VPL : Kagera Sugar Vs Young Africans

VPL : Kagera Sugar Vs Young Africans

Danny greeny

JF-Expert Member
Joined
Feb 6, 2014
Posts
3,856
Reaction score
1,648
Full Time | Kagera Sugar 2 - 6 YoungAfricans

90' Mins | sasa, hakuna kipya, timu zinaonyesha kucheza zaidi katikati ya uwanja, Yanga wakiwa wameridhika huku Kagera wakionekana kuwa wamekata tamaa

87' Mins | mpira wa kurusha wa Twite, Tambwe anagonga kichwa lakini Babu Ally anaokoa

78' Mins |Matheo Anthony anaingia kuchukua nafasi ya Kaseke

77' Mins | Amissi Tambwe anaingia upande wa Yanga kuchukua nafasi ya Obey Chirwa

73' Mins | Ngoma anaifungia Yanga bao la sita, ameunganisha pasi ya MSuva baada ya kumzidi kasi Kavila

63' Mins | GOOOOOO Chirwa anafunga bao la tano kwa Yanga, la pili kwake baada ya Ngoma kuuwahi mpira wa Juma Ramadhani aliyemrudishia kipa, lakini kipa Burhani akaokoa, mpira ukamkuta Chirwa ambaye amemlamba chenga na kupachika wavuni kwa mguu wa kushoto safi kabisa

57' Mins | GOOOOOOO Kaseke anafunga bao kwa shuti kali kabisa akiunganisha pasi nzuri ya MSuva aliyegongeana vizuri na Niyonzima

56' Mins | beki Juma ramadhani anafanya kazi ya ziada kuokoa mpira mzuri wa Niyonzima langoni mwake

55' Mins | krosi nzuri ya Niyonzima, Msuva akiwa katika nafasi nzuri lakini anashindwa kulenga. Beki wa kati wa Kagera wanaonekana kama kuzubaa hivi

54' Mins| Mbuyu Twite anaingia kuchukua nafasi ya Kessy ambaye ameumia

52' Mins | Kessy wa Yanga yuko chini akipatiwa matibabu, anatolewa nje

51' Mins | Msuva anagongeana vizuri na Niyonzima ambaye anapiga shuti kali lakini hakulenga lango

50' Mins | Msuva anaingia vizuri lakini badala ya krosi anajaribu kupiga shuti na mpira unatoka juuuu, goal kick

48' Mins | Mbaraka Yusuf anaunganisha pasi fupi ya Mangoma na kuifungia Kagera Sugar bao la pili katika mchezo wa leo. Huyu ndiye aliyefunga bao la kwanza

47' Mins | Ngoma anaingia vizuri lakini anageuka na kumpa pasi Niyonzima, lakini mpira wake unakuwa laini

46' Mins | Mpira umeanza taratibu Kagera wakigonga pasi nyingi fupifu

Second Half | Kagera Sugar 1 - 3 YoungAfricans

HALF TIME | Kagera Sugar 1 - 3 YoungAfricans

45' Mins | Yanga wanaonekana kuupoza mchezo na hawana haraka hata kidogo, wanagongeana taratibu kabisa hapa

40' Mins | Yanga wanagongeana vizuri, Mwinyi anapiga krosi tamu kabisa lakini Juma ramadhani anawahi kuokoa na kuwa kona. Inachongwa tena, haina manufaa

38' Mins | Dida anafanya kazi ya ziada, anatoka nje ya 18 na kuokoa mpira miguuni mwa Ally

37' Mins | Chirwa anaingia na kumdhibiti Juma Ramadhani, anatoa krosi safi kwa MSuva ambaye anapiga shuti, wanaokoa na kuwa kona. Inachongwa na Niyonzima lakini haina matun

35' Mins | Kessy analambwa kadi ya njano kwa kumchezea rafu Taita

33' Mins | Ngoma na Msuva wanagongeana vizuri na krosi safi lakini Burhani anaokoa vizuri kabisa

31' Mins | Kagera wanamuingiza Ali Ramadhani kuchukua nafasi Japhet Makaray, Pia wanamtoa kipa Casillas na nafasi yake inachukuliwa na David Burhani

30' Mins | Kagera wanaonekana kuwa wamepaniki sasa na wanakaba kibabe jambo ambalo linaweza kuwasumbua au kuwaponza kupata kadi

28' Mins | Yanga wanaonekana wanaendelea kushambulia kwa kasi zaidi wakiwapa Yanga

26' Mins | Gooooooal obrey chirwa anaipatia Yanga goli la Tatu

23' Mins | Selemani Mangoma wa Kagera analambwa kadi ya njano kwa kumuangusha Ngoma kwa makusudi
21' Mins | Niyonzima anageuka na kupiga shuti kali, Casillas anatema na Msuva anamalizia safi kabisa na kuiandikia Yanga bao la pili


15' Mins | Ufudu wa Kagera anafanya kosa hapa, anaingia Chirwa hatari lakini Juma Ramadhani anawahi na kuondosha hatari hiyo

14' Mins | mpira zaidi unachezwa katikati ua uwanja na inaonekana timu zina nafasi ya kugongeana kwa kuwa uwanja ni safi kabisa

9' Mins | Japhet Makalay anaingia vizuri baada ya kumtoka Kessy lakini krosi yake inaishia mikononi mwa Dida

8' Mins | Msuva anaingia tena, krosi safi kabisa hatariiii lakini Casillas anatokea na hudaka vizuri kabisa

6' Mins| Mangoma wa Kagera anaingia vizuri anaachia shuti kali kabisa lakini ni goal ki

5' Mins | GOOOOOOOO Ngoma anaifungia Yanga bao la kusawazisha baada ya kufunga kwa kichwa akiunganisha krosi safi ya Simon Msuva

3' Mins | GOOOOOOOOOO Mbaraka Yusuf anamtoka Yondani na kuachia mkwaju mkali unaomngonga Dante na kumpoteza maboya kipa Dida na unajaa wavuni

1' Mins | Yanga wanaonekana kuanza kwa kasi kama wamepanga kupata bao la mapema ikiwezekana kumaliza kazi mchezo



Kikosi cha Yanga SC leo dhidi ya Kagera Sugar

1. Deogratius Munishi
2. Hassani Kessy
3. Mwinyi Haji
4. Andrew Vicent
5. Kelvin Yondani
6. Thabani Kamusoko
7. Saimoni Msuva
8. Haruna Niyonzima
9. Donald Ngoma
10. Obrey Chirwa
11. Deusi Kaseke

Akiba
- Beno Kakolanya
- Oscar Joshua
- Vicent Bossou
- Mbuyu Twite
- Geofrey Mwashuiya

- Mateo Antony

Credit: Saleh Jembe Blog
 
Kagera Sugar piga mbwaa/chura wa kaunda...Yanga kufungwa ni lazima
 
Yellow card Selemani Mangoma kwa kumchezea rafu Donald Ngoma
 
Tunajua Kuwa Chaneta FC wana Ngoma! Lakini Kagera Sugar Vaeni Condom Muwagonge Hao Chaneta FC....
 
31' Mins | Kagera Sugar 1 - 3 Young Africans

03' Mbaraka Yusuph (Kagera Sugar)
05' Donald Ngoma (Young African)
21' Simon Msuva. (Young African)
26' Obrey Chirwa ( Young African)
 
Kwa mwendo huu wakununua makipa,basi yanga bingwa.
 
41' Mins | Kagera Sugar 1 - 3 YoungAfricans

03' Mbaraka Yusuph (Kagera Sugar)
05' Donald Ngoma (Young African)
21' Simon Msuva. (Young African)
26' Obrey Chirwa ( Young African)
 
Back
Top Bottom