Vodacom Tanzania yafanya Uboreshaji mkubwa wa Mtandao ili kuhakikisha mustakabali imara na wa muunganiko zaidi

Mpesa ndio imekuwa takataka hizi siku mbili nimetoka kwa wakala kutuma pesa,namba sahihi jina halionekani.Afrika kazi ipo.
 
Hakuna mabadiliko yeyote, Leo nimenunua luku, nimeweka namba ya siri sikupata response yeyote ,nikarudia tena, nimekaa kama dakika 20 meseji zikarudi na nikakatwa mara mbili, huku si kutiana hasara.
 
Acheni Tabia ya kunywa vifurushi vyetu, kama mnakunywa wine 🍷 🥸🥸🥸🥸.

Mnazingua sana Aise 🤔 🤔 🤔 Vodacom Tanzania
 
November ni keshokutwa tu ngojo tusubiri hayo mabadiriko tuone
 
Kuweni serious na issue ya miamala ambayo inaonekana inahang, watu wako kwenye kipindi kigumu ikizingatiwa ni mwisho wa mwezi wengine wanatumia hela familia zao, wengine wazazi wao, wengine wanalipa bills, wengine wana wagonjwa hospitali nk.

Mlishindwa kuwa na plan mapema bila kuinterfere production? Mlishindwa kuasses mapema na kuzuia baadhi ya huduma muhimu ili msiumize watu? hasa huduma za miamala ili watu waangalie alternative nyingine? Kwa nini isiwe scheduled kwa phases na iwe inafanyika usiku mnene kwa masaa manne manne?
 
As I equally surprised by your recent ONE. Month 4GB bonus I can now understand that it was a mockery, you knowing that with such a weak network I will barely use an MB. Congratulations!
 
Mbona taarifa hamkutoa mapema na haya marekebisho ni kila mwezi au maana matatizo ya Yale yale kila siku
 
Huu mtandao una wapigaji wengi.Yaani mimi kuna kipindi walikuwa wananikata hela wanadai nimejiunga sijui na SOKA sijui na nini.Wqkati simu yangu naimilik mwenyewe na sijajiunga huo undezi.Niliwahama mazima lain ipo kama haipo.
 
Sasa bando zetu hizi zinayeyuka tu. Maana juzi nimeshindwa kutazama mpira online kwa poor netwk.

Mnapoboresha hizi huduma mzingatie pia gharama tunazokuwa tumelipia lkn tunapata huduma hafifu.

Mawasiliano yamekuwa shida nyie leo ndio mnatoa tamko, mmeshindwa hata kutujulisha kwa sms kwenye simu zetu.

Kitengo cha huduma kwa wateja mjifanyie tathmin hasa sasa tunapoadhimisha mwezi wa huduma kwa wateja.
 

Dar es Salaam: Kampuni kinara ya teknolojia na mawasiliano nchini, Vodacom Tanzania, imetangaza kufanya mabadiliko makubwa katika miundombinu ya mtandao wake ikiwa ni sehemu ya kuwahakikishia wateja wake huduma bora na za kisasa zaidi.

Akizungumzia hatua hii, Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni hiyo, Philip Besiimire alisema kuwa Vodacom imejidhatiti kuwa kinara katika ubunifu na kuboresha huduma zake kila wakati. “Ili kuendelea kuwa kinara katika teknolojia na kuwapatia wateja wetu huduma bora, tumewekeza kwa kiwango kikubwa katika kuboresha miundombinu ya mtandao wetu,” alibainisha.

Hatua hii ni muhimu kwa kuwa inaiandaa nchi na wateja wetu kuwa tayari kupokea mabadiliko ya teknolojia ya kisasa kama vile Akili Mnemba (AI) ambayo inalenga kuleta maboresho makubwa ya upatikanaji wa huduma za mtandao kwa wateja.

Besiimire alifafanua kuwa maboresho haya yanalenga kuongeza kasi, kuimarisha mtandao na kuhakikisha huduma zinaendelea kubaki imara ili kukidhi mahitaji yanayoongezeka kila kukicha. Ingawa jitihada hizi ni hatua kubwa mbele, pia zinapitia mchakato mgumu ambao unaweza kuathiri upatikanaji wa huduma katika maeneo kadhaa kwa kiasi fulani.

“Tunaomba radhi kwa usumbufu wowote ambao umewaathiri wateja wetu na tunawahakikishia kwamba tunafanya kila jitihada kupunguza usumbufu huo. Zoezi hili linatarajiwa kukamilika ifikapo katikati ya Novemba, ambapo tutakuwa na mtandao wenye nguvu na unaotegemewa zaidi kwa manufaa ya wateja wetu wote,” alisema huku akiongeza kuwa timu yake itaendelea kuufahamisha umma wakati wote wa zoezi hili na kutoa msaada wowote utakapohitajika.

Sambamba na maboresho haya, kumekuwa na upanuzi wa mtandao kote nchini huku kampuni ikiimarisha mtandao wake. Mkurugenzi wa Mtandao wa Vodacom Tanzania, Andrew Lupembe, alisema kuwa Vodacom Tanzania inafanya uwekezaji mkubwa ili kupanua na kuimarisha mtandao wake.

“Mpaka sasa tumetumia asilimia 96 ya bajeti iliyowekwa kwa ajili ya miundombinu ya mtandao. Kwanza, tumetanua matumizi ya mtandao wetu kupitia uwekezaji wa NICTBB na Africa One. Pia tumeongeza uwezo wa vituo vyetu vya mtandao na kufungua vituo vipya Tanzania Bara na Visiwani,” alisema.

Lupembe aliongeza kuwa uwekezaji huu pamoja na uhimarishaji wa mifumo ya kampuni, utaleta huduma bora zaidi na inayoaminika katika wiki zijazo. “Wateja wetu wataweza kufurahia kasi zaidi, ulinzi ulioboreshwa wa mtandao, na huduma bora za mtandao bila changamoto yoyote,” alihitimisha.
 
Hata majuzi walituma ujumbe kama huo, siku ya pili mtandao ukaanza kutusumbua.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…