Freeland
JF-Expert Member
- Jan 24, 2012
- 14,481
- 10,227
Nashukuru sana kwa kukubaliana na low competency ya marefa wetu. Sisi Yanga tunapowalalamikia msiwe mnatuzodoa bali tuungane pamoja ili haki itendeke uwanjani kwa maslahi na mustakabali wa soka letu. Muda wa kuchekekelea mtu kuumizwa maadam ni wa timu pinzani umepita.
Mkuu pamoja na kwamba tunakubaliana wote kuwa soka ni mchezo wa amani,Upendo
Ndio essence ya Fair Play.Nakataa kabisa watu kuumizana kwa faulu zisizo za kimpira na waamuzi wasifanye kitu
Kitu ninachokipinga katika suala lenu la Tambwe ni kwamba limeamuliwa kisiasa.....Maamuzi yale yangefanywa bila kukurupuka...ripoti ya kamisaa ingesubiriwa.
Kwa minajili hiyo maaamuzi yale yalifanywa kwa kuzingatia picha mnato kwenye gazeti la championi tu.Picha mnato haziwezi kusema kila kitu.
Maamuzi ya kukurupuka kwa sababu tu Yanga wamelalamika.
Na hicho ndicho Sisi watu wa Simba tuakipinga