Vodacom wamenifanyia unyama, kesho naenda makao makuu na mwanasheria wangu.

Vodacom wamenifanyia unyama, kesho naenda makao makuu na mwanasheria wangu.

Nimejiunga na kifurushi cha SME package ya 50k kwa mwezi yenye GB 50 pamoja na dakika 2000, GB ziliisha juzi nikabaki na dakika ambapo mpaka ijumaa usiku nilikua na dakika 998

View attachment 3154486
Matumizi yangu kwa siku ya jana hayajazidi dakika 300 kwa mujibu wa call history.
Sijapokea sms yoyote kuonesha dakika kuisha na wala nisingeweza kutumia dakika 998 kwa siku ya jana,
Leo nimeamka asubuhi napiga simu naambiwa sina salio, baada ya kuangalia salio nakuta sina dakika hata moja
View attachment 3154516


Nimeongea na mhudumu wao yeye mwenyewe baada ya kukagua amekua shoked na kunipa zile sound zao za ombi lako litashuhulikiwa baada ya masaa 24 nimemwambia kauli hii sio ngeni jijini labda kwa wageni wa mji, kesho asubuhi sina kazi wafanyakazi watanikuta getini na sitoki ofisini kwao bila dakika zangu kuwepo kwenye simu



Sitakubali sound yoyote ile ya nenda dakika zako zitarejea otherwise wanirudishie pesa yangu.
Mkuu hili tatizo limenipata pia.
Nilideposit 20k tar 14 Nov.
Nimetumia hiyo bando siku mbili, leo asubuhi naambiwa sina salio.


Nimezungumza nao wanasema suala langu linashughulikiwa ndani ya 24hrs.

Vodacom wamekuwa hawaaminiki siku hizi
 
Tigo hawaoneshi salio la kifurushi leo siku zaidi ya tano.
Wanasema utatumiwa ujumbe wa SMS shortly wa salio. Haziingii hizo sms milele.
Kifurushi kinakata Kama upepo. Nimerudi Airtel.
Hawa niliwakaba 2007 walinirudishia salio tiGo pesa 25,000. Walikuwa wananiletea matokeo ya soka kwa meseji halafu wanakata hela km 200 kila meseji, sasa wataanza matokeo ya EPL na wapi huko sijui wanakata usiku wa manane wakati nina matokeo tayari. Kiliwaka kwa meneja pale Majani ya Chai wakawasiliana na wahindi in 5 days wakashusha muamala. Nililewaje sasa...!!!!????
 
Voda mi wananikera sana ukitaka kupiga simu kuongea na hduma kwa Wateja... Aiseee utaongea na robot mpaka basi
 
Mimi huwa nanunua bundle la 24 hrs kulingana na matumizi yangu ya siku hiyo.

Hii ni kote( intaneti na dakika).

Na kama hakuna ulazima naendelea na mambo mengine.
 
Back
Top Bottom