Voices From Within: Japo 2025 Tumepanga Twende na Mwanamke, 2025 Mama Akabidhi Kwanza Mwanamume, Kisha 2030 Ndipo Aje Mwanamke

Unadhani kuna Bunge la kumpigia SSH kura ya kutokuwa na imani naye?
 
Labda haukuwepo wakati wa Mwinyi na Kikwete au ulikuwa bado hujielewi.
Sijui kwa nini huwa unapenda kujibu watu namna hiyo!!! Kwa taarifa yako nipo toka kipindi cha utawala wa Nyerere. Kama utakuwa umenipita umri itakuwa ni kidogo sana. Uwe unajibu kwa heshima basi hatuko katika mashindano ya kujibu watu vibaya. Wewe si unasema umefundishwa maadili? Basi tuyaone hayo maadili katika majibu yako.
 

Kumbe unaweza kuota sauti ya kushauri! Kushauri inaweza kukubalika au kukataliwa. Vilevile ile sauti iliyosema Rais 2025 ni mwanamke imekuaje tena
 
Kumbe unaweza kuota sauti ya kushauri! Kushauri inaweza kukubalika au kukataliwa. Vilevile ile sauti iliyosema Rais 2025 ni mwanamke imekuaje tena
Mwenyewe nimeenda kufukua like kaburi lake P la 2025 twende na mwanamke, nikasomaa weeh, nikarudia rudia, kisha huku kusoma tena!

Nikajikuta naimba kigeugeu eeh kigeugeu, nimtazame nani, nimwamini nani, wananigeukia eeh!
 
Upo jikoni nini Mkuu haya sio maono tuliyoyazoea kila ukisemacho kitokee .
 
Kumbe unaweza kuota sauti ya kushauri! Kushauri inaweza kukubalika au kukataliwa. Vilevile ile sauti iliyosema Rais 2025 ni mwanamke imekuaje tena
Mkuu Kamundu, bandiko ni hili Watanzania, tuunge mkono 2025 ni zamu ya Mwanamke, ila sio lazima awe yeye bali yule aliyepangiwa na 'YEYE', kama ni yeye aliyepangiwa, then ni yeye! ni passuasive kuwataka Watanzania tuunge mkono hoja ya 2025, twende na mgombea mwanamke, na nikasema mwanamke huyo wa 2025 sii lazima awe yeye Mama, bali yule aliyepangiwa na YEYE. Nikasema kama ni yeye, ndiye aliyepangiwa na YEYE, ni yeye!.

Sasa nimesikia sauti akiambiwa awe only one term president. Kwa vile no one is certain hii sauti niliyoisikia kama ni sauti ya YEYE au ni yeye. Kama ni sauti ya YEYE, then litatimia. Kama ni sauti ya yeye, then hili litapita na 2025 tutamuingiza ikulu mgombea mwanamke.
P
 
Unajulikana wewe vitu muhimu kwako ni udini na unazi wa CCM, hata mdudu kunguni akiwa CCM na mwislam utampa kura yako akuongoze
Aaah huna la kuwasema hao, bure unajisumbuwa, Mwinyi na Kikwete wameacha alama za uongozi Tanzania hii.

Hao ndiyo walimfanya baba'ko au babu yako wajuwe kuvaa wewe. Enzi za Nyerere watu walivalishwa ma crimplin ya kugtoka China mpaka wakashika adabu ,kwa kuunguzwa na jua, si mwanamke si mwanamme, nguo ya crimplin ikipigwa na jua na jasho kidogo inaganda mwilini utafikiri plaster. Kuja mzee mwinyi? Kila kitu kikawa Rukhsa.

Dah, wakati wa Nyerere ukionekana umevaa jeans jipya la Lee au Levis unashikwa, ukaseme umelitowa wapi au umhonge askari shillingi mbili yaishe. Waulize waliokuwepo humu wakwambie, sabuni ya kuogea ilikuwa anasa (luxury). Unataka kusema nini wewe, tuulize tulioziona awamu zote AlhamduliLlah.
 
Sasa kipi kibaya nilichokujibu? Au ukweli unakuuma?

Kama ulikuwapo wakati wa Nyerere, ulikuwa unaishi mkoa gani?Ulikuwa unasoma darasa la ngapi, nyerere alipong'atuka? Tujuwe kama ulikuwa nazo zauelewa au bado ulikuwa kichinchiri.
 
Nilishasema kitambo HAHM angalieni threads na michango kabla, 2025 ndio mwisho wa Samia na yeye anajua hilo, ifahamike hivyo, tusipuuzwe hatubahatishi kwenye mambo msingi ya nchi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…