Vodacom Tanzania: Support thread (Maswali, malalamiko na Ushauri)

Waheshimiwa naombeni msaada,nimekwangua vocha vibaya nimeshindwa kuingiza baadhi ya number,nimejaribu kupiga Customer care sipati msaada [emoji25],nafanyaje ili niitumie hii vocha?
siku hizi mambo yamekua ya hovyo sana
watext neno "msaada" kwenda namba 100. Kisha fuata maelekezo.
 
Vodacom nilisajili line lakini mbona nikiweka kwenye simu haisomi inaandika no simcard lakini zingine zinasoma?
 
siku hizi mambo yamekua ya hovyo sana
watext neno "msaada" kwenda namba 100. Kisha fuata maelekezo.
Asante sana Mkuu kwa msaada wako, tangu jana nimehangaika sana,hata muda huu kabla sijasoma comment yako nimejaribu kuwapigia hakuna cha maana nilichoambulia.
 
Vodacom nawapenda na hasa internet yao shida nachukia kupokea hizi sms za kamari sijui tusua mapene nifanye nini nisipokee hizi sms za hovyo.
Iko na ile ya kuhakiki number yako,kila baada ya dk 2 inapop up,unafuata maelekezo yote lakini bado inakuja tu.Natamani hadi kublock vodacom wenyewe
 
Kwa nini Vodacom laini zenu kusevu majina mwisho majina mia moja(100)au ni laini yangu tu ndo ina ukomo huo?
 
Jamani voda kuna shida gani? Hapa maeneo ya Olasiti Arusha mtandao ni shida hasa kwa upande wa data.Signal ziko chini sana.Hili tatuzo ni la muda mrefu.
 
VODACOM mmekuja na mbinu mpya kuwaibia pesa wateja.
1. Mnaunganisha kimya kimya service ambayo siyo solicited, kama kuchagua miziki kwa makato ya shs 200/= kwa siku. Hata kwa siku moja tu, wateja 1,000,000 hapo mnaiba milioni 200!
2. Tusuamapene , ni utaratibu unakera sana. Unatumiwa msg zaidi ya 10 kwa siku ili uwachangie draw ambayo haipo.

Nina wasiwasi TCRA wanagawiwa makato kwa michezo hii.
 
Hili halina utatuzi ndugu labda tu umpate aliyekuuzia.
 

Malalamiko ya wateja kuibiwa pesa zao yamekuwa mengi na mmekaa kimya.
 
Hii mgodi ndio kitu gani nyie ?
 
Line za TIGO ,Airtel na halotel, ukiweka vocha hata ulale bila kujiunga utaikuta. Lakini voda uweke vocha haupiti muda Mara meseji za sokaletu, Wana pita na 200 Mara games za ajabu ajabu. Sasa huu wizi wa voda hebu punguzeni nshajitoa Mara kibao ila vocha ikiwekwa tu mnaunga nayo dahh
 
Hizi tabia zenu za kutuunga kwenye huduma ambazo mtu hajawahi kuomba ni ujinga, wizi na upumbafu. WHY, mnatuma SMS za mapenzi, kazi, michezo, na ushenzi mwingi ambao mtu hajaomba wala kujiunganisha? Kisa tu mkusanye TZS 100-150 kwa SMS, Kama mmeishiwa fungeni likampunilenu msilete njaa za kijinga hapa.
Bado mtu akitaka kujiondoa mnaleta chenga chenga, kwanza mjue kampuni zipo kibao ni sawa na kuchangu mademu, msibobadilika navunja line yenu na kusepa.
SHAME ON YOU!
 
Wajinga hawa imeshakuwa kampuni ya matola kulazimisha kuchukua hela kwa wateja kwa huduma ambazo hawajaziomba hata
 
Hapa nahisi kuna UKWELI kuwa TCRA wanajua kabisa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…