Voices From Within: Unaweza usiamini! Aliyetoa A Go ahead kwa Mdee na Wenzake ni Kigogo wa Chadema!. Alikuwepo Ukumbini na Vikaoni! Je, ni nani?

Voices From Within: Unaweza usiamini! Aliyetoa A Go ahead kwa Mdee na Wenzake ni Kigogo wa Chadema!. Alikuwepo Ukumbini na Vikaoni! Je, ni nani?

Nimeisoma hukumu, 1. Mahakama zetu zinarudia makosa yale yale ya ukosefu wa kutenda haki kwa sababu ya legal technicalities, kuwa Mahakama haiwezi kutoa uamuzi wa kitu ambacho hakikuombwa!.
2. Wabunge hawa 19 wa Chadema, walivuliwa uanachama wao kinyume cha katiba ya JMT na kinyume cha haki kwa kutokusikilizwa, kinyume cha katiba ya Chadema kwa kukiuka sheria, taratibu na kanuni!.
3. Kikao cha CCM ya Chadema, kilichowatimua kilikaa kama a kangaroo court na kutoa maamuzi ya kikangaroo!.
4. Katiba ya Chadema inasema mwanachama kabla hajafutwa uanachama, kwanza atatumiwa hati ya mashitaka kwa maandishi by despatch, kisha atapewa siku 14 za kujibu mashitaka. Chadema hawakuandaa hati zozote za mashitaka!. Hili Mahakama ilipaswa ilione!.
5. Baada ya watuhumiwa kupewa hati ya mashitaka, ndipo kikao cha CC kinaitishwa kama mamlaka ya nidhamu, kusoma majibu ya mashitaka, na ndipo kinawaita washikiwa na kuwasikiliza. Hili halikufanyika!.
6. Baada ya wabunge 19 wa Chadema kuapishwa, hapa Chadema waliposwa kufanya kitu kinachoitwa a due process ya nidhamu na sio zile Zimamoto za kikangaroo!. There was no emergency of whatsoever!. Mahakama ilipaswa ilione hili!.
7. Uthibitisho wa hakukuwa na any emergency ya kuitisha CC, ni the time taken, kuitisha kikao cha Baraza Kuu!.
8. Baada ya kuitishwa kikao cha Baraza Kuu, kitu cha kwanza kwa Baraza Kuu Chadema kuangalia ni uhalali wa kikao cha CC, pili jee katiba, sheria, taratibu na kanuni za mamlaka ya nidhamu ya Chadema zilifuatwa?.
8. CC ya Chadema ni mamlaka halali ya nidhamu ya wabunge wa Chadema, lakini CC ya Chadema sio mamlaka ya nidhamu ya Halima Mdee ambaye ni Mwenyekiti wa Bawacha!, Mamlaka yake ya nidhamu ni Baraza Kuu!, CC ya Chadema ilipata wapi mamlaka ya kumtimua Halima Mdee?!. Kikao cha Baraza Kuu kilipaswa hili kukuona!.
9. Japo kikao cha Baraza Kuu Chadema kiliitishwa kihalali kama mamlaka ya rufaa ya wabunge wa Chadema, lakini kitendo cha kikao hicho kubariki uamuzi wa CC kuwatimua bila kufanya mapitio yoyote, ni uthibitisho wa Chadema bado ni chama kichanga, mfano kingechukua nchi ile 2015!, it would have been disastrous!.
10. Kitendo cha Baraza Kuu kubariki maamuzi ya kikangaroo ya CC ya Chadema, kilifanya niyaite maamuzi yale pia ni ya kikangaroo, na kitendo cha Mahakama Kuu kuyabari maamuzi ya kikangaroo, Mahakama Kuu yetu nayo has joined the team!.
A Way Forward
1. Kwa vile Chadema imefanikiwa kuwatimua hao 19 sasa Chadema isikate tena rufaa, kupinga uamuzi huu, bali iitishe kikao cha Baraza Kuu , ASAP, kifanye a due process, hili la wabunge 19 liishe, wabunge hao 19 wavuliwe ubunge wao, Chadema wapeleke majina 19 mengine, wateuliwe waapishwe, tuwe na Bunge la vyama vingi!.

2. Chadema wakifanya tuu dillydalling kukaa rufaa, inakula kwao!. By the time rufaa inasikilizwa, ndipo kifuate kikao cha Baraza Kuu, I'm afraid the time left before the next election is too little too late, ikibaki muda wa chini ya miezi 12 kabla ya muda wa uhai wa Bunge kuisha, hakuna uchaguzi wowote wala uteuzi wowote wa wabunge wapya!.
3. Tena nashauri kikao hicho cha Baraza Kuu, pia sasa ndio kimtimue Halima Mdee, kikifuatiwa Mkutano Mkuu kuthibitisha. Hapa najua changamoto ni fedha!, kule kwenye kile chungu, zilikopatikana zile fedha za kugharimia Baraza Kuu lile, kile chungu bado kipo, kitagharimia vikao vyote viwili, na Chadema inaweza kupiga ndege wawili kwa jiwe moja kwa mtu kupumzishwa kwa heshima na dereva mpya kupatikana!.
Paskali.
😂 Dereva atoke 😂
Devera akitoka lazima atupe gari mtaroni
 
Wanabodi,


Angalizo la Mambo ya Sauti.

Sasa sauti imeniambia the one behind hii saga yote ya kina Mdee, ni Kigogo mmoja mkubwa tuu wa Chadema!. Sauti hiyo imeniambia Kigogo huyo alikuwepo ukumbini, kwenye vikao vyote viwili vilivyowatimua kina Mdee!. Jee Kigogo huyu ni nani?,
Paskali
Soon Kigogo huyu atabainika.
Now it's only a matter of time!.
Wanabodi,

Mimi ni muumini wa kitu kinachoitwa "Karma", na nimekuwa nikikihubiri mara nyingi tuu humu jukwaani kuwa karma ndio the power pekee ambayo hutoa hukumu ya haki hapa duniani, kwenye karma, mtu unaadhibiwa au kuhukumiwa kwa mawazo, maneno na matendo yako, karma haina mswalie Mtume, wala haujui nani ni nani!, kwenye hukumu ya karma, inatembeza bakra za kutosha na adhabu kubwa ya mwisho ya karma huwa ni kula kichwa!. "The Power of 'Karma'- Ndio Hukumu Pekee ya Haki Kamili Hapa Duniani!, Unahukumiwa kwa Matendo Yako!

Mungu Ibariki Chadema at least for once iweze kutenda haki, kuepuka adhabu ya karma, maana kiukweli Chadema hapo ilipo, ni almost dead kinachosubiri ni kukomelea tuu msumari wa mwisho kwenye naniliu la Chadema na kulishusha 6ft under!. The choice is theirs!

Mungu Ibariki Tanzania!.
Paskali
Nimeliona andiko hili japo sijalisoma its contents lakini hii ni habari njema kwa Chadema View attachment 3064986 kwasababu itawaepushia karma ya machozi, jasho na damu ya makamanda hawa.

Hiki ambacho Chadema inakwenda kukifanya sasa, mimi niliwashauri kitambo CHADEMA kubalini matokeo na m-survive, or shupazeni shingo. You go to hell 6ft under Hao Makamanda 19 ni mashujaa, kuendelea Ubunge wao

Hata baada ya Chadema kushinda kesi mahakamani kuwa wametimuliwa kihalali, bado tuliwashauri Chadema
Ushauri wa bure: CHADEMA iachane na issue ya Wabunge wake 19, iwasamehe waendelee na Ubunge wao. Kwa muda uliobakia kuwatengua hakuna maslahi yoyote!
Na hili la kuwasamehe likija kutokea, mimi ni miongoni mwa tutakao farijika sana kwasababu tulishauri, tukapuuzwa, ila ushauri wetu unatekelezwa step by step Siasa za Kijungu Jiko, Penye Uzia, Penyeza Rupia!. Hakuna Mkate Mgumu Mbele ya Chai!, Hata Uwe Mgumu Vipi, Mbele ya Chai/Rupia, Lazima Utalainika!

Wawasamehe tuu yaishe!.
P
 
Exactly baada ya mbowe kuona mambo yameenda kuharibika na aibu akaona vema amuite halima Mdee juu Kwa juu auteme ubunge na Ampe kazi Kwanini awe concerned namna hiyo???


Mbowe anahusika na Uhuni unaiandama chadema sana hawajui kwamba mambo yanaendelea kuwa wazi ,

Wafuasi vichwa maji wengi wakishaweka bando na kuwa na chaji wanakuja kutukana tu hapa!

Mdee hana courage ya Kwenda kuapa bila go ahead ya Mbowe , na ile signature ni kwamba mnyika alizungukwa
Aisee!
😂 😂 😂 😂Wafuasi wa chadema hata wapewe mwalimu wa kuwafundisha kwa njia ya picha hawawezi kuelewa
 
Soon Kigogo huyu atabainika.
Now it's only a matter of time!.

Nimeliona andiko hili japo sijalisoma its contents lakini hii ni habari njema kwa Chadema View attachment 3064986 kwasababu itawaepushia karma ya machozi, jasho na damu ya makamanda hawa.

Hiki ambacho Chadema inakwenda kukifanya sasa, mimi niliwashauri kitambo CHADEMA kubalini matokeo na m-survive, or shupazeni shingo. You go to hell 6ft under Hao Makamanda 19 ni mashujaa, kuendelea Ubunge wao

Hata baada ya Chadema kushinda kesi mahakamani kuwa wametimuliwa kihalali, bado tuliwashauri Chadema
Ushauri wa bure: CHADEMA iachane na issue ya Wabunge wake 19, iwasamehe waendelee na Ubunge wao. Kwa muda uliobakia kuwatengua hakuna maslahi yoyote!
Na hili la kuwasamehe likija kutokea, mimi ni miongoni mwa tutakao farijika sana kwasababu tulishauri, tukapuuzwa, ila ushauri wetu unatekelezwa step by step Siasa za Kijungu Jiko, Penye Uzia, Penyeza Rupia!. Hakuna Mkate Mgumu Mbele ya Chai!, Hata Uwe Mgumu Vipi, Mbele ya Chai/Rupia, Lazima Utalainika!

Wawasamehe tuu yaishe!.
P
Aisee wewe jamaa sio wa kawaida yote uliyoandika yanajitokeza
 
Lkn akina Pascal Mayalla hawa hawa ndiyo wanamlamba viatu huyo kigogo aliyefanya ubatili huo.

Watanzania tulilala kwa kweli, tulipaswa kujiuliza kwamba inawezekanaje wake wa viongozi wa juu wa chama wafoji barua bila waume zao kujua?
 
Aisee wewe jamaa sio wa kawaida yote uliyoandika yanajitokeza
Pasco mimi sijawahi kumdharau hata siku moja.

Inaonekana huwa yuko ndani ya system kabisa.

Akiandika kitu huwa anakificha kwenye maneno mengi mpaka uwe na akili ya kuchqnganua vitu ndio utaona.
Na akili za kuchqnganua mambo wafuasi wengi wa chadema wamenyimwa ndio maana huwa wanaishia kumkejeli.
 
Lkn akina Pascal Mayalla hawa hawa ndiyo wanamlamba viatu huyo kigogo aliyefanya ubatili huo.

Watanzania tulilala kwa kweli, tulipaswa kujiuliza kwamba inawezekanaje wake wa viongozi wa juu wa chama wafoji barua bila waume zao kujua?
Pasco Mayalla ana nyuzi nyingi sana humu za kuwashtua chadema, ila walikuwa wanampuuza maana walikuwa wanaishia kusoma title tu na mahaba kwa Mbowe
 
Wanabodi,

Kama kawaida yangu, mimi Mzee wa "the voices from within" na Maswali Fikirishi.

Angalizo la Mambo ya Sauti.
Kuna mambo ni yetu, na mambo mengine sii yetu, mambo ambayo ni yetu, unaweza kuuliza, lakini kwa mambo ambayo sii yetu, huwezi kuuliza, miongoni mwa mambo ambayo sii yetu ni pamoja na haya mambo ya mtu kusikia sauti, ni unasikia tuu, hakuna sababu yoyote, wala ushahidi wowote ni unajikuta umeambiwa tuu.

Hapa nimesikia sauti ambayo mimi huwa naiita ""Voices From Within", hii voices from within, ni sauti ambayo unaisikia kutokea ndani yako, inakuambia kitu fulani, huwezi kuiuliza chochote ila unaweza kujiuliza kama hicho ulichoambiwa its makes sense, na kina logic?, then unajiuliza nikiseme au nisiseme, unajifanyia a self objectivity assessment tes na self censorship kwa kujiuliza nikisema kina faida, kitasaidia, au ninyamaze just to keep to myself. Unajifanyia self censorship, kisha unafikia maamuzi kusema ili kuwajulisha na wengine lakini sio lazima useme kila ulichosikia.

Hizi sauti ziko za aina nyingi, wengine huoteshwa kama ndoto, wengine huonyeshwa kama visions, na wengine, haswa ma deep thinkers, likitokea jambo, ukalifikiria sana, wakati umetulia, usually usiku mkubwa, kwenye ukimya na utulivu, ndipo unaisikia hiyo sauti au vision, wabunifu na wavumbuzi wengi hivi ndivyo wanavyovumbua!. Archimedes alipovumbua law ya floatation, alikuwa bafuni akioga kwenye bath tub, alitoka hivyo hivyo alivyo from the bathroom hadi mtaani huku akipiga kelele "eureka!, eureka!, ... yaani nimegundua, nimegundua, wala hakukumbuka tena kama alitoka hivyo hivyo bafuni kama alivyozaliwa!, wastaarabu wakamdaka kwa kunshika kwa nguvu kumsitiri wakijua ni kichaa!. Hata Sir Isaack Newton, mvumbuzi wa Newton's laws of motion, kuna siku alikuwa anapima yai linaanza kuchemka dakika ya ngapi, akachukua saa akaiweka kwenye sufuria, na kuichemsha huku amelishika yai mkononi akipima muda!, alikaa hivyo muda mrefu hadi mkewe akamuuliza ndipo akashtuka.

Hiki nilichosikia, unaweza usiamini!., unaweza kuniona Pasco ni kichaa fulani, haijalisi ni sauti ya nani, just take it or leave it, ikitokea ikiwa kweli, wewe mwana jf, unakuwa na a jf advante "be the firts to know" kumbe aliyetoa a go ahead kwa kina Mdee na kundi lake, ni kigogo wa Chadema!. Mimi niliuliza humu mkaniona kama ni kichaa fulani.

Sasa sauti imeniambia the one behind hii saga yote ya kina Mdee, ni Kigogo mmoja mkubwa tuu wa Chadema!. Sauti hiyo imeniambia Kigogo huyo alikuwepo ukumbini, kwenye vikao vyote viwili vilivyowatimua kina Mdee!. Jee Kigogo huyu ni nani?, andamana nami....

Nilikuwa nachangia mada hii

Kamati Kuu ni mamlaka ya nidhamu ya wabunge but not Halima. Kesi ya wabunge iliendeshwa kikangaroo hivyo hukumu ile ya CC ni batili.

Baraza Kuu ndio mamlaka ya rufaa ya wabunge. Baraza Kuu lilipaswa kwanza kujiridhisha kama CC ilitenda haki, halikufanya, likaubariki ukangaroo wa CC!. Hapa sasa ndio mamlaka ya nidhamu ya Halima Mdee. Hakuna kesi yoyote ya Halima iliyowasilishwa Baraza Kuu. CC ya Chadema ilipata wapi mamlaka kufukuza Halima wakati hata Baraza Kuu halina mamlaka hiyo?!. Kesi ya Halima ingetoka Baraza Kuu na kuingia Mkutano Mkuu ndio pekee wenye mamlaka hiyo. Kilichofamyika ni uhuni, ambao mimi nimeuita ni ukangaroo.

Kitendo cha kukazia hukumu batili nao ni ukangaroo!.

Rufaa zote lazima zifuate kikao kinachofuatia, Halima alikata rufaa Baraza kwasababu CC sio mamlaka yake ya nidhamu na haina uwezo wa kumfukuza!.

Hawaeezi chochote kwasababu hakuna kikao chochote kilichowateua, kule NEC hawahitaji taarifa za kikao, wanahitaji barua ya uteuzi na fomu zilizosainiwa. Barua ilikuwepo na fomu zilikuwepo na hapa ndipo nikaisikia sauti from within kuwa mtu aliyewapa go ahead kina Mdee ni Kigogo mmoja wa Chadema, ni mjumbe wa CC na siku ya kikao cha Kamati Kuu Chadema, kilichokaa kama a Kangaroo court na kuwatimua, alikuwepo!. Siku ya Kikao cha Baraza Kuu, kubariki ule Ukangaroo wa Kamati Kuu Chadema alikuwepo ukumbini!. Sauti Imeishia hapo.

Jee Kigogo Huyu ni Nani?.

Kule nyuma nimawahi kutoa tuhuma kuwa Chadema kuna kirusi, leo nilitaka ku update huu uzi CHADEMA Kuna Kirusi! Je, Unajua kirusi hiki ni Nani?! Na The Motive Behind? kwa kirusi hiki kipya, nikakuta umefungwa!, kumbe I was wrong, sio kuwa Chadema kuna "ki"- rusi!, Chadema kuna "vi" rusi! maana ni more than one!. Jee unaweza kuamini aliyasaini barua za kina Halima ni mnene mmoja wa Chadema ambaye ni mjumbe wa CC na alikuwepo ukumbini kwenye kikao cha Kamati Kuu na Kikao cha Baraza Kuu?!.

Can you mu imagine Kigogo huyu ni nani?. Anza kutafakari, mimi nitakusaidia

Nilitamani kumalizia nikupe kitu kamili lakini sisi sekta binafsii maisha yetu ni ya kukimbizana, kufukuzia tenda, tenda nyingi deadlines zake ni Monday, hivyo kuna tenda nakimbizana nayo, deadline yake ni saa 4:00 asubuhi hii

Nitarejea...
ila Matokea ya Kikao cha Baraza Kuu Chadema kuwatimua waanawake wa shoka, mashujaa 19 wa Chadema waliokipigania Chadema kwa machozi, jasho na damu, bado yanatawala mijadala mbalimbali humu jf.

Anza kwa kutembelea haya mabandiko haya anzia
hapa Ni Ubatili Mtupu Mpaka Basi!. CC ya CHADEMA ilipata wapi mamlaka?. Baraza Kuu halina mamlaka hiyo!. Je, inawezekana CHADEMA ni chama majanga ila?
na A Kangaroo Court Moja, Kutoa Hukumu Kikangaroo, Kisha Kikao cha Rufaa, Kikiyabariki Maamuzi yale ya Kikangaroo. Je, nacho ni A Kangaroo?
na Je, wabunge 19 wa CHADEMA walijiteua? Je, CC ya CHADEMA ni Kangaroo Court? Je, Baraza Kuu litabariki ukangaroo ule?
na Chadema, P'se, Msisusie Mkutano wa Vyama, Wasilisheni Hoja Zenu Mezani, Zitamfikia Samia, Ana Nia Njema na Nchi Hii, Mpeni Ushirikiano!.
na CHADEMA kubalini matokeo na m-survive, or shupazeni shingo. You go to hell 6ft under Hao Makamanda 19 ni mashujaa, kuendelea Ubunge wao
na Mmezoea vya kunyonga hamviwezi vya kuchinja. Hongera sana Halima Mdee na Makamanda wote kwa kugomea wito wa kienyejienyeji
na Makamanda walioigharimia CHADEMA kwa machozi, jasho na damu, leo ni wakuitwa wasaliti? Karma Haitawaacha salama, itawatandika tu
na Kufanya Kosa Si Kosa, Kosa Kurudia Kosa, CHADEMA is Almost Dead, Due to deadly mistakes!, This Your Only Survival, Do or Die!, Msirudie Kosa!.
na Je, wajua Vyama vya Siasa TZ ni Public Parties? Maamuzi yake lazima yazingatie Public Interest na siyo kufuata ujinga na ubinafsi wa viongozi insane!
na Bunge jipya lina hali mbaya! Serikali itafanaje kuliokoa Bunge ili kuwa na Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni?

na JPM, CCM wakishinda, Freeman Aikaeli Mbowe ni lazima ajiuzulu, amwachie Tundu Lissu. Lissu aache Uanaharakati, aonyeshe Statesmanship

na For the sake of National Unity, Je tumshauri Dkt. Magufuli aahidi kumteua Tundu Lissu kuwa Mbunge?

Paskali
Swala la Akina Halima lilifanyika ktk mazingira magumu ya kisiasa na kiuchumi. Kwanza angalia selection ya watu walioteuliwa nikuonyesha kuwa lile jambo halikuwa la siri kwasabu nasikia kuna baadhi ya wake wa viongozi na michepuko wao wote wapo. Kwahiyo hili swala lilipangwa vizuri tu. Kwenye CDM kunajulikana kuna watu wanapenda pesa maswala ya chama ni baadaye kwahiyo mipango yote ilikuwa wazi kwa mabosi wakubwa na walikuwa wanajua kila kitu ndiyo maana mimi kwa upande wangu sijawahi kuwalaamu hata mara moja Covid19 na nisinge shauri wafukuzwe kwa sababu chama chenyewe kilikuwa na viongozi ndumi la kuwili.
 
Pasco mimi sijawahi kumdharau hata siku moja.

Inaonekana huwa yuko ndani ya system kabisa.

Akiandika kitu huwa anakificha kwenye maneno mengi mpaka uwe na akili ya kuchqnganua vitu ndio utaona.
Na akili za kuchqnganua mambo wafuasi wengi wa chadema wamenyimwa ndio maana huwa wanaishia kumkejeli.
Sio wafuasi tu wa chadema,hii ni shida kubwa sana ya watanzania kariba wote,ACT,TLP,NCCR,CUF,CCM na hao Chadema...nilicheka sana jana watu walivyokuwa wanamshambulia Kigwangala kwenye ujumbe wake kule X
Mayala atakuwa ni mtu wa system ya ndani kabisa,system iliyojichimbia chini ardhini
 
Back
Top Bottom