakufungia kisha wanakupigia simu kukuekewesha kilichotokea? Unafungaje laini ya mtu moja kwa moja bila kumsikiliza? Kama kauza bidhaa je?!
 
Hii menu mpya mliyotoa ya kuset seed ya internet ina faida na hasara gani?
 
vodacom ni lini nitapata huduma ya mikopo ya songesha na m pawa? naona nafanya miamala sana.. 0752495777
 
Simu yangu Infinx Hot 9 Play X680. Inasoma mwisho 3G haisomi H+. Line ni Voda 4G. Msaada tafadhali.
 
Back
Top Bottom