Vodacom Tanzania: Support thread (Maswali, malalamiko na Ushauri)

mtandao unasumbua au hizi kampuni ziko chini ya waswahili maana siku hizi ni shiida tupu badilikeni tunatumia pesa zetu c makaratasi toeni huduma nzuri kwa wateja au kwakuwa mpini mmeshika nyie.
 
Vodacom mlaaniwe.

Mmefyeka dk zangu 230 nilizonunua wiki iliyopita. Leo naambiwa bado dakika saba. Shame on you. Kwa matumizi yangu so far, zingebakia dakika si chini ya 150.
 
Vodacom mmekua wa ajabu sana. Cheka bombastic kuna option ya kupiga mitandao yote, ajabu ukimpigia mtu wa mtandano mwingine unaambiwa hapatikani, ukipiga kwa line nyingine unampata. Matokeo yake muda wa kifurushi kuisha unafika. Huu ni wizi wa mchana, BADILIKENI
 
Voda bundle kwenye vifurushi vyenu havi kidhi, mnanyonya sana watanzania ukilinganisha na kiasi mtu anachokitoa..ni simply wizi
 
Mbona mmepungunguza sana MB ktk vifurushi vyenu????

Mf. Kifurushi cha 899 ilikuwa upata 100MB... Mmepunguza hadi 10MB...... Bora mngepunguza SMS.
 
punguzeni uhuni voda mnakera sana,yani kujiunga cheka ya 500 unapata dk 19 na mb 50!! wakati ilikua 20min na 100mb!! mmeniudhi kweli na ntahamia airtel mmezidi kujifanya viziwi! mkafie huko na limtandao leo la kijizi
 

Habari Shark taarifa fupi za akaunti ya M-Pesa zinapatikana ukitembelea dukani kwetu na sio kwamba utapewa taarifa ya salio lako la mwisho.
Katika utatuzi wa masuala kuna mambo ya msingi ambayo inabidi tuelekezane na kupeana ufahamu kuhakikisha kwamba mteja anafahamu utendaji kazi wa kifaa anachotumia. Endapo unahitaji ufafanuzi wa suala lolote usisite kuwasiliana nasi.
 
Last edited by a moderator:
Habari papason hatujaondoa Personal Hotspot kwenye simu ndugu mteja, hili hutokea pindi mteja anapopandisha mfumo wa uendeshaji simu (Operating system).

Unaweza kuingia hapa kwa utatuzi zaidi;

How To Fix The Missing Personal Hotspot Feature On iOS
Fix for Personal Hotspot Missing After iOS Update | OSXDaily
 
Last edited by a moderator:
Nawashauri vodacom, kwa sisi wamiliki wa mpesa, muwe mnatutumia kamisheni zetu kwenye laini ile ile ya kazi, kama tigo pesa wanavyofanya, inakuwa usumbufu kamisheni inaingia kwenye laini ya management halafu ndo uhamishe, bado sijaona mantiki yake, kama ni kuogopa kuibiwa na mfanyakazi basi wangeondoka cash wanazofanyia kazi pamoja na float
 
Mimi nilipotelewa na salio la muda wa maongezi. Nikwapigia watoa huduma wakashindwa kutatua tatizo langu wakalipeleka mbele zaidi kwa wataalamu. Wataalamu wenu wakanipigia simu wakashindwa kuonyesha ni kivipi pesa yangu ilitumika. Baada ya kushindwa kutoa maelezo wakakata simu kwa ahadi ya kunipigia tena. Hawakufanya hivo. Nikaamua kwenda vodashop. wale waudumu nao tukashindwana wakanielekeza kwa meneja naye akokosa la kuthibitisha ni kivipi pesa yangu imetumika. mpaka sasa namsubilia mwanasheria wangu anipe ushauri.
 
Vodacom mlaaniwe.

Mmefyeka dk zangu 230 nilizonunua wiki iliyopita. Leo naambiwa bado dakika saba. Shame on you. Kwa matumizi yangu so far, zingebakia dakika si chini ya 150.
Habari, tafadhali tunaomba namba ya simu PM kwa msaada zaidi. Pole
 

Mfa maji ni kwa kipindi gani umekuwa ukipata tatizo hili tafadhali.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…